Timu yetu ya Taifa Tanzania bara kwa sasa iko katika mashindano ya kombe la Chalenge nchini Kenya.. timu imecheza na Zambia imeonyesha uhai kidogo ambao kama ungeongezewa baadhi ya wachezaji timu ingelikuwa bora zaidi hasa katika katika idara ya upachikaji mabao na ushambuliaji.. inakumbukwa wakati mchezaji Mwaikimba alipokuwa Taifa Stars na ilipoenda kule Senegal vyombo vya habari na wapenzi wa soka walikuwa na hofu naye na kusababisha awekewe ulinzi mkali.......sababu ya umbile lake... hivi Betraim Mwombeki kweli hastahili kuitwa katika timu ya Taifa ili asaidiane na akina Ngassa, Samata Ulimwengu na hao wengine? binafsi naamini Mwombeki akiitwa stars atakuwa msaada mkubwa na tishio kwa mabeki wa timu mbalimbali