Biashara ya mobile toilets kwenye foleni dar

blessings

JF-Expert Member
Jul 9, 2012
6,983
6,237
Wadau nimekuja na wazo la kuanzisha mobile toilets pembezoni mwa barabara zenye foleni sana hapa Dar maana nimefanya uchunguzi nimegundua kuna uhitaji mkubwa. Hasa mida ya jioni kuanzia saa 9 k kuanzia nitaweka Maeneo ya Ubungo Mataa, Ubungo Kibo, Mwenge Mataa, Kona ya Clouds/Mikocheni, Jangwani & TAZARA.Tutunze Usafi Jijini kwa kutojisaidia vyo.
 
Jiji watakunyima kibali mpaka uwambie ulaji wao utakuwa kiasi gani.

Maana mamlaka zetu kichefu chefu
 
Hapo andaa hela ya Meya, Engineer wa Manispaa, madiwani, DED, Mkuu wa Wilaya ndo utapata kibali vinginevo andik umeumia
 
Idea nzuri sana. ungeweza hata fanya 200 kwa 500. Kumbuka unafuel costs za kusogeza hivyo vyoo.
Tatizo sasa nchi yetu hii, ni kama wadau walivosema hapo.
Watu wanakuwa na ideas nzuri zakutatua matatizo ila wanaona haiwezekani ukafaidika bila kitu "kidogo". Sio siri mimi nimetulia kwanza na simple idea zangu za kujaribu kurahisisha mambo mijini maana nilihisis nazeeka kabla ya siku zangu halafu nikaona nitakuja kuidharau sana ngozi yangu sababu ya ujinga wa wachache wacha wenye exposure waongezeke kidogo.
 
jitahidi usafi maaana dah vile huwa vinanuka sana hasa mtu akiwa anashusha mzigo huko ndani hadi nje ukipita vina kismell flan hv
 
Mkuu hivyo vinyesi utakuwa unavibebaje kila siku baada ya kufunga biashara?
 
Wadau nimekuja na wazo la kuanzisha mobile toilets pembezoni mwa barabara zenye foleni sana hapa Dar maana nimefanya uchunguzi nimegundua kuna uhitaji mkubwa. Hasa mida ya jioni kuanzia saa 9 k kuanzia nitaweka Maeneo ya Ubungo Mataa, Ubungo Kibo, Mwenge Mataa, Kona ya Clouds/Mikocheni, Jangwani & TAZARA.Tutunze Usafi Jijini kwa kutojisaidia vyo.

Hahaha, wazo tamu sana hili, kama unaiogopa serikali endelea kuwaogopa hivyohivyo ili sisi wanazi tuibe wazo uone vyoo vimezagaa mitaa yote muhimu! Halafu kuna dada yangu huwa anakodisha hivi vyoo kwenye functions mbalimbali, au ndiyo wewe?
 
attachment.php

Hii picha nimeikuta kwa Mdau wa JF inaweza saidia biashara yako?
kujisaidia ni kiu cha faragha sasa km ni kwenye foleni sijui km unaweza pata wateja bila ya kuwasitiri ili wasitiri maungo yao ya utupu na kujiswafi
 
Back
Top Bottom