Habari zenu wakubwa. naomba ushauri wa biashara ya kufanya,mimi ni kijana niliye graduate mwaka huu ila mpaka sasa sifikirii kuajiriwa nahitaji kujiajiri mwenyewe ili baadaye na mimi nitoe ajira kwa watanzania wenzangu,nimejikusanya na kupata million 3.5 ,kabla ya hapa nlifikiria biashara ya kufuga kuku wa kienyeji kutokana na capital yangu lakini tatizo likawa ni market kwa hao kuku kama kwenye mahotel makubwa n.k,kama mtu anaweza kunipa ushauri ni biashara gani nyingine inaweza kunikomboa kwa kutumia mtaji wangu mwenyewe.