Biashara si kufungua Ofisi na kusajili Kampuni bali ni Uwezo wa Kuuza (No Sales = No Business_

GLOBAL CITIZEN

JF-Expert Member
Jun 5, 2014
767
1,655
Wakuu,

Vijana wengi wanaoanza business hapa Tz naweza sema hawana idea biashara ni nini hasa.

Nikisema hivyo baadhi wanashangaa.

Wengine wanakasirika.

Kwasababu wanaona kama vile “bright ideas” walizo nazo nazithoofisha.

La hasha, hilo si lengo langu.

Nipo hapa kwaajili yakushare uzoefu wangu kwahiyo ni vyema ukiwa na mawazo tofauti unaweza ukaongezea hapo kwenye comment section.

Binafsi nimekutana na watu wengi wanaoanzisha business wakiwa wameshakosea tayari. Na niseme tu, hata mimi nilikuwa hivyo.

Give thanks to my brother Metthew yeye ni “big shark” hapa Arusha kwahiyo najifunza kwake (hasahasa Hustle za offline).

Yes man, ni muhimu kuwa na mentor/guru/teacher wakukupatia “connection” pale inapobidi.

Ok, turudi kwenye mada.

Hii issue yakuanza business vibaya inawakamata watu wengi wanaoanza business mpya. Iwe Online au hizi traditional business.

Unakuta mtu yupo moto, ana raise mtaji, anakodi ofisi, anaajiri na wafanyakazi kabisa mwisho wa siku asifahamu nani hasa atanunua vitu au service anazouza.

It’s crazy situation.

Baada ya muda hizi business zinakufa.

Na kitu kibaya hazifi hivi hivi tu.

Lazima ziwe zimekukamua mfuko.

Planning kwenye business is VERY VERY IMPORTANT.

Na haiishii hapo.


Ili kuifanya hili darasa liwe simple ngoja ni list down kwanini Business si kufungua ofisi au kuharakia kusajili kampuni nakulipa kodi.

1 • Biashara zinazofanikiwa mara nyingi ni zile zinazo “grow organically”

Ok, ngoja twende sawa namaanisha nini na haya maneno “grow organically”.

Hapa namaanisha namna ile unaanza biashara kidogo kidogo huku wateja wakiamini katika kazi zako na si tu kukurupuka kisa una mtaji wakuanzisha Business.

Kuna uzi fulani hapa JF ulikuwa unamuongelea Jackline Mengi sasa kwenye huo uzi watu wengi walikuwa wame focus zaidi kwenye kumshambulia huyu mwanadada kwasababu ameshindwa kuendesha business alizoanzisha.

Note : Kwa dhati kabisa mimi sifahamu lolote kuhusu uendeshaji wa biashara za Jackline Mengi iwapo anapata faida au hapati. Na hilo si lengo langu kutaka kufahamu. Ni vile tu nimeona nitumie mfano huu kwasababu nimeona umesomwa na watu wengi na itafit hapa.

Ok, sasa Kuna comment moja ili “catch” attention yangu.

Mchangiaji alidai Jackline Mengi biashara yake ya kutengeneza high end furniture haikulenga mbinu hii ya “ku-grow organically” kwahiyo akaingia katika mtego wakudhani “ukianzisha business” basi wateja watakuja tu kitu ambacho si cha kweli kwahiyo biashara yake inapumulia mashine (ipo ICU)

Mchangiaji yeye aliona Jackline aliingia kwenye hii Business kwasababu tu aliona ni Business flani hivi “ya kishua” kwahiyo ni Business profitable bila kuangalia uhalisia ambao ndiyo lengo la hii thread yangu.

Kwamba Jackline kwasababu tu alikuwa na access ya capital kwahiyo akaona akikimbilia kuunda ofisi kali na product kali basi atapa wateja lakini mwisho wasiku biashara imekuwa ngumu hakuna anayenunua toka kwake.

Binafsi bila kujalisha ni kweli au si kweli naelewa watu wengi wanaanza biashara kwa mamna hii they are doomed to fail.

Kisa cha Jackline Mengi ni mfano tu.

Unajua watu wengi wanaoanza business wana focus zaidi kwenye Wrong things.

Na moja ya Wrong things ni kutotumia mbinu yaku “grow organically” kwakuanza kwanza kuunda authority katika eneo wanaotaka kuanzisha business.

Kwa mfano unafikiria kuanzisha biashara ya kuuza magari je si vema ukaanza kwa kufahamu jinsi business ya magari ilivyo? Kwamba unaongea na watu, unapata maarifa na unakuwa expert katika eneo hili.

Kwa namna hii utakuwa na uhakika mkubwa unachokifanya watu wanakipenda na vile wanavyokuwazia.

Huu ni mfano kwa kila aina ya Business.

