Biashara itakayokupa faida ya bilioni 1 kwa mwaka

puker

JF-Expert Member
Nov 22, 2018
940
1,847
Habar zenu wadau.

Mimi ni mfanyabiashara wa kati, yupo mzee mmoja ni mteja wangu wa muda kidogo...kiasi Cha kuwa rafiki.

Baada ya kuniona namna ninavyofanya biashara yangu...alipenda. akanipa kazi ya kumuandalia mpango wa biashara (Business plan) yenye mtaji usiozidi mil 20, ambayo anataka kumfungulia kijana wake. Nilianza kutekeleza agizo lake ingawaje ilinichukua muda kidogo...maana hata mzee mwenyewe sio mtu wa hovyo...hivyo sikutaka kumchagulia kitu Cha hovyo hovyo...nashukuru Mungu niliamaliza na last week nimemkabidhi.

Sasa baada ya kupitia kwa makini, juzi aliniita ofisini kwake kwa ajili ya kunipa mrejesho. Kiukweli aliipenda Sana na akasema hakuamini Kama Nina weza kuwaza nje ya box kiasi kile.

Ila kilichonishangaza, amesema anataka kunipa kazi nyingine kabla hiyo haijafanyiwa utekelezaji. Kidogo alinipa mashaka kuona anaweza kunidhulumu wazo langu akalitumia bila Mimi kunufaika.

Ila aliweka wazi hana lengo la kufanya hivyo ila baada ya kusoma wazo langu amegundua Nina kitu kikubwa zaidi ya hicho.

Ananiambia nifikirie mradi utakaoweze kuzalisha faida ya 1bilioni moja ndani ya miezi 12 (mwaka mmoja). Kiukweli nimewaza na kuwazua bado sijapata, Ni biashara gani hasa inaweza kuzalisha fedha nyingi kiasi hicho ndani ya hicho kipindi hicho kifupi. Yani Mil 83.3 kwa kila mwezi.

Ukizingatia hali yetu ya kiuchumi kwa hapa nchini. Naomba tupeane mawazo wadau angalau nipate hata mwanga juu ya hiyo biashara.

Sijui ana malengo gani huyu mzee..ila anaonekana yuko very serious, na business plan ya kwanza amenirudishia ili niondoe hofu juu ya kunidhulumu haki yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna swali gumu duniani katika maswala ya kiuchumi kana kuulizwa ni biashara gani ina faida kubwa kuliko zote.

Kwa uoni wangu biashara zote ni nziri na zinalipa.

Ila jitahidi sana usifanye biashara za kuuza bidhaa, kama utafanya hivyo basi hakikisha unazalisha mwenyewe sio kuagiza mzigo na kuuza, mwanzoni utapata stress nyingi sana na kama sio mvumilivu unaweza kupotea kabisa katika dira.

Naomba kuwakilisha.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazo langu la kwanza lilikuwa ni kilimo ndio naamini inaweza kuzalisha hiyo faida endapo utaamua kuwekeza vilivyo ila ndio Sina elimu nacho sijui nianzie wap au niishie wap

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kibongo bongo hio aimed profit ni kubwa sana per annum ...labda kwa kuuza "Sembe ya Mexico"
Huo mtaji anao kweli huyo mzee au anataka kutembelea nyota yako??

Sent using Jamii Forums mobile app
biashara zipo nyingi saana ambazo mtu anaweza akafanya na kupata hiyo faida ila ukweli uliopo ni kuwa kibongobongo matajiri hawako radhi kulipa gharama ya idea.
naweza kuwa na idea na biashara fulani na nikampa mtu ila sasa utekelezaji ikawa ngumu kidogo.
 
Habar zenu wadau.

Mimi ni mfanyabiashara wa kati, yupo mzee mmoja ni mteja wangu wa muda kidogo...kiasi Cha kuwa rafiki.
Baada ya kuniona namna ninavyofanya biashara yangu...alipenda. akanipa kazi ya kumuandalia mpango wa biashara (Business plan) yenye mtaji usiozid mil 20, ambayo anataka kumfungulia kijana wake. Nilianza kutekeleza agizo lake ingawaje ilinichukua muda kidogo...maana hata mzee mwenyewe sio mtu wa hovyo...hivyo sikutaka kumchagulia kitu Cha hovyo hovyo...nashukuru Mungu niliamaliza na last week nimemkabidhi.

Sasa baada ya kupitia kwa makini, juzi aliniita ofisini kwake kwa ajili ya kunipa mrejesho. Kiukweli aliipenda Sana na akasema hakuamini Kama Nina weza kuwaza nje ya box kiasi kile.
Ila kilichonishangaza, amesema anataka kunipa kazi nyingine kabla hiyo haijafanyiwa utekelezaji. Kidogo alinipa mashaka kuona anaweza kunidhulumu wazo langu akalitumia bila Mimi kunufaika.

