Biashara ipi ya kuwekeza kipindi hiki kwa mtaji wa milioni 30 -50?

Nikikuwa nahitaji ushauri wenu nina Mtaji wa millioni 30 nahitaji kufungua biashara dodoma mlikuwa mnanishauri na biashara gani
Tafuta center iliyochangamka chukua mchele grade tofauti tofaut,tafuta maharage yanayopendwa kama aina tatu iv,unga na mazagazaga ya vyakula vingine uza jumla jumla if possible nunua na boda fanya delivery
 
Kama mjuavyo kwasasa kuna mdororo wa biashara hapa nchini haswa Dar kutokana na sababu mbalimbali. Kuna mdau anataka mawazo kuhusu mradi upi awekeze, waswahili husema penye wengi hakiharibiki kitu.

Biashara pendekezwa
1. Kununua na Kuuza Spare Parts za magari
2. Hardware ya vifaa vya ujenzi
3. Video & Photography/digital studio business
4. Workshop ya kushona na kuuza nguo kama suti (tailoring)

Mtaji: mpaka milioni 40 kutokana na biashara
Mahali: Dar

Mwekezaji:
Huyu anaishi Dar lakini ana majukumu ya kila siku ya muajiri yanamuweka bize hivyo hawezi kuendesha mradi muda na saa za kazi. Anapendelea kutafuta msimamizi au mshiriki/partner ambae anamuda ili kusimamia mradi/biashara kwa pamoja.

Ushauri unaohitajika:
Ushauri je ni biashara ipi itamfaa kati ya hizo au nyinginezo haswa ukizingatia hana muda na pia hajawahi fanya hizo biashara anatagemea usimamizi wa mtu au mshiriki kama akipatikana. Tafiti zinaonyesha usimamizi hafifu huchangia sana biashara kufa kutokana na hasara.

Wadau wenye biashara ambao hawazisimamii wao wenyewe mnaombwa kutoa uzoefu ili kupata mwazo chanya.
Kwa upande wangu number 2 and 4 ndio zitakua biashara nzuri Cha muhimu location na msimamizi atakempata awe serious pia kwa kushona creativity ikihusika kidogo kufanya kitu Cha tofauti itapendeza.
 
Nikikuwa nahitaji ushauri wenu nina Mtaji wa millioni 30 nahitaji kufungua biashara Dodoma. Mlikuwa mnanishauri na biashara gani?
Kama unapenda magari( narudia tena kama unapenda magari) chukua Civilian toka japan baada ya mwaka na nusu pesa yako itakuwa imerudi then anza mipango mingine. Unless otherwise nichek tuonane ana kwa ana tufanye uwekezaji wa maana. Nipi dodoma
 
Nikikuwa nahitaji ushauri wenu nina Mtaji wa millioni 30 nahitaji kufungua biashara Dodoma. Mlikuwa mnanishauri na biashara gani?
Kwa Dodoma Fanya haya.

1.machine ya kusaga na kupark unga.

2.hardware kwa maeneo kama chang'ombe kwenda ndanchi.

3.machine ya kukamua alizeti hii waweza iweka popote kwa Dodoma.


4.usafirishaji kama bajaji,kwahy hela utapata bajaji nne na change inabaki nyingi tu,hii biashara ndo nafanya yaani ni nzuri sana.

Anyways ideas ni nyingi sana if interested njoo Pm kidogo
 
40m kwenda China ? Inabidi ufanye utafiti wa kutosha..la sivyo utaenda mara moja tu na mtaji utakata...gharama ya kwenda na kurudi si chini ya 3m...bado hujatoa mzigo bandarini....frem hujakodi ...leseni.. TRA ..kumbuka sio lahisi kuuza mzigo wote ukaisha lazima katikati kabla mzigo haujaisha uende tena.

hapo ndio utangundua mtaji ni mdogo...labda uwe unchukua oder kwa wenye maduka mzigo ukifika unauza tu. Au subiri wale wanao shusha conterner chukua mzigo na ww uza..wengi ndio wanafanya hivyo kkoo.
Hao wanaoshusha kwenye macontainer unawapatia wapi boss
 
Kama mjuavyo kwasasa kuna mdororo wa biashara hapa nchini haswa Dar kutokana na sababu mbalimbali. Kuna mdau anataka mawazo kuhusu mradi upi awekeze, waswahili husema penye wengi hakiharibiki kitu.

Biashara pendekezwa
1. Kununua na Kuuza Spare Parts za magari
2. Hardware ya vifaa vya ujenzi
3. Video & Photography/digital studio business
4. Workshop ya kushona na kuuza nguo kama suti (tailoring)

Mtaji: mpaka milioni 40 kutokana na biashara
Mahali: Dar

Mwekezaji:
Huyu anaishi Dar lakini ana majukumu ya kila siku ya muajiri yanamuweka bize hivyo hawezi kuendesha mradi muda na saa za kazi. Anapendelea kutafuta msimamizi au mshiriki/partner ambae anamuda ili kusimamia mradi/biashara kwa pamoja.

Ushauri unaohitajika:
Ushauri je ni biashara ipi itamfaa kati ya hizo au nyinginezo haswa ukizingatia hana muda na pia hajawahi fanya hizo biashara anatagemea usimamizi wa mtu au mshiriki kama akipatikana. Tafiti zinaonyesha usimamizi hafifu huchangia sana biashara kufa kutokana na hasara.

Wadau wenye biashara ambao hawazisimamii wao wenyewe mnaombwa kutoa uzoefu ili kupata mwazo chanya.
Mkuu 40 M ni hela nzuri sana,

Biashara unaweza fanya zenye return ya kati ya 3% kwa mwezi hadi 15% kwa mwezi,Full Reported,Well managed,Low Risk,Transparent etc.Kwa maelezo zaidi PM.Vigezo na Masharti kuzingatiwa.
 
Back
Top Bottom