Pasco_jr_ngumi
JF-Expert Member
- Nov 20, 2010
- 1,802
- 282
hoja
waheshimiwa wabunge
mnaunga mkono
hoja?..Ndiyooooooooo!..........
Hizi ndio kauli kuu mbili kwa wabunge
wetu ya kwanza ni ya baadhi ya
wabunge ambao wakisimama hawaachi
kusema kauli hiyo ya kuunga mkono
hoja huku ya pili ikitumika mara nyingi
na spika kwenye kufikia maamuzi
mbalimbali ambapo wabunge wetu mara
nyingi ni watu wa ndiyo.
Inasikitisha sana! Wabunge wetu
wamekuwa wavivu wa kujenga hoja
wamepwaya sana kiasi cha kwamba
wamebaki kuwa watu wa ndiyo tu hata
kwa mambo ambayo hayana maslahi
kwa taifa au hao wananchi wa
majimboni mwao, inasikitisha kuona
kuwa kila mwaka bajeti ya nchi
imekuwa ya uchungu kama sio jasho na
damu kwa mtanzania masikini, bajeti
hizi zimekuwa zinashindwa kumkomboa
mtanzania kutoka kwenye lindi la
umasikini lakini cha ajabu ni kuwa bajeti
hizi zilipitishwa bungeni na wabunge
wetu na iwapo wewe msomaji wangu
unadhani huu ni mzaha au naongopa
basi subiri hilo bunge la bajeti la mwezi
juni utaona hali halisi jinsi wabunge
wetu walivyopwaya kwenye kujenga
hoja watapitisha bajeti itakayozidi
kutukamua.
Huwa nashindwa kuelewa hivi kuna
wabunge wanaenda bungeni kusema
ndiyo tena kwa makelele makubwa?
utadhani hizo kelee zao za ndiyo
zinaboresha shule za kata majimboni
kwao? Au zinawasaidia mamia ya
masikini wa jimboni kwao kuweza
kujikimu kimaisha? Wabunge hawa
ndiyo huonekana majimboni kila baada
ya miaka mitano kisha hawachaguliwi
bali wanatumia fedha kununua uongozi
na kwa bahati mbaya ndiyo hivyo
TAKUKURU haina la kufanya na hata
ikithubutu mara kibao watuhumiwa
wanashinda kesi na kuachiwa huru kisa
TAKUKURU wanakosea kufungua
mashtaka, ajabu sana!
Na hata baadhi ya wabunge wa vyama
Fulani wakijitutumua kusema umezuka
mchezo wa kitoto wa kuwazomea ,
inasikitisha kuona kuwa CCM ndiyo
walikuwa vinara wa kuwazomea
wabunge wa CHADEMA na hata kuna
wakati wabunge wa CHADEMA
wamemlaumu waziwazi spika Anne
Makinda kuwa anakibeba chama chake
cha CCM na hata wabunge wa upinzani
wakijitutumua kupinga maamuzi
legelege kwa nguvu ya hoja kwa
bahati mbaya wenzao wa CCM wapo
wengi hivyo wanatumia hoja ya nguvu
kuzima hoja za wapinzani.
Hivi wabunge wetu wanajua kweli kwa
nini wapo bungeni? Wanafahamu tabu
tulizonazo? Hivi hawa wabunge
wanaounga mkono hoja wanafahamu
kuwa kuna ndugu zetu wako mahabusu
kwa mwaka wa tatu sasa bila
kusomewa kesi? Hivi wanafahamu kuwa
kuna ndugu zetu wanaporwa ardhi
kwa hoja za uwekezaji? Wanafahamu
kuwa madini yetu yanazidi kuisha na
kubakisha mashimo ya kuzalisha mbu
wa maralia huku wenyewe hatufaidiki
kitu? Hivi hawa wabunge wanafahamu
kuwa kuna ndugu wamefeli kwenye
shule za kata kwa sababu tu serikali
inafanya mzaha na elimu?
Hivi hawa watu wanafahamu kuwa ajali
za bararani zinazidi kutumaliza kwa
uzembe wa vyombo husika? Hivi hawa
watu wanafahamu jinsi gani vijana
wetu walipigwa pale Mlimani na Dodoma
kwa sababu ya kudai nyongeza ya
fedha za kujikimu kitu cha haki kabisa?
Inauma sana waache mzaha kabisa sisi
masikini wa nchi hii tunateseka tu bila
sababu za msingi haiwezekani
tukaendelea kuwa masikini huku
wanaotusababishia umasikini huo ni
wao tunawajua , HAKIKA HAWA
HAWAVUMILIKI MAANDISHI YASHAANDIKWA
UKUTANI UNABII NI LAZIMA UTIMIE TU.
Hivi kwani hawa wabunge wasioweza
hata kuchambua mambo kwa hoja kwa
nini wasijiuzulu tu? Wanafanya nini
bungeni? Au kuitikia ndiyo? Wanakera
sana yaani wanakubali kila kitu kwa
nini lakini? Mbona wenzetu kule
Uingereza wanajadili mambo kwa hoja?
Au hapo Kenya mbona bunge lao si
mchezo kwa jinsi wanavyojadili mambo
kwa hoja, sisi tuna nini? tumerogwa ?
mbona sisi ni watu wa ndiyo huku
tukiendelea kudidimia kwenye umasikini
wa kutisha? Naam! Tatizo ni wabunge
wetu kupenda kupiga makofi hata
kwenye mambo yasiyotusaidia
wamekuwa watu wa ndiyo sana wana
uwezo mdogo sana wa kuje
waheshimiwa wabunge
mnaunga mkono
hoja?..Ndiyooooooooo!..........
