youzam
Member
- Apr 9, 2020
- 19
- 21
Watu wengi sana wamekuwa wakitafuta huku na huko kujua ni biashara gani inalipa. Yawezekana wengi hatuelewi maana ya biashara inayolipa. Ukweli ni kwamba, biashara inayolipa ni ile ambayo ina uhusiano chanya kati ya kipato unachopata na matokeo ya kile unachokitoa.
Mfano. Kama wewe ni mwalimu na ukafungua twisheni ukapata milioni 6 kwa mwezi, na mwisho wa siku wanafunzi wako wakafeli, basi hujaanzisha biashara inayolipa. Ili iwe biashara inayolipa, ni lazima wanafunzi wako wafahuru, maana kuwa, lazima kuwe na uhusiano chanya wa moja kwa moja kati ya pesa uliyoingiza na matokeo ya kile ulichokifanya.
Kuna mtu atanambia kinachoangaliwa ni pesa. Hapana, pesa si kila kitu. Ukweli ni kwamba, biashara yoyote inayoanzishwa kwa lengo la kuangalia pesa mwisho wake huwa inakufa. Kinyume chake ni kwamba, kama biashara yako ukianzisha kwa kuangalia ni matokeo gani wateja wako watapa kulingana na pesa wanayokupa, basi hapo utakuwa umeanzisha biashara itakayodumu na kukua haraka sana.
Hii ni kwasababu, watu wanahitaji kupata ufumbuzi wa matatizo yao. Mtu akipata ufumbuzi wa tatizo, haoni shida kutoa pesa yoyote ilimradi tu apate bidhaa au huduma inayokidhi mahitaji yake.
Ushahuri wangu ni kwamba, katika biashara unayofanya, hakikisha unaweka mteja wako mbele na pesa nyuma, hapo ndipo utakuwa na biashara inayolipa na haitakufa. Tutajifunza zaidi namna ya kuanzisha biashara inayolipa kwa muktadha wa hii post.
Mfano. Kama wewe ni mwalimu na ukafungua twisheni ukapata milioni 6 kwa mwezi, na mwisho wa siku wanafunzi wako wakafeli, basi hujaanzisha biashara inayolipa. Ili iwe biashara inayolipa, ni lazima wanafunzi wako wafahuru, maana kuwa, lazima kuwe na uhusiano chanya wa moja kwa moja kati ya pesa uliyoingiza na matokeo ya kile ulichokifanya.
Kuna mtu atanambia kinachoangaliwa ni pesa. Hapana, pesa si kila kitu. Ukweli ni kwamba, biashara yoyote inayoanzishwa kwa lengo la kuangalia pesa mwisho wake huwa inakufa. Kinyume chake ni kwamba, kama biashara yako ukianzisha kwa kuangalia ni matokeo gani wateja wako watapa kulingana na pesa wanayokupa, basi hapo utakuwa umeanzisha biashara itakayodumu na kukua haraka sana.
Hii ni kwasababu, watu wanahitaji kupata ufumbuzi wa matatizo yao. Mtu akipata ufumbuzi wa tatizo, haoni shida kutoa pesa yoyote ilimradi tu apate bidhaa au huduma inayokidhi mahitaji yake.
Ushahuri wangu ni kwamba, katika biashara unayofanya, hakikisha unaweka mteja wako mbele na pesa nyuma, hapo ndipo utakuwa na biashara inayolipa na haitakufa. Tutajifunza zaidi namna ya kuanzisha biashara inayolipa kwa muktadha wa hii post.