Huu uzi ningekutana nao mwezi ulopita,ningekupa deal. Kuna mtu anatuletea mayai ya kienyeji ofisini tray 12000, ametushika staff wote. Jamaa anapiga hela. Pole lkn pambana.
 
nimenunua huyo kuku wa kienyeji aliyefugwa mjini kwa kweli ni hasara tupu.mgumu ladha 0 ,bei ghali sana nikajilaumu sana.bora ningechukua wa kisasa nijue moja
 
Huyo wa trey 12,000 niunganishe nami awe ananiletea. Wengi wanauza 16,000 hadi 18,000. Note watanzania tunapenda vitu vya bei rahisi.....
Sawa ntafanya hivo. Na akiishiwa mayai, mimi huwa nayafuata Magomeni sokoni, pale usalama, reja reja wanauza moja 500, huwa nachukua tray2 kwa Tshs 25000-27000
 
Pole kaka... lakn usikate tamaa, kila kitu kina changamoto zake ,hata hao wa mayai kuna kpnd masoko yanasumbua, inafikia kpnd wanauza mayai kwa bei ya hasara maana hayakai muda mref ukilinganisha na ya kienyej.
Komaa kutafuta soko zur ,,never give up
 
Kama unafuga mjini bado sio sababu ya kukosa soko,ingia gharama wapatie vitu vya kuwafanya wawe wa kienyeji,wape majani kwa wingi,hata kama ya kununua,mm kuku wangu nawanunulia fungu moja la mchicha au spinachi kila siku.

Mm nauza tray 10,000,hlf nikuhakikishie,soko la kienyeji liko tyr kuliko hao wa kisasa,achana na wateja wanaosumbua,km mtu ana swali mweleweshe km haelewi achana nae,kwa changamoto zilizopo kiafya watu wanapenda mayai ya kienyeji,unless km hao kuku huwafugi kienyeji,ie kuwafungulia watoke nje wajitafutie na ww kuwapa nyongeza kidogo ya chakula hada majani.
 
Wana JF habari zenu?

Kwanza nianze kwa kumshukuru Mungu kwa Karama ya Ufugaji aliyonijalia.
Mimi ni mfugaji wa Kuku wa kienyeji,nilianza mwaka 2011 na Tetea 2 kwasasa nna Tetea wakubwa 100,Majogoo 20,Vifaranga vya miezi miwili 59,Vifaranga vya Wiki moja 50.
Hao Tetea na majogoo kwasasa wana miezi 7,Tetea ndo wameanza kutaga,kwasasa nakusanya Trei 1.5 kila siku,plan zangu wafikishe Trei 2 Kila siku ili Trei moja Igharamie Chakula chao na dawa,Trei nyingine iwe ni kama faida ya kunisaidia kutunza Vifaranga.
Ila Changamoto iliyonifanya niandike uzi huu ni Ukosefu wa Soko la uhakika la Mayai ya Kienyeji.Na kwa wachache nnao wapata nakutana na majibu haya:
"Mh! Haya mayai ya Kienyeji?,mbona mengine makubwa kama ya kisasa?.Mh! Kiini chake mbona sio njano sana?,au yamechakachuliwa,Afu mayai ya kienyeji huwa na ganda jeupe nje yakwako mbona mengine brown?Hao kuku umefugia wapi kama ni hapa mjini Hakuna kuku wa kienyeji wote wamechakachuliwa"
Kiukweli majibu haya yananikatisha tamaa sana mpaka najiona niliingilia mlango wa kutokea,Kuku nimewafuga kwa shida sana mpaka walipofikia,nilijua huu utakuwa muda kupumua baada ya kaz ngumu,matokeo yake nimekutana na Changamoto ya Soko la mayai,ambayo ndo Msingi wa faida ya mfugaji yeyote yule.Na mimi nna rafiki yangu amefuga kuku wa kisasa yaani mwenzangu saizi anapiga pesa ni balaa,sababu ni kwamba mwenzangu Soko lipo nje nje tu.
Na Kiukweli kama wana JF,hamtonisaidia kuikabili Changamoto hii naapa Kuwauza kuku wa Kienyeji wote,na nianze kufuga wa Kisasa.Sababu ni kwamba Watanzania tunapenda vitu vya Bei rahisi hata kama vina Athari kwa afya zetu.Tathmin yangu butu inanionesha kuwa Mayai ya kisasa yanaliwa na watu wengi zaidi kuliko ya Kienyeji.

