God bell
JF-Expert Member
- May 13, 2011
- 590
- 210
Acha niseme kabisa, ninayo kila sababu ya kuisifu JF. Liwe ni wazo zuri au baya kila ninapoomba ushauri/mongozo nilipata majibu mazuri sana. Niliwahi kusoma thread ya mtu 1 aliyetoa ushauri jinsi ya kufanikiwa kwene biashara nikafanya hivyo nikafanikiwa. Kuna mtu aliomba ushauri wa kitabibu na alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa fulani, nikawa na mimi nina tatizo hilo hilo. Ushauri alopewa na mim nikaufatilia, leo hii nimepona ni mzima wa afya njema kabisa. Kwa ujumla mafanikio yangu ya maisha nimeyapata humu JF. Kwa nini nisiwamwagie sifa Jf?