chapanga01
Senior Member
- Apr 10, 2020
- 102
- 75
Habari wana jamvi.
Kifupi mimi ninaelimu ya chuo kikuu nilimaliza 2013, Ila kiuhalisia mimi sipendi kuajiriwa pia sipendi kupangiwa napenda kujiajiri.
Mwaka 2014 nilikuwa nimeajiriwa kampuni flani hapa Dar nilifanya hadi mwaka 2015 nikaachishwa kazi kwa vile Bosi alinishtukia kwamba napiga dili namuibia tenda zake kisha nafanya bifasi.
Ila kipindi ananifukuza nilikuwa na 5m nikarudi nyumbani nikawa nanunua mpunga na kukoboa nauza mchele wazo langu nifungue duka la nafaka Dar.
Mzigo wa mwisho niliponunua nikaweke godown, Nisubiri muda nije kuukoboa nibebe mchele nilete kwenye flame ambayo ningepanga Dar
Ila kabla sijafungua ule mzigo pale mashineni ukauzwa na msimamizi wa mashine na akatoroka.
Hapo ndio plan yangu ikafa maana Bosi wa mashine akawa ananilipa kidogokidogo ambayo pesa ikawa haitunziki.
Nikarudi tena kwenye ajira hadi sasa ila mpango wangu bado upo vilevile sasa nafanya kazi pia nalima mwisho nifungue duka langu la mchele.
Shida yangu je naweza pata mtu mzoefu wa biashara ya mchele humu ili anifundishe mambo yanayonisumbua kichwani mwangu.
Kifupi mimi ninaelimu ya chuo kikuu nilimaliza 2013, Ila kiuhalisia mimi sipendi kuajiriwa pia sipendi kupangiwa napenda kujiajiri.
Mwaka 2014 nilikuwa nimeajiriwa kampuni flani hapa Dar nilifanya hadi mwaka 2015 nikaachishwa kazi kwa vile Bosi alinishtukia kwamba napiga dili namuibia tenda zake kisha nafanya bifasi.
Ila kipindi ananifukuza nilikuwa na 5m nikarudi nyumbani nikawa nanunua mpunga na kukoboa nauza mchele wazo langu nifungue duka la nafaka Dar.
Mzigo wa mwisho niliponunua nikaweke godown, Nisubiri muda nije kuukoboa nibebe mchele nilete kwenye flame ambayo ningepanga Dar
Ila kabla sijafungua ule mzigo pale mashineni ukauzwa na msimamizi wa mashine na akatoroka.
Hapo ndio plan yangu ikafa maana Bosi wa mashine akawa ananilipa kidogokidogo ambayo pesa ikawa haitunziki.
Nikarudi tena kwenye ajira hadi sasa ila mpango wangu bado upo vilevile sasa nafanya kazi pia nalima mwisho nifungue duka langu la mchele.
Shida yangu je naweza pata mtu mzoefu wa biashara ya mchele humu ili anifundishe mambo yanayonisumbua kichwani mwangu.