Biashara ya shule za private kwa kidato cha V yaingia mdudu

Feb 8, 2012
92
8
Kutokana na matokeo mabovu ya form IV mwaka 2011,shule za private zimekosa wanafunzi wa kidato cha tano mwaka huu (2012) kwa idadi wanayoihitaji.Baadhi ya shule imepokea mpaka wanafunzi watatu mpaka 10.Hali hii imetokana na matokeo yasiyoridhisha ya kidato cha tano ingawa serikali imejitapa kwamba kiwango cha ufaulu kimeongezeka.Kilichoongezeka hapa ni division IV na kupungua zero.Wamiliki wa shule hizo za private wameonekana kuchanganyikiwa kwani hata hao wanafunzi wachache wenye div1 mpaka III wanagombeana na shule za serikali.Kuna baadhi ya shule za serikali zimekosa kabisa wanafunzi wa kujiunga kidato cha tano,baadhi ya shule hizo zimeaghirisha kuchukua baadhi ya michepuo kutokana na matokeo mabovu ya kidato cha nne.Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2012 watatangazwa hivi karibuni.
 
Kuna siku yaja navvyo vyuo vikuu vitakosa wanafunzi wa mwaka wa kwanza.Hili ni tatizo la kutokuwa na mfumo mzuri wa utoaji wa Elimu tulio nao TZ
 
Back
Top Bottom