Bernard Membe: Polepole apelekwe shule kuijua vyema itikadi ya CCM. Ni ajabu Kamati Kuu kukaa bila Katibu Mkuu

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,818
Uchambuzi wa Waziri wa Mashauri ya Kigeni Mstaafu Bernard Kamilius Membe juu ya mwenendo wa CCM chini ya Mwenyekiti Rais Magufuli na Katibu wa Itikadi na Uenezi H.Polepole.

1. VYAMA BORA.

Sanctity(usafi, utakatifu) Ideology (Itikadi, dira) na Organization( Mfumo.) Cold War iliigawa Dunia kwenye Makundi Mawili. East and West, yaani Wakomunist/ Wajamaa(East) vis a vis Capitalism.(West)(1) Vyama vya nchi za kibepari ni tofauti kabisa na vyama vya Kikomunist/ Kijamaa. Vyama vya kibepari vipo pale kwa ajili ya kuandaa kampeni na fedha kwa ajili ya kushinda uchaguzi ujao.

Mwenyekiti wa Chama hawi Rais. Ni Mtu anachaguliwa na mkutano Mkuu (Congress). Kazi zake ni tatu. 1. Kuandaa mkutano ujao wa Uchaguzi. 2. Kukusanya fedha za uchaguzi.3. Kuendesha mikutano ya Primaries(ya mchujo ).

Wanachama ni mashabiki wowote wa kadi tu wa mrengo huo. Mashabiki ndiyo wanatoa fedha za kumsaidia Mbunge ashinde uchaguzi. Mbunge hatoi fedha ili kupata Ubunge.Ndiyo maana husikii sana maneno ya rushwa.Kwa kifupi vyama vya kibepari havina mifumo kama ya vyama vyetu vya mrengo wa Kikomunist/ Kijamaa. Ni kwenye Mabunge yao tu ndiko vyama vyao huo na mfumo wa Party Caucus na vinajitokeza kupambana na wenzao. Na hata huko Bungeni, Mbunge anaweza ku- cross the party line yaani akaunga hoja ya upande mwingine na bado akabaki kwenye Chama chake.

Wabunge hao huitwa "rebels."(waasi)Hawafukuzani. Vyama cha kibepari havina mfumo unaolingana na Serikali wala kuwa na structure za Politburo, Central Committee au NEC. Wana mikutano ya Congress tu. Vyama cha havishiki hatamu za Uongozi. Rais akichaguliwa wanachama hawana lao tena. Wanawaachia wanachama wao Bungeni. Kwenye ngazi za Mikoa hivyo hivyo.Vyama havishiki hatamu. Hii ni part one.

Part two ndiyo inayotuhusu sisi. Hapa nitachambua sanctity, ideology na organisation na ubora wa vyama vyetu.

2. Vyama Vyetu. Ubora wa vyama vyetu vyenye uasilia wa Ukomunisti/ Ujamaa unategemea ushindi wake kwenye vigezo vitano vifuatavyo:

1. Clarity kwenye Itikadi yake. 2. Historia yake iliyotukuka. 3. Mfumo wake. 4. Wanachama wake. 5. Alama/ nembo za utambulisho wake. 1.Je Chama na Serikali yetu inafuata Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea? Ni kitendawili. Azimio la Arusha lipo? Wenzetu Wachina, Wacuba, Warusi, Wa Algeria, Waangola, wapo very clear! Ni Wajamaa kwa maneno na vitendo na Dunia inawatambua hivyo. Sisi tumeandika siasa yetu ni ya Ujamaa lakini tuna practise Free Market Economics ( soko huria)na Azimio la Arusha ni historia. Tunawashindaje hao vingunge kwa hili. 2. HISTORIA. Hapa ndipo penye nguvu ya CCM. Chama chetu kina historia ya Ukombozi kwa nchi yetu na nchi zinazotuzunguka. Heshima yetu ipo kwenye historia. Yaani Uzamani wetu. Huwezi kufuta Uzamani huo ukaleta Upya. Kufanya hivyo ni kujiua.Hapo tumewapiku wengi isipokuwa Cuba. 3.MFUMO. Wenzetu wana Politburo, Central Committee, NEC na Congress.Na wengi wa wanachama wana kofia mbili mbili.

