Tila-lila2
JF-Expert Member
- Oct 20, 2019
- 653
- 1,058
Inasemekana hali imezidi kuwa tata na haijulikani alipo! Ndugu yangu aliyepo Dodoma jirani yao kanitonya!
=====
Tumefuatilia kwa karibu taarifa za Polisi Tanzania kumshikilia Bi. Fatma Jumanne, msaidizi wa nyumbani wa Bi. Joyce Mukya, kinyume cha sheria tangu jana. Amekuwa akihojiwa kama shahidi wa jeshi hilo kuhusu tukio la kuvamiwa, kushambuliwa na kujeruhiwa Mkiti wa Chama Mhe. Freeman Mbowe.
Jana jioni jeshi hilo likabadili na kuanza kumhoji kama mtuhumiwa, kuwa ametoa taarifa za uongo kuhusu tukio la kushambuliwa na kujeruhiwa kwa Mhe. Freeman Mbowe Bi. Fatma amenyimwa dhamana huku zikiwepo taarifa za kupigwa na kuteswa. Tutatoa taarifa kamilo juu ya suala hili.
Kwa mujibu wa mawakili wanaofuatilia suala hilo, katika mahojiano aliyofanyiwa, Bi. Fatma amelalamika kuwa amekuwa akilazimishwa aseme mambo ambayo hayajui, wanayotaka polisi, kuhusu tukio la kuvamiwa, kushambuliwa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mhe.Freeman Mbowe.
Kutokana na mazingira yanayozunguka suala la kuendelea kushikiliwa, kutofikishwa mahakamani na kunyimwa dhamana kwa Bi. Fatma kinyume cha taratibu za kisheria, tayari wanasheria wameanza utaratibu wa kuwasilisha Mahakama Kuu ombi maalum la kulitaka Jeshi la Polisi limwachie.
Chanzo: CHADEMA
=====
Tumefuatilia kwa karibu taarifa za Polisi Tanzania kumshikilia Bi. Fatma Jumanne, msaidizi wa nyumbani wa Bi. Joyce Mukya, kinyume cha sheria tangu jana. Amekuwa akihojiwa kama shahidi wa jeshi hilo kuhusu tukio la kuvamiwa, kushambuliwa na kujeruhiwa Mkiti wa Chama Mhe. Freeman Mbowe.
Jana jioni jeshi hilo likabadili na kuanza kumhoji kama mtuhumiwa, kuwa ametoa taarifa za uongo kuhusu tukio la kushambuliwa na kujeruhiwa kwa Mhe. Freeman Mbowe Bi. Fatma amenyimwa dhamana huku zikiwepo taarifa za kupigwa na kuteswa. Tutatoa taarifa kamilo juu ya suala hili.
Kwa mujibu wa mawakili wanaofuatilia suala hilo, katika mahojiano aliyofanyiwa, Bi. Fatma amelalamika kuwa amekuwa akilazimishwa aseme mambo ambayo hayajui, wanayotaka polisi, kuhusu tukio la kuvamiwa, kushambuliwa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mhe.Freeman Mbowe.
Kutokana na mazingira yanayozunguka suala la kuendelea kushikiliwa, kutofikishwa mahakamani na kunyimwa dhamana kwa Bi. Fatma kinyume cha taratibu za kisheria, tayari wanasheria wameanza utaratibu wa kuwasilisha Mahakama Kuu ombi maalum la kulitaka Jeshi la Polisi limwachie.
Chanzo: CHADEMA