Biashara ya Ngono jijini Dar inatisha, yazidi kunawiri

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
48,777
102,139
Kahaba.jpg

Jana tulianza kuchapisha makala maalum kuhusu kushamiri kwa biashara ya ukahaba kwenye maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, katika uchunguzi huo imebainika kuwa, kuna kushamiri zaidi kwa watoto wadogo chini ya miaka 18 kujiingiza kwenye biashara hiyo haramu.

Timu ya waandishi wa Mwananchi imefika katika maeneo na kuzungumza na watu mbalimbali, wakiwemo wahusika ambao wameeleza masaibu wanayokutana nayo. Endelea

Ushuhuda wa wahusika

Mmoja wa makahaba wanaojiuza kwenye baa moja maarufu maeneo ya Manzese akijitambulisha kwa jina la Jack (28), alizungumza na gazeti hili na kubainisha kuwepo kwa makahaba walio na umri chini ya miaka 18, lakini akasema ni vigumu kuwabaini kwa sababu ya muonekano wa maumbile yao kufanana na watu wazima.

Anasema makahaba wanaoonekana wadogo huwa wanafukuzwa wanapojaribu kuingia katika baa hiyo, lakini wenye maumbo makubwa wanaruhusiwa kuingia.

“Ni vigumu kujua kama huyu ana umri chini ya miaka 18, lakini wale ambao wanaonekana wadogo huwa wanafukuzwa hapa. Wakiondoka unakuta wanarudi tena na kuendelea na biashara kama wengine,” alisema Jack.

Kahaba huyo anaeleza kwamba anafanya biashara hiyo kwa sababu hana shughuli nyingine ya kumwingizia kipato cha kukidhi mahitaji yake ya kila siku.

Anasema wale wateja wa haraka (short time) wanalipia Sh7,000 hadi Sh10,000 ambapo Sh2,000 wanalipia chumba kwa kila anapoingiza mwanamume na kwa siku za wikiendi anaweza kuwahudumia wanaume kati ya 15 hadi 20. “Siku za kawaida hakuna watu wengi, naweza kupata Sh40,000 hadi Sh50,000 lakini siku za wikiendi nafikisha Sh100,000 mpaka Sh150,000,” anasimulia kahaba huyo ambaye alianza biashara hiyo miaka miwili iliyopita.

Ndani ya baa hiyo (jina linahifadhiwa) kuna vyumba vya kulala takribani vinane ambavyo ndani yake kuna kitanda kwenye kila chumba na kapu la taka. Vyumba hivyo ndiyo vinatumiwa na makahaba hao kwa huduma za haraka, lakini pia kuna vyumba maalumu (VIP) ambavyo viko sehemu tofauti ndani ya baa hiyo na bei yake ni tofauti.

Majirani katika maeneo ambayo biashara hizo zinafanyika wanasema makahaba hao wanawaharibu kimaadili watoto wao kwa sababu wanaona wanachofanya na wao wanaiga, jambo ambalo ni hatari kwa maisha yao.

Kwa upande wake, mkazi wa mtaa wa Mnazi Mmoja, Kuluthum Mrisho alisema wanaishi nao hivyo hivyo kwa sababu nyumba yao ipo katika eneo hilo na hawana sehemu nyingine ya kwenda.

“Sisi tulishawazoea, kila mtu na maisha yake. Tutafanya nini, tutakwenda wapi baba yangu,” anasema mwanamke huyo.

Mwananyamala ‘Kwa Wahaya’

Mkazi wa Mwananyamala, Ramadhani Juma anasema eneo la Mwananyama maarufu kama “Kwa Wahaya” ni la muda mrefu na lilianza miaka ya 1980 walipohamia hapo kutoka Kisutu.

Anasema wanawake hao hawakuanza biashara hiyo hivi karibuni, bali walianza zamani kwa kuwafurahisha wanajeshi wa jeshi la kikoloni wakati huo.

“Hawa wanawake walihamia hapa miaka ya 1980 wakitokea mjini karibu na soko la Kisutu, hawa walikuwa pale kwa ajili ya kuwafurahisha wanajeshi wa kikoloni, siku zilivyozidi kwenda walihamia maeneo mengine,” alisema Ramadhani.

Alisema hadi eneo hilo linaanzishwa ni kwa sababu wapangaji walikuwa wanasumbua kulipa kodi, lakini kwa hawa makahaba, mwenye nyumba anakuwa na uhakika wa kulipwa bila usumbufu. “Wapangaji hawa hawasumbui katika suala la kodi, kama ni kwa mwezi au miezi sita uhakika wa kulipa upo tofauti na wengine inapofika wakati wa kulipa wanasumbua,” alisema.

“Binafsi namfahamu rafiki yangu alikuwa na nyumba ya kawaida yenye vyumba vitano, kutokana na kusumbuliwa na wapangaji aliamua kugeuza vyumba vidogo vidogo na kuwapangisha makahaba hao.

“Hii biashara ilianza kwa nyumba moja, kadri siku zilivyozidi kwenda watu wengine walinunua nyumba na kuzifanya hivyo, lengo ni kuachana na usumbufu wa kodi, kwani hawa wana uhakika wa kulipa,” alisema.

Juma alibainisha kuwa wanaofanya biashara hiyo wamekuwa wakipanga vyumba hivyo na umri unapokwenda wamekuwa wanawapangisha watu wengine.

Chanzo: Mwananchi
 
Ni hatari sana na wanaume wanaonunua wana roho ngumu na hawana kinyaa yaani unajua kabisa unaweza ukawa ni 13 hivi kwa siku hiyo na bado unaenda na wewe sehemu walipotoka wenzio
Hata walio oa hivyo hivyo

Unakuta mwanamke katoka kuchepuka na li jamaa anarudi kwa mme wake jioni na mme wake kwa kutaka kumfurahisha mkewe anataka kulamba na papuchi

Hapo na mkewe anakubali daah uchafu huu
 
24 Reactions
Reply
Back
Top Bottom