Wajumbe wa Kamati juu kwa mfano, kuna mawaziri, Mabalozi na makatibu wakuu. Balozi Lukoki wa Angola nchini Tanzania kwa mfano, ni mjumbe wa Kamati juu ya MPLA. Wanafanya hivyo ili kuziongoza na kuzishauri Serikali zao ndani kwa ndani. Hawasubiri vikao. Sisi tunauondoa utaratibu huo. Nafasi yetu ya pili inatokana na nini? Mfumo wetu wa kutenganisha kofia? Aidha wenzetu wana utaratibu wa kusimamisha wagombea bila ya kuwashindanisha na wenzao wa Chama hicho hicho kwa baadhi ya majimbo wanayoamini wabunge wao wanafanya vizuri. Ni yale tu ambayo yana Wabunge lege lege ndiyo wanashindanisha wagombea kutoka Chama kimoja. Faida ya utaratibu huo ni kuleta Umoja ktk Chama, kutambua Wabunge wanaofanya vizuri na utaratibu huo unapunguza tuhuma au vitendo vya rushwa. Sisi hatufanyi hivyo. Tunapambanisha wagombea wetu ktk kila jimbo, vitendo vya rushwa vinakithiri,na wengine wanafitinishwa hata kama hawatoi rushwa n.k. Je hiki ni kigezo kinachotupa sifa Duniani? Wenzetu hawakubaliani nasi kwa hili.

4. WANACHAMA.

Sisi Chama chetu ni Mass party. Yaani "kumbakumba", ni Chama cha wengi na ili uwe mwanachama, wala jina lako haliendi Central Committee kuchunguzwa na kisha kupewa kadi ya Uanachama. Sisi ni matakwa yako. Hata mtu wa chama cha Upinzani kwa kutumwa au kujituma anaweza kujiunga na Chama chetu siku yoyote tena kwa sherehe na nderemo.Wenzetu kamwe hawafanyi hivyo. Utakuwa vetted ( kuchunguzwa kwa kina) kabla ya ombi lako la kutaka kujiunga na Chama kukubaliwa. Je hii ndiyo sifa inayotupa nafasi ya Ubora Duniani? Wenzetu hawakubali.

5. MAVAZI/ NEMBO. Kila Chama hujitambulisha kwa Mavazi na Nembo. Vitu hivi ni muhimu lakini hatushindanishwi navyo. La muhimu hapa ni kujua kuwa upya wa Chama hauwi kwenye mavazi, wala nembo wala watu wapya. Upya wa Chama chochote Duniani upo kwenye Historia yake, Itikadi yake na mfumo wake. Kama vitu hivyo vitatu ni constant ( yaani havibadiliki) badala yake tunabadilisha nembo, mavazi na watu, Chama chetu kitakuwa bado ni kile kile. Hakiwi kipya. Uzamani wa Chama ni kama mvinyo. Mvinyo wa zamani ni mtamu sana na una bei kubwa kuliko mpya. Nirudi kwenye hoja na nimalizie. Chama chetu lazima kiwe clear na Historia yake, Itikadi yake na Mfumo wake.

Historia yetu ipo clear lakini lazima tuiishi! Tukasema nini kuhusu Palestine, na Western Sahara kwa mfano. Vinginevyo tutakuwaje wa pili kwa Ubora? Tumejiondoa kwenye Open Government Forum ya Umoja wa Mataifa. Yaani hatutaki tufuatwe fuatwe kuhusu Good Governance na haki za binadamu. Tutasifiwaje? Pili Itikadi yetu haijawa clear. Tupo kama popo! Hatueleweki kama sisi ni ndege au Wanyama! Siasa ya Ujamaa kwenye vitabu na Soko huria kwenye maisha ya kila siku.Wapi na Wapi? Tukitangaza kuwa sisi tunafuata Siasa ya Ujamaa na tunarudisha Azimio la Arusha, Investors wote watakimbia kama bado hawajaanza. Ni itikadi gani tunayosifiwa nayo? Wenzetu China, Urusi, N.Korea, Cuba, Algeria,Ethiopia na Angola wana resources ambazo zipo tapped tayari na wanajitegemea. Ndiyo maana wametamka na kuyaishi matamko yao ya kufuata itikadi ya kikomunisti. Sisi hatujawa clear! Hatuwezi kuwashinda.

Mfumo wetu lazima uendane na maamuzi ya pamoja. Ni kikao gani kimeamua nini, lini, na kwa nini. Hakuna uamuzi wa mtu mmoja wala usio na kikao cha kikatiba. Kule Nje kwa hao wenzetu, kama Party Secretary General Hayupo kwa sababu yoyote ile, Central Committee haifanyiki siku hiyo.