Hata kama unafanya Business yakutengeneza na kuuza Yatch kule Monte Carlo au Miami au Marbella.

Inabidi kwanza watu wakufahamu.

Ukitumia hii mbinu hakika business yako haitakufa kuliko kukurupuka unaenda kukopa pesa bank kisa umesikia watu wengi siku hizi wananunua magari.

Mtu wangu utajikuta unalamba hasara hadi utashangaa.

Kuna faida nyingi zakuanza biashara organically.

Moja ya faida ni uwezekano wa kutumia pesa za watu wanaokuona mjuzi katika eneo lako wakitaka wenyewe ufanye nao biashara.

Deals zinazokuja namna hii ni tamu sana kwasababu ni uhakika asilimia 100 mteja anayetoa pesa yupo.

Hii mbinu watu wengi wanaikwepa kwasababu wanaona ni kazi sana kuanza kutengeneza connection na watu kwenye aina ya business wanayotaka kuanza kwasababu wao wanapenda kufanya Business kwa hisia zaidi kuliko reality.

2 • Biashara ni kuuza. Kama hakuna Sale hapo hakuna Business mtu wangu. Hata kama una Ofisi down town.

Umeshaona watu wanakimbilia ku rent chumba cha biashara cha mamilioni halafu baada ya miezi sita kodi ikiisha wanakimbia?

Hawa nao wanafanya makosa yale yale.

Kisa wameona fulani ana Business ya duka la nguo mjini kati linapata wateja basi na yeye akifungua duka atapiga pesa.

Nakwambia you are more likely to fail.

Ili uwe kwenye Business you need to make a SALE.

Na ili uuze wala haihitaji physical office. Trust me on this.

Watu wengi wanaanzisha big business bila ya ofisi mpaka pale wanapotengeneza some profit ndiyo wanahamia kwenye kupanga ofisi na kulipa kodi.

Ukiona wewe upo concerned sana na sijui kodi au mambo ya formalities sana you don’t have what it take to run a business.

Ukiwa kwenye Business focus yako ni “ku make a sale” na si kuingia gharama za kulipa rent.

3 • Kama bado hufahamu namna yaku LEVERAGE pesa za watu wengine, muda wa watu wengine, utachelewa sana kutengeneza REAL PROFIT.

Aisee hii point watu wengi hawailewi ndiyo maana Hustle/Business zao hazipigi hatua.

Unakuta Business imeanzishwa na ina potential ya kupiga hatua kutengeneza some real profit lakini kwasababu yakukosa mbinu zaku “scale up” basi business inabaki ndogo miaka yote.

Kwenye Business inabidi uwe BULL.

Hauhitaji kufanya kila kitu mwenyewe hatahivyo.

Jifunze ku-outsource zile kazi zinajirudia rudia.

Hapo maana yake una leverage muda wa mtu mwingine na wewe kuweka muda zaidi kwenye mambo unavyoweza kufanya kwa ufanisi.

Pia niseme kama kweli wewe ni real entrepreneur kamwe huwezi lalamikia sana kuhusu mtaji.

Kama kweli una KIU yakufanikiwa kwenye Business fulani lazima tu utapata namna. Na hapa ndipo inakuja point yakujifunza jinsi unavyoweza kutumia pesa za watu wengine kutengeneza za kwako.

Kumbuka, si lazima uanze na idea ya kwanza ya Business unataka kufanya. Unaweza ukaanza na idea nyingine ambayo ni rahisi kutumia hii mbinu yaku levarage pesa za watu wengine ili upate mtaji unaouhitaji.

Mfano rahisi wa biashara ya namna Hii ni ku-promote bidhaa au huduma ya mfanyabiashara mwingine ili akilipe commission Kwa kila deal utakalofanikisha. Business za namna hii hazihitaji capital kuanza. Ni wewe tu na confidence yako.

Binafsi nimepiga sana kazi za real estate na kulipwa commission. Na hi business naendelea nayo na imenipatia connections muhimu. Sikuhitajk capital kuunza labda uwezo wakufikira kwa usahihi na kuweza kuuza basi.

4 • Je, Business unayotaka kufanya ina solve “Real World Problem?”

Hili swali halijibiwi kwa kufanya assumption.

Ukifanya hivyo tu umepotea.

Nikwambie kitu kimoja, unaweza ukawa na idea fulani bright sana ukasema Aaah hii nikiitekeleza basi utakuwa millionaire. Lakini baada ya kuingia gharama nyingi unatambua no one is willing to buy from you.

Umeshakutana na hii mambo?

Hili tatizo linatokea kwasababu watu wanaoanza Business wanafikiria Business is about them na vile wanavyojisikia kuhusu hiyo business.

Nikwambie mtu wangu, biashara ni mteja.

Uza kile tu watu walichotayari kuunua toka kwako.

