Better to return home from a failed marriage than coming back home in a coffin

Lusungo

JF-Expert Member
Jan 4, 2014
27,102
39,279
Hello members,

Ni kipindi sijakutana nanyi tena ndugu zangu wa MMU natumai mu wazima.

Leo nimekuja na kisa nilichoshuhudia kilichonifanya niandike uzi Huu Siku ya Leo tukielekea valentine day.

Kichwa cha uzi kinasema kwa kimombo “better to return home from a failed marriage than coming back home in a coffin”

Kwa tafsiri sisisi tunaweza kusema “Ni bora zaidi kurudi nyumbani kutoka Ktk ndoa iliyokushinda kuliko kurudi nyumbani ndani ya jeneza”

Huu ni msemo maarufu wa mwanafalsafa fulani wa kizungu.

Kisa kilichopelekea kuandika haya ni tukio la kweli la hivi karibuni la msichana mrembo kuuwawa na mumewe na wazazi kupelekewa mwili wa mtoto wao kwenye jeneza.

Baada ya kufwatilia kisa na mikasa ya ndoa Yao tulibaini msichana alivumilia ukatili usiomithilika toka kwa mwenziwe uliopolekea mauti yake.

Kwanini kuvumilia yote hayo? Kwanini kuficha yote hayo?

Kisa cha msichana huyu kinaakisi maisha yetu wengi tunayopitia humu ndani. Kisa hiki kinawakilisha mlolongo wa madhila yanayotupata wengi ktk mahusiano na tunaamua kuyafumbia macho.

Hebu tutafakari ni uchungu na hasara ya namna gani tunaachia wazazi na jamaa zetu.

Sio aibu kurudi nyumbani kuanza upya ukiwa na tumaini jipya kuliko kurudi ndani ya jeneza.

Nawatakia heri ya siku ya wapendanao.
 
Sasa mbona kisa cha huyo msichana ambacho ndio kiini cha huu uzi haujaezea?.. Huu uzi ukibaki hivi hivi unakosa maana japokuwa wazo lako ni zuri
 
vipo vya kuvumilia vipo visivyovumilika

kama mumeo anakushirikisha vyote mpaka hela anayoimake ili tu wewe mkewena watotomuishi siku akikwambia sina stahmili hilo linavumilika

akirudi amelewa anakupiga tu yan hata ukizidisha chumvi anakupiga, akirudi ukachelewa kufungua mlango anakupiga mwisho umeamua unyamaze ukipigwa hulii anahamia kwa watoto anawapigapas nakisa hii haivumiliki eti vumilia atabadilika, kubadilika kwake labda afe au ufe hii haivumiliki

hata mimi nina ndugu yang tulishamzika muda tu tena yeye alikua mjamzito, mume alikua anapiga kama anapigangoma akimwambia mama yakeanajibiwa vumilia mwanangu ndio ndoa mwisho wa siku kaletewa mait ya mwanae
 
Hello members,

Ni kipindi sijakutana nanyi tena ndugu zangu wa MMU natumai mu wazima.

Leo nimekuja na kisa nilichoshuhudia kilichonifanya niandike uzi Huu Siku ya Leo tukielekea valentine day.

Kichwa cha uzi kinasema kwa kimombo “better to return home from a failed marriage than coming back home in a coffin”

Kwa tafsiri sisisi tunaweza kusema “Ni bora zaidi kurudi nyumbani kutoka Ktk ndoa iliyokushinda kuliko kurudi nyumbani ndani ya jeneza”

Huu ni msemo maarufu wa mwanafalsafa fulani wa kizungu.

Kisa kilichopelekea kuandika haya ni tukio la kweli la hivi karibuni la msichana mrembo kuuwawa na mumewe na wazazi kupelekewa mwili wa mtoto wao kwenye jeneza.

Baada ya kufwatilia kisa na mikasa ya ndoa Yao tulibaini msichana alivumilia ukatili usiomithilika toka kwa mwenziwe uliopolekea mauti yake.

Kwanini kuvumilia yote hayo? Kwanini kuficha yote hayo?

Kisa cha msichana huyu kinaakisi maisha yetu wengi tunayopitia humu ndani. Kisa hiki kinawakilisha mlolongo wa madhila yanayotupata wengi ktk mahusiano na tunaamua kuyafumbia macho.

Hebu tutafakari ni uchungu na hasara ya namna gani tunaachia wazazi na jamaa zetu.

Sio aibu kurudi nyumbani kuanza upya ukiwa na tumaini jipya kuliko kurudi ndani ya jeneza.

Nawatakia heri ya siku ya wapendanao.
Siku hizi hakuna ukatili wa vipigo kama zamani kama upo ni KIWANGO kidogo sana.
Hali ya sasa ni ukatili wa kihisia na maisha magumu.
Wasichana wakikutana na maisha magumu wanakimbia
 
ujumbe mzuri, ila ujumbe ungekua mzuri zaidi ungetuambia kilicho msibu uyo binti ili iwe fundisho kwa wengine.
 
Tatizo la wanawake wa siku hizi wanapenda Sana kulazisha wawe sawa na wanaume Jambo ambalo piga ua haliwezekani.

Sijui wanadanganywa na Nani??..?
 
Tatizo la wanawake wa siku hizi wanapenda Sana kulazisha wawe sawa na wanaume Jambo ambalo piga ua haliwezekani.

Sijui wanadanganywa na Nani??..?
Achilia mbali those lame reasons of yours.
Hakuna mwenye haki yakuchukua uhai wa mwenzie kakushinda muache over!
 
Umesema vyema mkuu.

Tatizo jamii imelitafsiri vibaya lile neno la "mwanamke mpumbavu huvunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe" kiasi mwanamke asipovumilia akatoka Basi ni mwanamke atanyooshewa vidole kuwa sio mvumilivu na mengine Kama hayo.

Kiasi imepelekea wanawake wengi waendelee kuishi kwa mateso Hadi kifo kije kuwaokoa
 
Back
Top Bottom