Nakereka sana na nyimbo za majipu, huku nchi ikizidi kuzama kwa siasa uchwara! Na wewe umenikera kumwita mtu jipu au mpiga dili kwa sababu tu ameamua kuuza "asset" yake. Mtu humjui wala hakujui, anaamua kuuza asset yake wewe unaibuka kwenye keyboard kumuita jipu na mpiga dili. Kwanini mnakubali kugeuzwa waimba nyimbo chonganishi wakati majipu akina Lugumi wanazidi kutanua? Badala ya kukomalia akina Lugumi, Escrow ambayo inazidi kukukwangua kila siku hata wewe mwenyewe kila siku, wewe unakurupuka na mtu ambaye ameamua kuuza chake. Umenikera sana Mama Obama, samahani lakini!Mbona umekasirika? Jamani Chabusaru ama ukweli unauma? Hakuna mutu masikini, MASIKINI ni yule mtu anaulemavu ana ANA afya mbaya ama mvivu hawezi kufanya kazi. Kila mtu ni tajiri,lakini watu wanakuwa MASIKINI kwasababu wezi wanaojiita viongozi na WAFANYA BIASHARA feki wanatufilisi kwa kutuiibia ndiyo maana wengi wetu ni masikini kwa kuwa tunadhurumiwa na wachache. Kama wewe siyo mmoja wa wadhurumaji basi usikadirike. Na kama wewe ni jipu ama umefaidika kwa BIASHARA za dili basi badilika fanya kazi ama fanya biadhara halali.