Mambo mengine ni mahaba yako tu. Wala si uhalisia wa kile potential customers wanataka.

Na haiishii hapo.

Lazima urudi kwenye point number moja ili watu wanunue toka kwako. Unaweza rudi mwanzo usome upya.

Unaona jinsi haya mambo yanavyokwenda kwa planning?

Ok ngoja niishie hapa.


Cheers
 
Mkuu asante nimejifunza mengi! nilianza biashara kwa kuweka bidhaa ambazo mimi niliona zitaifanya biashara ionekane nzuri, lakini baadaye nilikuja gundua wateja walikuwa wahitaji huduma na bdihaa nyingine kabisa, nilivyorekebisha mambo yakaanza kwenda vizuri
 
Mkuu asante nimejifunza mengi! nilianza biashara kwa kuweka bidhaa ambazo mimi niliona zitaifanya biashara ionekane nzuri, lakini baadaye nilikuja gundua wateja walikuwa wahitaji huduma na bdihaa nyingine kabisa, nilivyorekebisha mambo yakaanza kwenda vizuri

Ndiyo ukweli huo wengi hawaelewi
 
Lhii inaitwa kisu kwa mfupa..taratiiibu tutawezana

Yes bro,

Ukifanya uchunguzi wako mdogo utagundua hili.

Binafsi business kadhaa nilizojaribu kuanzisha kwasababu tu nadhani “watu wataipenda” zilikufa ndani ya kipindi kifupi tu.

Kuna mdau hapo kasema yeye alianzisha business akaweka bidhaa “zinazopendezesha duka” Alidhani watu wakiona duka lake zuri watanunua kumbe watu wanataka bidhaa nyingine kabisa
 
Nice message boss, hakika kuna lessons kbao za kujifunza Na kuzingatia

However, I would like to add kitu kingine ambacho ni very crucial na ndicho kinapelekea kutimiza end goal ya Sales which means biashara itasurvive na kuwa profitable

THAT IS MARKETING,... Traditional na kwa dunia ya sasa lazima tuongezee na online marketing, especially social media marketing

Am knowledgeable in these areas, na naona kbs sometimes kinachofelisha wafanyabiashara sio bad products /service bali ni POOR MARKETING EFFORTS

mfano hata uyo Jacklin mengi uliyemtaja, na hata izi biashara zingine nyingi.. Zinafel because of marketing

You might have the best products /services in town,but if no one knows or is persuaded enough to come and buy from you.. Eventually you'll fail in your business

Social media marketing is very crucial, and marketing in general... Na sio kutumia tactics za kupush products tu through paid ads, bali kwa kutanguliza adding value and solving problems of customers first.. Before asking for a sale

Nakubaliana naulicho andika mkuu.

Kabla yakupata sales kazima kwanza umefanya ushawishi fulani huyu mteja akubali kununua toka kwako.

Hili ndilo somo langu KUU hapa JF.

Sales inakuja baada ya kufanya marketing.

Na marketing maana yake ni chochote kile unachoweza kufanya kumshawishi au kumvutia aone umuhimu wakufanya biashara na wewe.

Sasa ukifikia hatua hiyo inamaana hutosumbuka kwenye kuuza kwa huyu potential customer kwasababu tayari umeshampa reason kwanini ni muhimu kununua kwako.

Hiyo ni first stage.

Tatizo kubwa wafanyabiashara wasiofahamu kuuza wana jump moja kwa moja kumuuzia mtu bidhaa. Hapa unaweza ukauza lakini si effective in long run.

Kuhusu digital marketing? Mimi nina team ya marketing kuanzia Facebook Ad expert, Google Ads, video editor, voice talent, telemarketers, mtu kwaajili ya kuunda professional landing pages + kuhakikisha ana maintain campaign hadi potential customers wananunua product au service, copy writing expert.

I work as a team.

Lakini inategemea client ninayemfanyia kazi anahitaji nini hasa.

Wingine yeye anataka tu apate Facebook Advertising itakayomletea kweli wateja.

Client mwingine inaweza ikawa ni kampuni ya magari wao wanataka “full package” yaani una manage department yote ya marketing. Hii ni big business na sasa hivi ndiyo nafanya kazi. Inahitaji mazungumzo ya kina na client na hata ku-sign contracts.

Ok ngoja niishie hapa.
 
Uko Arusha na unafanya real estate?

Yes mimi ni real estate agent.

Ninafanya kazi na wageni wengi toka nje (au mtu yeyote yule) kuwafanikishia kununua au kupata apartments au nyumba zakupanga hapa Arusha. This is what I do almost everyday. Pia mimi ni AirBnB host kwahiyo nipo na uzoefu kwenye hili eneo.
 
36 Reactions
Reply
Back
Top Bottom