Tupeane Uzoefu: Biashara gani ilikushinda?

Biashara ya bodaboda kwangu inafanya poa tu,ninazo 6 na madereva nimewapa mkataba baada ya mwaka mmoja pikipiki nawaachia,so wanafanya kazi kwa molali..changamoto zipo mojamoja ila sio za kunifanya niache hii biashara
Wewe hii mbinu nahisi inasaidia sana!
 
Nilishawishika nikanunua ist kwa mtu nikaiingiza kwenye Uber. Kilichotokea kila nikiona simu ya dereva roho inanipasuka. Nikatafuta mtu nikamuuzia ile gari roho ikanitulia maana ningekonda kwa presha
Vip mkuu ilikuwa na Matatizo au?
 
Magroup gani ayo na Mimi nijiunge!!?
Jipange tu, kuna watu nipo nao kwny groups wanapiga hela
[/QUOTE]
 
Dah hiyo nayo ni kari, kwahiyo vp ulifanikiwa kumuuzia?
Bishara ya kuza dawa za chooni aiseee nilikutana na changamoto Sana ila hili la mteja mmoja kunikabidhi dekio chafu ni lisugue kwa dawa likitakata ndo anunue sikulivumilia na kupiga chini hiyo biashara
 
Mkuu kwa biashara ya pkpk ungewapa za mkataba hao bodaboda mbona unge furahi maana we ni kupokea Elfu 70 kila juma na hakuna usumbufu wa kupigiwa simu kila mara ooh bosi taa imevunjika ooh bosi mnyororo umeisha yaan kila kitu ni juu yake we ni kunyoosha mkono ukiwa tupu na kuurudisha mfukoni ukiwa na 70 elfu. Lakn hata huo mkataba nao una changamoto yake.

Kipindi niko first year chuo nlinunua bodaboda mbili aisee io changamoto yake usipime stres tupu madereva pasua kinoma nikapiga chini nikaziuza zote aisee
 
Mkuu kwa biashara ya pkpk ungewapa za mkataba hao bodaboda mbona unge furahi maana we ni kupokea Elfu 70 kila juma na hakuna usumbufu wa kupigiwa simu kila mara ooh bosi taa imevunjika ooh bosi mnyororo umeisha yaan kila kitu ni juu yake we ni kunyoosha mkono ukiwa tupu na kuurudisha mfukoni ukiwa na 70 elfu...... Lakn hata huo mkataba nao una changamoto yake.
Mkataba watu wanaandikishana lakini wapi mkuu labda kama wewe unawapaga pikipiki mwaka ukiisha...
 
biashara iliyonishinda ni ile wanakuambia "GOOD MORNING BILLIONAIRE UNACHOTAKIWA KUFANYA NI KULETA WENZAKO WA2 NA WAO WALETE WATU WA2 KISHA UNAANZA KUPIGA HELA KWENYE HIO NETWORK YAKO"
Global marketing

Alliance walikuwa nini hao
Wanachuo wanatekwa Sana nao
 
Back
Top Bottom