Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu ushauri mzuri sana, nakufuata pmMkuu hiyo biashara ni nzuri sana tatizo linokuja kudhoofisha biashara ni suala la Parking ya nyama
Changamoto kubwa hiko hapo bado wa Tz hatuwezi ku design parking nzuri ya product kama ya nyama ndio maana katika Supermarket zetu wanauza sana nyama ya Nje kwasababu ina kidhi viwango vya kimataifa
Ushauri wangu
1 Jenga banda sehemu yenye ardhi ya kutosha ambayo pia kuwe na Majani ya kutosha ( ranch kidogo hivi unakipiga na fensi)
2 Jenga Machinjio madogo ya kisasa
3 Tafuta alternative source of energy usitegemee umeme wa tanesco kwa sababu bucha za kisasa zinatumia mashine kukatia nyama na sio vigogo na hizo mashine zinatumia umeme kwaiyo ukitegemea umeme wa Tanesco unaweza ukakaa siku bila kufanya kazi
4 Kuusu Parking nenda TFDA kuna wataalam watakupa ushauri wa jinsi gani unaweza kufanya parking ya International standard
5 Usikope hela bank kwaajili ya kuanzisha biashara hii inaweza ikakugharimu biashara ikawa ngumu mwanzoni alafu jamaa wakaanza kukuchachamalia mwishowe ukamwaga manyanga
6 Fanya Study tour nakushauri nenda pale SUA ( Moro) yuko Professor mmoja Ana mradi mkubwa wa hii kitu na anapiga hela ndefu sana atakupa muongozo wa kila kitu usitegemee ushauri wa hapa Jf tu
Sent using Jamii Forums mobile app
Ahsante kaka, ni miundo mbinu ipi ya ziada inayohitajikaKama unaweza kufanya kila kitu kinachohitajika kwenye biashara hii kikamilifu, ni biashara nzuri. Unapaswa kuwa na mabucha yako, machinjio, maduka au wateja kama supermarkets. Pia unapaswa kuweza kukata nyama kitaalamu kwa kutumia machine na kuzipaki vizuri. Pia usisahau kwamba utahitaji freezers kubwa kuweza kuhifadhi nyama kabla ya kuuza.
Biashara hii inahitaji uwe na gari/magari yako, moja la kubeba ng'ombe na jingine kusafirisha nyama kwa wateja. Vyote hivi vinahitaji uwekezaji mkubwa.
Sikushauri uanze na ng'ombe 60 ni wengi mno kama huna miundombinu na nyenzo nyingine utapata shida na pengine hasara.
Thanks tataBinafsi sijawahi kuona biashara ya nyama ikimtupa mtu. Labda ka wale wenzangu na mimi wanaonunua ng'ombe "cheap" wa wizi
Sawa mdadaChagua kati ya mikoa hii mifugo mingi manyara,shinyanga, tabora huko mwanza
all the best
Huyu kadata na harufu ya utumbo kabla hajaanza kuuza nyama.Hutaki ushauri...Ila kubadilishana mawazo??
😂😂😂😂😂viatu stakki mimi...lolHuyu kadata na harufu ya utumbo kabla hajaanza kuuza nyama.
Hutaki nini utumbo au bucha?viatu stakki mimi...lol
Uchokozi wako...Hutaki nini utumbo au bucha?
Pole sana.Uchokozi wako...
Ndio,najua watu watanikejeliHutaki ushauri...Ila kubadilishana mawazo??
Nimekuelewa mkuu asanteKuwa makini sana mnadani unaweza kuta ng'ombe mkubwa sana ila uzito ni 87kg