Hizi ndio kauli kuu mbili kwa wabunge
wetu ya kwanza ni ya baadhi ya
wabunge ambao wakisimama hawaachi
kusema kauli hiyo ya kuunga mkono
hoja huku ya pili ikitumika mara nyingi
na spika kwenye kufikia maamuzi
mbalimbali ambapo wabunge wetu mara
nyingi ni watu wa ndiyo.
Inasikitisha sana! Wabunge wetu
wamekuwa wavivu wa kujenga hoja
wamepwaya sana kiasi cha kwamba
wamebaki kuwa watu wa ndiyo tu hata
kwa mambo ambayo hayana maslahi
kwa taifa au hao wananchi wa
majimboni mwao, inasikitisha kuona
kuwa kila mwaka bajeti ya nchi
imekuwa ya uchungu kama sio jasho na
damu kwa mtanzania masikini, bajeti
hizi zimekuwa zinashindwa kumkomboa
mtanzania kutoka kwenye lindi la
umasikini lakini cha ajabu ni kuwa bajeti
hizi zilipitishwa bungeni na wabunge
wetu na iwapo wewe msomaji wangu
unadhani huu ni mzaha au naongopa
basi subiri hilo bunge la bajeti la mwezi
juni utaona hali halisi jinsi wabunge
wetu walivyopwaya kwenye kujenga
hoja watapitisha bajeti itakayozidi
kutukamua.
Huwa nashindwa kuelewa hivi kuna
wabunge wanaenda bungeni kusema
ndiyo tena kwa makelele makubwa?
utadhani hizo kelee zao za ndiyo
zinaboresha shule za kata majimboni
kwao? Au zinawasaidia mamia ya
masikini wa jimboni kwao kuweza
kujikimu kimaisha? Wabunge hawa
ndiyo huonekana majimboni kila baada
ya miaka mitano kisha hawachaguliwi
bali wanatumia fedha kununua uongozi
na kwa bahati mbaya ndiyo hivyo
TAKUKURU haina la kufanya na hata
ikithubutu mara kibao watuhumiwa
wanashinda kesi na kuachiwa huru kisa
TAKUKURU wanakosea kufungua
mashtaka, ajabu sana!
Na hata baadhi ya wabunge wa vyama
Fulani wakijitutumua kusema umezuka
mchezo wa kitoto wa kuwazomea ,
inasikitisha kuona kuwa CCM ndiyo
walikuwa vinara wa kuwazomea
wabunge wa CHADEMA na hata kuna
wakati wabunge wa CHADEMA
wamemlaumu waziwazi spika Anne
Makinda kuwa anakibeba chama chake
cha CCM na hata wabunge wa upinzani
wakijitutumua kupinga maamuzi
legelege kwa nguvu ya hoja kwa
bahati mbaya wenzao wa CCM wapo
wengi hivyo wanatumia hoja ya nguvu
kuzima hoja za wapinzani.
Hivi wabunge wetu wanajua kweli kwa
nini wapo bungeni? Wanafahamu tabu
tulizonazo? Hivi hawa wabunge
wanaounga mkono hoja wanafahamu
kuwa kuna ndugu zetu wako mahabusu
kwa mwaka wa tatu sasa bila
kusomewa kesi? Hivi wanafahamu kuwa
kuna ndugu zetu wanaporwa ardhi
kwa hoja za uwekezaji? Wanafahamu
kuwa madini yetu yanazidi kuisha na
kubakisha mashimo ya kuzalisha mbu
wa maralia huku wenyewe hatufaidiki
kitu? Hivi hawa wabunge wanafahamu
kuwa kuna ndugu wamefeli kwenye
shule za kata kwa sababu tu serikali
inafanya mzaha na elimu?
Hivi hawa watu wanafahamu kuwa ajali
za bararani zinazidi kutumaliza kwa
uzembe wa vyombo husika? Hivi hawa
watu wanafahamu jinsi gani vijana
wetu walipigwa pale Mlimani na Dodoma
kwa sababu ya kudai nyongeza ya
fedha za kujikimu kitu cha haki kabisa?
Inauma sana waache mzaha kabisa sisi
masikini wa nchi hii tunateseka tu bila
sababu za msingi haiwezekani
tukaendelea kuwa masikini huku
wanaotusababishia umasikini huo ni
wao tunawajua , HAKIKA HAWA
HAWAVUMILIKI MAANDISHI YASHAANDIKWA
UKUTANI UNABII NI LAZIMA UTIMIE TU.
Hivi kwani hawa wabunge wasioweza
hata kuchambua mambo kwa hoja kwa
nini wasijiuzulu tu? Wanafanya nini
bungeni? Au kuitikia ndiyo? Wanakera
sana yaani wanakubali kila kitu kwa
nini lakini? Mbona wenzetu kule
Uingereza wanajadili mambo kwa hoja?
Au hapo Kenya mbona bunge lao si
mchezo kwa jinsi wanavyojadili mambo
kwa hoja, sisi tuna nini? tumerogwa ?
mbona sisi ni watu wa ndiyo huku
tukiendelea kudidimia kwenye umasikini
wa kutisha? Naam! Tatizo ni wabunge
wetu kupenda kupiga makofi hata
kwenye mambo yasiyotusaidia
wamekuwa watu wa ndiyo sana wana
uwezo mdogo sana wa kuje