John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Mshambuliaji wa Simba, Bernard Morrison ameomba radhi kwa wachezaji wenzake, benchi la ufundi pamoja na kwa uongozi wa klabu yake kwa utovu wa nidhamu aliouonyesha.
Imeelezwa kuwa Morrison ambaye ni raia wa Ghana ametumia group la mtandao wa WhatsApp kuomba radhi kwa wenzake kisha akaomba wafikishe salamu kwa uongozi, lakini pia aliutuma ujumbe huo pia kwa viongozi.
Mchezaji mmoja wa Simba ameeleza kuwa Morrison ambaye alidaiwa kutoroka kambini wiki iliyopita, kisha kusimamishwa na uongozi wa klabu kutokana na kufanya matukio ya kujirudia, anajutia makosa yake aliyoyafanya lakini uongozi haujatoa jibu lolote kwake hadi sasa, na hata wachezaji wenzake hawajamjibu chochote.
Simba wapo katika mchakato wa kujiandaa na mchezo wa Hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast, Jumapili Februari 13, 2022.
Source: Mwanaspoti
Imeelezwa kuwa Morrison ambaye ni raia wa Ghana ametumia group la mtandao wa WhatsApp kuomba radhi kwa wenzake kisha akaomba wafikishe salamu kwa uongozi, lakini pia aliutuma ujumbe huo pia kwa viongozi.
Mchezaji mmoja wa Simba ameeleza kuwa Morrison ambaye alidaiwa kutoroka kambini wiki iliyopita, kisha kusimamishwa na uongozi wa klabu kutokana na kufanya matukio ya kujirudia, anajutia makosa yake aliyoyafanya lakini uongozi haujatoa jibu lolote kwake hadi sasa, na hata wachezaji wenzake hawajamjibu chochote.
Simba wapo katika mchakato wa kujiandaa na mchezo wa Hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast, Jumapili Februari 13, 2022.
Source: Mwanaspoti