Ila aliweka wazi hana lengo la kufanya hivyo ila baada ya kusoma wazo langu amegundua Nina kitu kikubwa zaidi ya hicho.

Ananiambia nifikirie mradi utakaoweze kuzalisha faida ya 1bilioni moja ndani ya miezi 12 (mwaka mmoja). Kiukweli nimewaza na kuwazua bado sijapata, Ni biashara gani hasa inaweza kuzalisha fedha nyingi kiasi hicho ndani ya hicho kipindi hicho kifupi. Yani Mil 83.3 kwa kila mwezi. Ukizingatia hali yetu ya kiuchumi kwa hapa nchini. Naomba tupeane mawazo wadau angalau nipate hata mwanga juu ya hiyo biashara.

Sijui ana malengo gani huyu mzee..ila anaonekana yuko very serious, na business plan ya kwanza amenirudishia ili niondoe hofu juu ya kunidhulumu haki yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kiasi gani anakusudia kuwekeza mfano?
Pia ni eneo gani anataka afanyie biashara kwanza, mfano mimi naweza kuwa na wazo la biashara mfano wa tofali za kuchoma morogoro lakini hili wazo haliwez mfaa mtu wa dar.
Je ni mtu ambaye anaweza chukua risks zozote au uvumilivu hata miezi miwili ?
Idea mimi nina idea moja inaweza fikisha almost kiasi hicho lakini je nafaidikaje pale napokuuzia idea yangu, ukaifanya na kufanikiwa bila mimi kunufaika na ukichukulia inaweza isiwe idea mpya machoni lakin kiutendaji nikawa na njia mpya za kutekeleza. Idea moja ibeba bidhaa tatu za kutengeneza na zote zinaanzia kwenye chanzo kimoja
 
Kiasi gani anakusudia kuwekeza mfano?
Pia ni eneo gani anataka afanyie biashara kwanza, mfano mimi naweza kuwa na wazo la biashara mfano wa tofali za kuchoma morogoro lakini hili wazo haliwez mfaa mtu wa dar.
Je ni mtu ambaye anaweza chukua risks zozote au uvumilivu hata miezi miwili ?
Idea mimi nina idea moja inaweza fikisha almost kiasi hicho lakini je nafaidikaje pale napokuuzia idea yangu, ukaifanya na kufanikiwa bila mimi kunufaika na ukichukulia inaweza isiwe idea mpya machoni lakin kiutendaji nikawa na njia mpya za kutekeleza. Idea moja ibeba bidhaa tatu za kutengeneza na zote zinaanzia kwenye chanzo kimoja
Kwa ukubwa wa biashara...sidhani Kama location Ni tatizo ili mradi iwe ndani ya nchi na ndio mana kanipa uhuru wa kutafuta hiyo idea, ila tu kuwepo na ushawishi wa kimantiki akaona ni wazo linalowezekana na sio bra bra, nafikiri unajua Business plan ime consist vitu gani. Na kama hilo wazo unalo unaweza kunipa few details ili tuweze kuongea Kama nitaona mwanga ktk hoja zako. Kiuchumi Ni mtu anaejiweza anafanya biashara ya pesa nyingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vile vile kama unafikiri biashara ambayo ina low entry risk basi fikira kuwekeza kwenye Technology,Research and Development.Zipo Idea Kibao so cha muhimu ni kujua kiasi cha mtaji uliopo,na muda uliopo then ideas zinaweza kumiminika kama mchele.Msisitizo.Kutengeneza a bilion per year kuna hitaji both a good idea and a good business plan
 
Vile vile kama unafikiri biashara ambayo ina low entry risk basi fikira kuwekeza kwenye Technology,Research and Development.Zipo Idea Kibao so cha muhimu ni kujua kiasi cha mtaji uliopo,na muda uliopo then ideas zinaweza kumiminika kama mchele.Msisitizo.Kutengeneza a bilion per year kuna hitaji both a good idea and a good business plan
Nimekuelewa vyema mkuu...najua hi sio Kazi nyepesi natakiwa kufanya reseach ya kutosha. Asante kwa mchango wako boss.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kufika turn over ya bil.moja sio jambo gumu ni rahisi sana. Pia sio jambo rahisi pia ni ngumu sana. Kwa kuwa.ni lazima uchangue njia mbili kuu. Mosi uandike kuhusu Bulk business, pili manufacturing industries. Shart kuu ni lazima uwekezaji ( cost of Investment) ivuke mil 500. Sasa usiwaze sana ni biashara gani pia waza how utawekeza vema, ( wise investment) ya 500mil.
 
Back
Top Bottom