Naombeni msaada wa Soko kwa anaelifaham,au nihamie Upande wa pili!
Hongera kwa kujiajiri
Na pole kwa changamoto bro
Ila usikate tamaa na hzo changamoto
Mimi kama mtaalamu wa Mifugo nakushauri mambo yafuatayo
1.Chagua mbegu bora ya kuku ili uweze kuzalisha mayai ya aina moja
2.Zingatia chakula bora ili kukabiri soko mfano mahitaj ya kiin cha njano na ukubwa wa mayai
3.Ili ukaribiane na changamoto ya kupata hasara jitahid kufuga kuku mchanganyiko yaani wa kienyeji na wa kisasa ili uzibe mwanya wa mashindano ya soko lako
4.Boresha lugha ya kibiashara ili uwavutie wateja wako
Mwisho tutazid kuwa pamoja
By animal scientist
 
Hongera kwa kujiajiri
Na pole kwa changamoto bro
Ila usikate tamaa na hzo changamoto
Mimi kama mtaalamu wa Mifugo nakushauri mambo yafuatayo
1.Chagua mbegu bora ya kuku ili uweze kuzalisha mayai ya aina moja
2.Zingatia chakula bora ili kukabiri soko mfano mahitaj ya kiin cha njano na ukubwa wa mayai
3.Ili ukaribiane na changamoto ya kupata hasara jitahid kufuga kuku mchanganyiko yaani wa kienyeji na wa kisasa ili uzibe mwanya wa mashindano ya soko lako
4.Boresha lugha ya kibiashara ili uwavutie wateja wako
Mwisho tutazid kuwa pamoja
By animal scientist
Umesomeka mkuu,ila hyo namba 3,nimeielewa sana.
 
Kama unafuga mjini bado sio sababu ya kukosa soko,ingia gharama wapatie vitu vya kuwafanya wawe wa kienyeji,wape majani kwa wingi,hata kama ya kununua,mm kuku wangu nawanunulia fungu moja la mchicha au spinachi kila siku.

Mm nauza tray 10,000,hlf nikuhakikishie,soko la kienyeji liko tyr kuliko hao wa kisasa,achana na wateja wanaosumbua,km mtu ana swali mweleweshe km haelewi achana nae,kwa changamoto zilizopo kiafya watu wanapenda mayai ya kienyeji,unless km hao kuku huwafugi kienyeji,ie kuwafungulia watoke nje wajitafutie na ww kuwapa nyongeza kidogo ya chakula hada majani.
Ahsante kwa wazo,mimi nauza kwa 12,000 nilichojifunza kwako suala la bei.Nadhani natakiwa nipunguze bei kidogo ili niwe kwenye mzunguko wa haraka.
 
Pole sana, mimi ninao 30 nilipitia changamoto hizo, nikaamua niwe nawapa majani kwa wingi, taratibu kiini kikaanza kuwa cha njano. Ila kiukweli soko la mayai ya kienyeji sio la wazi...hii pia ikanifanya kufuga kuku wa mayai ya kisasa. Mayai ya kisasa yanasoko linaloonekana na pia yanawalaji wengi.
Ushauri, uwape kuku majani kwa wingi, Pia jitahidi kutafuta soko katika maofisi mbali mbali kwa Dar ukiuza tray 12,000 lazima yatoke.
 
Pole sana ndugu. Kweli kuna changamoto kwenye soko. Niliwahi kupata shida ya kuuza mayai ya kienyeji. Tafuta mahali watakapokuamini uuze. Tafuta bank, hospitali, sehemu yenye wafanyakazi supply hapo mara kwa mara. Ukiweza tafuta mteja atakayechukua kwa bili na mpelekee mayai fresh. Mimi nafuga kwale na nauza mayai kwa bili sihangaiki na soko. Usiuze reja reja niliwahi kusumbuka kila mtu anakugongea geti anataka yai moja mawili, matatu ni usumbufu. Pia tumia unaweza kutumia njia ya kubadilishana. Mimi mayai yangu ya kienyeji nampa mtu wa gengeni hela sichukui nachukua bidhaa kama nyanya, mboga mboga, na mahitaji mengine.
 
Pole sana ndugu. Kweli kuna changamoto kwenye soko. Niliwahi kupata shida ya kuuza mayai ya kienyeji. Tafuta mahali watakapokuamini uuze. Tafuta bank, hospitali, sehemu yenye wafanyakazi supply hapo mara kwa mara. Ukiweza tafuta mteja atakayechukua kwa bili na mpelekee mayai fresh. Mimi nafuga kwale na nauza mayai kwa bili sihangaiki na soko. Usiuze reja reja niliwahi kusumbuka kila mtu anakugongea geti anataka yai moja mawili, matatu ni usumbufu. Pia tumia unaweza kutumia njia ya kubadilishana. Mimi mayai yangu ya kienyeji nampa mtu wa gengeni hela sichukui nachukua bidhaa kama nyanya, mboga mboga, na mahitaji mengine.
Mayai ya kwale soko kuu ni kwenye vitengo, tatizo ukitoka pale washikaji wakikuona wanaweza pakazia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom