mukama talemwa
Senior Member
- Jun 14, 2011
- 160
- 28
Hivi wadau hizi bia na soda na bidha nyingine ambazo huwa wanapewa majeshi bila kodi zina maana gani?Mimi kwasasa niko Shy ila kitu cha kushangaza kuwa Polisi na Magereza wamefungua mabaa na kuuza bia kwa sh 1300 na wanauzia kila mtu pale baa,na wafanyabiashara wanalalamika kuwa biashara mbaya maana kila mtu anakimbilia kule kwenye bei ndogo maana ni baa kama baa nyingine na hakuna masharti yeyote kupata kinywaji.Kuna kiongozi mmoja wa kambi moja ya jeshi naye anamiliki baa bia anazouza nizile ambazo hazina kodi na bila aibu nimeshuhudia akitelemsha bia na soda kutoka kwenye gari la jeshi nakupeleka katika baa yake na waliokuwa wanafanya kazi hiyo ni wanajeshi.Hivi nchi yetu imekosa ufuatiliaji kiasi hicho,na kwanini serikali inakosa kodi bila sababu yeyote maana vinywaji hivyo vinafanyiwa biashara kama kawaida.