11 January 2010
Zitto kazana na shule, achana mambo ya siasa kwa sasa.Siasa utazikuta ukishapata PhD yako, si una ndoto ya kugombea urais wewe? Sasa ukifeli hiyo shule hiyo ndoto yako utaitimizaje? Mshika mawili moja humponyoka, kazana na shule wee, kwetu Ujiji wasomi wanahesabika lakini wanasiasa ni wengi tangu enzi ya ukoloni, kina Mzee Takadiri na wengineo.Sasa na wewe usiwe kwenye kundi la wanasiasa waliokuja wakapita.
Ukimaliza shule yako hapo unaitwa Daktari (kule kwetu watakujia wagonjwa uwatibie, itabidi ufanye kazi ya ziada ya kuwaambia mie shio Daktari wa kutibu watu bali kutibu maneno falsafa) utakuwa na nafasi kubwa na nzuri ya kuendelea na siasa.
Narudia tena achana na hayo mamitandao sijui nini, kimsingi kama ni umaarufu ulishapata unahangaika nini? Kwanza kama unasema huyo Mhariri ni MwanaBidii (sijui bidii ya nini hapa) ina maana kuwa maoni yako aliyaona huko kwenye forum yenu ya Bidii na kwa kuwa yeye ndiye EDITOR angeweza kumwambia mwandishi wake kuwa hii habari uliyoiandika si ya kweli, kwa sababu sivyo alivyoandika Zitto huko kwenye forum. Kwa kuwa aliipitisha ikatoka gazetini ina maana imetoka kwa baraka zake zote. Sasa unatuleta USANII hapa kuwa nimemuomba mhariri, unamuomba nini na wewe una hakika hukutendewa haki na vyombo vinavyohusika na maadili ya vyombo vya habari viko kwa ajili yenu? Kwanini usipeleke malalamiko yako ukalishtaki gazeti na Mhariri wake? Ama ni njia yako ya kutaka umaarufu, maana hata bad publicity inalipa si watu wanakusikia uko hewani umeandikwa aidha kwa mazuri au mabaya lakini uko hewani.
Mie ushauri wangu kwako, acha usanii, kama ni kweli wamekukosea, basi wafikishe kunakohusika, sio kuleta blah blah kwenye mitandao. Maana kusema umejitoa kwenye Bidii forum, bado haujatupa ushahidi wa kutosha jinsi hao Bidii Forum walivyohusika na kukuandika vibaya kwenye gazeti la Tanzania Daima. Maana ingekuwa huko kwenye Bidii Forum moderator amebadilisha maoni yako uliyoyatoa hapo ningesema kuwa una haki ya kuwalaumu na kuwasema vibaya na kujitoa kwao. Lakini waliokuandika vibaya ni gazeti la chama chako kipenzi, gazeti la Chadema Tanzania Daima, ningetegemea unasema jamani eeh mie nimeshachoka kupakwa matope na hawa Chadema kupitia gazeti lao na kuanzia leo nachukua hatua zifuatazo, 1, 2, 3.
Nakuuliza tena una shea huko Chadema au kwenye hilo gazeti???
Ni mimi dadaako kutoka Ujiji
bi Mkora
CHANZO: Mtandao wa Kwanzajamii.com
Zitto kazana na shule, achana mambo ya siasa kwa sasa.Siasa utazikuta ukishapata PhD yako, si una ndoto ya kugombea urais wewe? Sasa ukifeli hiyo shule hiyo ndoto yako utaitimizaje? Mshika mawili moja humponyoka, kazana na shule wee, kwetu Ujiji wasomi wanahesabika lakini wanasiasa ni wengi tangu enzi ya ukoloni, kina Mzee Takadiri na wengineo.Sasa na wewe usiwe kwenye kundi la wanasiasa waliokuja wakapita.
Ukimaliza shule yako hapo unaitwa Daktari (kule kwetu watakujia wagonjwa uwatibie, itabidi ufanye kazi ya ziada ya kuwaambia mie shio Daktari wa kutibu watu bali kutibu maneno falsafa) utakuwa na nafasi kubwa na nzuri ya kuendelea na siasa.
Narudia tena achana na hayo mamitandao sijui nini, kimsingi kama ni umaarufu ulishapata unahangaika nini? Kwanza kama unasema huyo Mhariri ni MwanaBidii (sijui bidii ya nini hapa) ina maana kuwa maoni yako aliyaona huko kwenye forum yenu ya Bidii na kwa kuwa yeye ndiye EDITOR angeweza kumwambia mwandishi wake kuwa hii habari uliyoiandika si ya kweli, kwa sababu sivyo alivyoandika Zitto huko kwenye forum. Kwa kuwa aliipitisha ikatoka gazetini ina maana imetoka kwa baraka zake zote. Sasa unatuleta USANII hapa kuwa nimemuomba mhariri, unamuomba nini na wewe una hakika hukutendewa haki na vyombo vinavyohusika na maadili ya vyombo vya habari viko kwa ajili yenu? Kwanini usipeleke malalamiko yako ukalishtaki gazeti na Mhariri wake? Ama ni njia yako ya kutaka umaarufu, maana hata bad publicity inalipa si watu wanakusikia uko hewani umeandikwa aidha kwa mazuri au mabaya lakini uko hewani.
Mie ushauri wangu kwako, acha usanii, kama ni kweli wamekukosea, basi wafikishe kunakohusika, sio kuleta blah blah kwenye mitandao. Maana kusema umejitoa kwenye Bidii forum, bado haujatupa ushahidi wa kutosha jinsi hao Bidii Forum walivyohusika na kukuandika vibaya kwenye gazeti la Tanzania Daima. Maana ingekuwa huko kwenye Bidii Forum moderator amebadilisha maoni yako uliyoyatoa hapo ningesema kuwa una haki ya kuwalaumu na kuwasema vibaya na kujitoa kwao. Lakini waliokuandika vibaya ni gazeti la chama chako kipenzi, gazeti la Chadema Tanzania Daima, ningetegemea unasema jamani eeh mie nimeshachoka kupakwa matope na hawa Chadema kupitia gazeti lao na kuanzia leo nachukua hatua zifuatazo, 1, 2, 3.
Nakuuliza tena una shea huko Chadema au kwenye hilo gazeti???
Ni mimi dadaako kutoka Ujiji
bi Mkora
CHANZO: Mtandao wa Kwanzajamii.com