Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,808
- 11,973
Membe anahoji:
"Je Tupo tayari kwenda kwenye Uchaguzi bila kuwa na tume huru?
Tume huru ya Uchaguzi ndugu zangu, maana yake ni kwamba uwe na Tume katika ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa ambayo ina watu wa aina zote. Wa dini zote, vyama vyote, aina zote za Elimu, Wanasiasa Maarufu bila kujali chama Tawala, Wanakuwa kwenye hilo kundi.
Ili wanapo amua kuhusu Mwanachama anayeomba Udiwani au Ubunge, apitishwe bila Upendeleo.
Sasa mtu mmoja akaniuliza, "Kwani huko nyuma Mheshimiwa mlipitishwaje?". Nikasema tulipitishwa kwa utaratibu huo huo lakini katika mazingira ya sasa hivi, ambayo Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa au Mkurugenzi, anajisikia hofu kwamba akipita Mtu wa Chama kingine Cheo chake kinaweza kuondoka, anaweza akafanya vitendo vya Upendeleo kulinda Masrahiya cheo chake.
Kwahiyo katika Mazingira ya sasa lazima tuwe na Tume Huru.
Nikawa najiuliza, hili swala la Tume huru tunafanyaje? Twende nalo hivyo hivyo au tuwe na Tume huru? Jibu likawantiwe na tume huru.
Nikawa pia najiuliza kwamba safsri hii tumeambiwa Waangalizi wa Uchaguzi wa dunia( International observers) hawatakuwepo kwa sababu UNDP hajatoa fedha za Uchaguzi, hawatakuwepo sababu wengi wanahofia Corona.
Je, tupo tayari kwenda kwenye Uchaguzi katika mazingira ya kutokuwa na Waangalizi wa Uchaguzi kutoka kote Duniani watakao Sema Uchaguzi huu ulikuwa wa haki, ulikuwa huru na unao heshimika, tupo tayari kufanya hivyo bila kuwa na Waangalizi wale?
Nikawa najiuliza haya Maswali. Wakati fulani nikasema, inawezekana Uchaguzi huu hautafanyika karibuni utafanyika baadae.
Lakini Wanasiasa wengine wakasema hapana, tukazanie moja tu la kuwa na Tume Huru na kuwa na Waangalizi wa Uchaguzi. Mambo Mawili lakini tuendelee kuwa na Uchaguzi.
Sasa ndo maana tukachukua wiki nzima toka wiki iliyopita, kuongea na Wanasiasa ndani ya Chama na nje ya chama watupe Mwanga wa nini kifanyike".
Pia soma:
Elections 2020 - Membe: Kamati Kuu haina mamlaka ya kunifukuza Uanachama wa CCM bali Halmashauri Kuu ya Taifa. Asema kati ya Juni na Oktoba chochote kinaweza tokea
CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama