Wadau nauliza kama kuna mbongo ambaye amewahi fika Goma DRC ili nijue boda aliyopitia na ugumu uliopo. Nasikia kuna watannzania wanafanya biashara huko, nataka nikachungulie.
Je ni kweli kuna biashara maana mim pia nilitaka kwenda kuchungulia nimeambiwa huko mambo ni mazur ukipeleka vyakula kama unga, chumvi n.k alimradi ni bidhaa za cyakula naskia biashara huko imekaa vyema
tafuta milioni zako mbili au tatu nenda mzima mzima ukafanye research mwenyewe, utapata network za kutosha kabla hata ya kuja kuchukua mzigo na istoshe to the minimum milioni moja itatosha kwenda na kukaa wiki moja kwa uchache na kufanya utafiti wenye mafanikio makubwa, wabongo wapo kuna jamaa yangu uko jeshini alikuwa ananipa habari, future iko nje nje kule
Nenda ukachungulie lakini kuwa makini. Pitia kigali panda bus la tawfiq ukifika kigali utapanda bus la gisenyi borda hapo ndio borda ya Ruanda na Goma. Angalia sana watu wa Ruanda wengi hawawapendi watzWadau nauliza kama kuna mbongo ambaye amewahi fika Goma DRC ili nijue boda aliyopitia na ugumu uliopo. Nasikia kuna watannzania wanafanya biashara huko, nataka nikachungulie.
Je wapo watanzania wanaofanya kazi au biashara eneo hilo,? Ninauzoefu kidogo katka mji wa lilongwe malawi kule watanzania wapo wa kutosha hadi wakulima wa karanga wapo huko hivyo kwasisi waganga njaa ukifika hapo lazma utakuta mtanzania anazagaa maeneo ndio nauliza je eneo hilo wapo watanzania?
Nenda ukachungulie lakini kuwa makini. Pitia kigali panda bus la tawfiq ukifika kigali utapanda bus la gisenyi borda hapo ndio borda ya Ruanda na Goma. Angalia sana watu wa Ruanda wengi hawawapendi watz
kama uko Dar chukua bus ( sumry) adi Bukoba 60,000 tsh kisha chukua bus adi kampala ( bukoba adi kampala ni kama km 300 nauli 15,000 tzsh.
kisha kampala chukua bus ( horizon bus) utoka saa 1 jioni na ufika Goma congo saa 4 asubuh. bus upitia rwanda naul ni kuanzia 20,000 tsh.
au chukua bus za rwanda kisha goma congo.
Mkuu vipi usumbufu mipakani? Suala la vibali limekaaje? Kuna maeneo mengine yafaayo kutembelea mbali na Goma?
visa je unachukua ubalozi hapa au unaipata kulekule na kiasi gani ,, maana mimi tayari nisavutiwa kwenda huko insha Allah
visa je unachukua ubalozi hapa au unaipata kulekule na kiasi gani ,, maana mimi tayari nisavutiwa kwenda huko insha Allah
Visa unapata mpakani kwa dolla 50.na ni ya miezi 3
Swali dogo:
Toka Tz nitapita Rwanda ndio niingie DRC. Vipi kuhusu kupita Rwanda, suala la visa limekaaje? Na pia pesa ipi inayotumika kwa biashara?
nchi 5 za afrika mashariki ukiingia ni bure ulipii visa,watakuuliza tu unakaa muda gani sema kutembea,na unagongewa visa,nchi hizo ni Uganda,kenya,tanzania,rwanda na burundi.
kuhusu matumizi ya pesa,unabadilisha pesa kulingana na nchi uliyopo,pia mpaka wa Rwanda na tanzania upo Rusumo mkoani kagera