Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
King Kong...Nakufuatilia sana Mkuu Mohamed ,kwenye historia ya uhuru tuliambiwa kwamba Mzee Aikaeli Mbowe(Mkristo) alimchangia pesa Mwalimu nyerere ya kwende UNO na alikuwa mfadhili wa harakati nyingi za kupigania uhuru lakini watu kama hao hauwazungumzii kwasababu ni wakristo ,angekuwa muislam ungemzungumzia kama yule aliyetoa kiwanja cha ccm ofisi ya lumumba.
Ada...Nilikuwa mfuatiliaji mzuri sana wa historia na matukio ya zamani ktk blog yako. Siku hizi siioni hewani kulikoni?
Lengo la Mleta mada ni kuwafanya watu wajue kuwa walioshiriki vita vya majimaji ni WaislamMajina ya Kiislam au ya Kiarabu? Kumbuka Waziri wa mambo ya Nje wa Iraq wakati wa Saddam Hussein alikuwa mkristo mwenye jina la kiarabu "Tariq Aziz"
Nafuu umemfahamu huyu Mlaaniwa Mohamed SaidLengo lako ni moja tu!
Kutuambia mashujaa waliopigana vita vya majimaji ni waislamu na unataka kutuambia kuwa historia imewatenga.
Mzee kwa Udini hujambo.
Itabidi ugombee urais kupitia NRA ama ACT/CUF na uchaguliwe tuone utatufikisha wapi kama watanzania.
Sijui utaisilimisha nchi yote ama lah!
Eti Wanakwepa majina ya kiislam, kwani wasipokwepa itawasaidia nini na wakikwepa inawasaidia nini?Kipuyo,
Hakika umesema kweli.
Lengo la makala yangu ni kueleza kwa nini katika Vita Vya Maji Maji wanahistoria wa mwanzo wamejitahidi kwa kiasi kikubwa kukwepa majina ya Kiislam?
Ikiwa mimi kufanya hivyo unaona nafanya makosa inakuwaje kwa hawa wanaokwepa kutaja majina ya Waislam wakawataja kwa majina siyo?
Ndipo nikaliweka jina la Bi. Khadija Mkomanile na jina la Abdulrauf Songea Mbano.
Bahati mbaya kama wewe unaumizwa na hizi juhudi zangu za kusahihisha historia hii.
Uongo na Uzushi utakunyima Firdaus MzeeKing Kong III,
Historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika imejaa visa na mikasa mingi ya Waislam na sababu ni kuwa wao ndiyo walikuwa wengi kwenye harakati.
Hupendi kusoma historia hii?
Mzee wetuMsanii,
Historia ya.Maji Maji ina mengi.
Soma barua ya Nduna Abdulrauf Songea Mbano kwa Sheikh Mataka Hamim Massaninga unaweza ukaelewa.
Mzee anayeujua ukweli na kulazimisha utumike Kidini ili kueneza haiba ya kibaguzi.Mzee Mohamed wewe mashujaa wako ni waislamu tu,sijawahi kuona ukiwasifia wakristo waliopigania uhuru.
Ni kweliKatika picha unakomaa na Abdulrauf Songea Mbano badala ya kutuonyesha shujaa wetu Bi. Khadija Nkomanile ambae ndiye main character wa huu uzi!🚶🚶🚶
Huo ni unyanyasaji wa kijinsia ya ke ndani ya siku ya wanawake duniani!Beh...
Umesema kweli.
Nataka msomaji asome katikati ya mistari.
Beh...Huo ni unyanyasaji wa kijinsia ya ke ndani ya siku ya wanawake duniani!
Obe...Kusema ukweli, Mzee Mohamed Said umekuwa Mwalimu nzuri sana wa kutupatia elimu kubwa juu ya Viongozi waliokuwa vinara katika kupigania Uhuru wa Tanganyika na hatimaye Tanzania baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar!
Mwenyezi Mungu akujalie maisha marefu uweze kutufunza mengi!
Angalia picha na soma yaliyoandikwa.Kwahiyo hivyo Vita vya jihad vilitumia ushirikina? Hayo maji Ni ushirikina.
Sidhani Kama ni sahihi kusema Vita vya maji maji Ni Jihad.