Biashara ya bodaboda imeua ndoto za vijana wengi

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,684
36,045
Habari!

Hapa naomba tuelewane kuwa sizungumzii pesa bali nazungumzia ndoto za vijana katika kuliinua taifa na familia zao.

Pamoja na kazi ya bodaboda kuwapatia kipato vijana na baadhi ya wazee ambao wanaifanya hiyo biashara lakini imechochea uchumi wa China na India kwa kiasi kikubwa.

Hapa kwa lugha rahisi niseme bodaboda Afrika wanatimiza ndoto za vijana wa India na Uchina kwa kuwafanya mabilionea kila siku.

Ukikaa bandarini na kuona maelfu ya pikipiki zinazoingia kwa siku utajua kuwa huko China na India wamejipanga kukusanya mabilioni.

Twende kwenye point.
Biashara ya bodaboda ina kilevi ndani yake, kila anayeingia anaingia kwasababu za kukwama akijisemea moyoni kuwa nafanya mwaka mmoja tu, au nafanya ili nitimize jambo hili tu kisha niache nirudi kwenye ndoto zangu.
Lakini ni kama 0.001% ndio wanaweza kurudi kwenye ndoto zao, wengi humezwa jumla. Wakikatika miguu huwapa mzigo mama zao maskini walioko kijijini.

Ndoto za kuwa madaktari. Ndoto za kuwa walimu. Ndoto za kubuni viwanda vidogo. Ndoto za kumiliki Education center na baadaye shule.

Nakadhalika, nakadhalika, zimemezwa na vijiwe vya bodaboda. Wanasiasa wanalitumia kundi hili kujiimarisha kisiasa.

Hata Wamachinga wengi pia wanatimiza ndoto za vijana wa Kichina kwa kuuza bidhaa za China.
 
Habari!

Hapa naomba tuelewane kuwa sizungumzii pesa bali nazungumzia ndoto za vijana katika kuliinua taifa na familia zao.

Pamoja na kazi ya bodaboda kuwapatia kipato vijana na baadhi ya wazee ambao wanaifanya hiyo biashara lakini imechochea uchumi wa China na India kwa kiasi kikubwa.

Hapa kwa lugha rahisi niseme bodaboda Afrika wanatimiza ndoto za vijana wa India na Uchina kwa kuwafanya mabilionea kila siku.

Ukikaa bandarini na kuona maelfu ya pikipiki zinazoingia kwa siku utajua kuwa huko China na India wamehipanga kukusanya mabilioni.

Twende kwenye point.
Biashara ya bodaboda ina kilevi ndani yake, kila anayeingia anaingia kwasababu za kukwama akijisemea moyoni kuwa nafanya mwaka mmoja tu, au nafanya ili nitimize jambo hili tu kisha niache nirudi kwenye ndoto zangu.
Lakini ni kama 0.001% ndio wanaweza kurudi kwenye ndoto zao, wengi humezwa jumla. Wakikatika miguu huwapa mzigo mama zao maskini walioko kijijini.

Ndoto za kuwa madaktari. Ndoto za kuwa walimu. Ndoto za kubuni viwanda vidogo. Ndoto za kumiliki Education center na baadaye shule.

Nakadhalika, nakadhalika, zimemezwa na vijiwe vya bodaboda. Wanasiasa wanalitumia kundi hili kujiimarisha kisiasa.

Hata Wamachinga wengi wana wanatimiza ndoto za vijana wa Kichina kwa kuuza bidhaa za China.
Sasa unashauri nini kifanyike?
 
Nilishasema bodaboda na machinga wanakuza uchumi wa china, kama madalali wa viwanda vya china. China inafaa izifutie madeni nchi za Afrika sababu mikopo yao ujilipa yenyewe kupitia bodaboda na machinga.
 
Lakini ni kama 0.001% ndio wanaweza kurudi kwenye ndoto zao, wengi humezwa jumla. Wakikatika miguu huwapa mzigo mama zao maskini walioko kijijini.

Ndoto za kuwa madaktari. Ndoto za kuwa walimu. Ndoto za kubuni viwanda vidogo. Ndoto za kumiliki Education center na baadaye shule.

Nakadhalika, nakadhalika, zimemezwa na vijiwe vya bodaboda. Wanasiasa wanalitumia kundi hili kujiimarisha kisiasa.
 
Sio kila anayeibua tatizo anapaswa kutoa suluhisho. Hata wewe msomaji unaweza kuonyesha njia ya kutoka
Kuna Jamaa Alianza na kuendesha boda Muda huu ana gari nzuri na bajaji kadhaa na boda pia kawapa vijana wanatafuta ugali

Life is pray more + hard work na kijitambua


Jambo la msingi ni kuhakikisha vijana wanajitambua kwanza Hilo ndo Jambo la msingi kuzidi yote
 
Kuna Jamaa Alianza na kuendesha boda Muda huu ana gari nzuri na bajaji kadhaa na boda pia kawapa vijana wanatafuta ugali

Life is pray more + hard work na kijitambua


Jambo la msingi ni kuhakikisha vijana wanajitambua kwanza Hilo ndo Jambo la msingi kuzidi yote
Hujui jinsi anavyopata pesa.
Wewe akikusimulia atakusimulia njia ile unayoijua wewe tu.
Go and try it.
 
Tujenge viwanda vikubwa vya kimkakati kuinua uchumi wa vijana miaka mingi vijana hawajapata ajira. Serikali iajili Kwa sasa na pia sector binafsi zipewe uwezo zitoe ajila kuisaidia Serikali ni kweli bodaboda imekua shimo Kwa vijana wengi.
 
Tujenge viwanda vikubwa vya kimkakati kuinua uchumi wa vijana miaka mingi vijana hawajapata ajira. Serikali iajili Kwa sasa na pia sector binafsi zipewe uwezo zitoe ajila kuisaidia Serikali ni kweli bodaboda imekua shimo Kwa vijana wengi.
Viwanda Gani vya kimkakati....
 
Tujenge viwanda vikubwa vya kimkakati kuinua uchumi wa vijana miaka mingi vijana hawajapata ajira. Serikali iajili Kwa sasa na pia sector binafsi zipewe uwezo zitoe ajila kuisaidia Serikali ni kweli bodaboda imekua shimo Kwa vijana wengi.
Tena shimo kubwa.
Wanazingua kutoka haiwezekani
 
Nilivyoona kichwa cha mada nilidhani kinazungumzia biashara ya boda boda kuua ndoto za vijana wengi kutokana na ajali nyingi zinazosababisha vifo na ulemavu!

Inasikitisha sana, biashara ya bajaji na bodaboda imeachwa ijiendeshe kiholela kana kwamba hakuna serikal!

Hawaheshimu Sheria za usalama barabarani, hawana vituo maaum vya kusubiri wateja, wanapakia mizigo hatarishi k.m. nondo, bati nk.

Kama zikiendelea kuongezeka kwa kasi hii, itafika wakati Barbara za miji yote zitakuwa kero kubwa kwa watumiaji wengine.

Serikali inapaswa kuchukua hatua stahiki kurekebisha hali hii pamoja na kwamba wamechelewa sana!
 
Ni kweli mzeee .ifike wakati hizi pikipiki zipigwe marufuku kuingia nchini mana zishakuwa fujo na usababishaji wa ajali kila siku .

Zilizopo kwenye mzunguko zinatosha kabisa kuendana na soko husika.

Nchi imekuwa kama dampo kila aina ya uchafu unaletwa huku

Hizi boda boda ni uchafu unaonekana dhahabu na ajira kwa vijana wa kileo.

Bodaboda na pikipiki zimekuwa kama aina ya siasa kwa watawala

Watu wanahoji zikipigwa marufuku au kuondolewa hao vijana wanakuwa wezi kama zamani ,hili jambo sio kweli kwani tangia boda zimeingia na wizi wanatumia hizo hizo boda boda kuiba na kukimbia

.

Piga ban pikipiki kuingia nchini hata baada ya miaka miwili kwanza

Bodaboda wanachosha kwanza wengi wao hawana elimu ya uendeshaji
Alafu hawa boda boda wa mjini wana tamaaa kishenzi , juzi kati hapa eti boda kuanzia mtaa wa kongo hadi karibia na serena sheli pale anataka buku tano.

Pumbavuuuuu kabisaaaa
 
Back
Top Bottom