The Party Secretary General is indispensable. Baada ya yote hayo, najiuliza ni kipi kinachofanya CCM iwe na Ubora wa pili baada ya China? Chama chetu lazima kipeleke vijana viongozi kama ndugu yetu Polepole Urusi, Cuba, N.Korea, Algeria, Angola, na Ethiopia ili kujifunza zaidi kwa faida ya Chama chetu na Taifa kwa ujumla.

Kidumu Chama cha Mapinduzi.
 
Mimi sina tatizo na wale wanaoikosoa CCM kwa sababu bila kukosolewa haiwezi kujitathmini, tatizo langu ni hawa wakosoaji wa kinafiki au wanaokosoa baada ya maslahi yao binafsi ndani ya CCM kuzibwa.

Benard Membe wakati akiishi angani na kubadilisha mabegi uwanja wa ndege hakuwahi kuona mapungufu ya CCM ili kuishauri CCM!

Leo yuko kwenye kijiwe ameanza kuona mapungufu ya CCM!

Kwa hiyo Membe wakati akiwa kwenye serikali na kuishi angani hakujua kuwa, ''Siasa ya Ujamaa kwenye vitabu na Soko huria kwenye maisha ya kila siku.Wapi na Wapi?''

Ukichunguza utagundua kuwa msingi wa andiko lake lipo kwenye maneno haya' Tumejiondoa kwenye Open Government Forum ya Umoja wa Mataifa. Yaani hatutaki tufuatwe fuatwe kuhusu Good Governance na haki za binadamu''. Haya mengine ni porojo tu za kuficha lengo lake kuu.

Open Government partnership ilikuwa legacy ya Membe na kundi lake na ndiyo ilimfanya kuishi angani huku akihudhuria mikutano na makongamano ya Open Government partnership.

Kuitetea hoja yake ya Open Government Partnership anataka kutuambia eti Algeria Ethiopia, Angola and et al zenyewe zinaweza kujitoa kwa sababu resources zake zimeshakuwa tapped! Ni resources zipi hizo zilizokuwa tapped ambazo Tanzania hazijakuwa tapped?

Masuala sijui ya Morroco akaihoji AU ambayo imeitambua Morocco na kuipa uanachama wa AU. Tanzania ni nchi mwanachama wa AU.

Katiba ya CCM katika Ibara ya 122(4) inasema, ‘’Manaibu Katibu Mkuu wa CCM watakuwa ndio wasaidizi wakuu wa Katibu Mkuu wa CCM na watafanya kazi zozote za CCM watakazopangiwa na Katibu Mkuu wa CCM’’.

Maneno ya msingi na muhimu katika ibara hii ni watafanya kazi zozote za CCM watakazopangiwa na Katibu Mkuu wa CCM.

Membe anatakiwa atuambie ni wapi kwenye Katiba ya CCM inasema, Kamati Kuu haiwezi kufanya vikao vyake kama Katibu Mkuu hayupo na majukumu ya vikao amewapa Manaibu Katibu Wakuu?

Tanzania bila unafiki haiwezekani!
 
Bernad Membe iwapo leo atapotea au kupigwa risasi itakuwa pigo kubwa kwa
wana Ccm wote wanaofikiri bado wanaweza kushawishi direction ya ccm na nchi
naona bado wako in denial....
waamke nyakati zishabadilka...sauti zao hazihitajiki sana now
 
Nafikiri Membe anajaribu "kukosoa" mabadiliko ya kichama yanayotaka kufanywa na Mwenyekiti mpya chini ya mtekelezaji na mpaza sauti wa Itikadi ya Chama ndugu Polepole.

Membe anajua namna walivyoikwepa Morocco kwa muda mrefu katika urafiki utakaoiathiri Western Sahara,ndio maana wakati ule,Kiongozi au "Rais" wa Western Sahara alifanya ziara ya kuja Tanzania chini ya uratibu wa Membe ili kusaruji msimamo wa Tanzania kuitambua Western Sahara na kuikanya Morocco kuikalia W.Sahara.

Juhudi zile za Membe,zimefifishwa na JPM...Kwa madoido tumemleta Mfalme wa Morocco,tukampa na eneo la kujenga uwanja,na pale AU-Addis Ababa tulimuhakikishia kumuunga mkono ili apate uanachama wa AU,kule Mashariki ya Kati tulikuwa upande wa Palestina,Mwalimu na Yasser Arafat walikuwa marafiki wa itikadi ya kupinga uonevu,sasa tumefungua ubalozi wa Israel Tanzania,huu ni ujumbe kwa Wapalestina kuwa CCM ya Mwalimu hadi JK si ile ya JPM...Hatujulikani kama popo,je sisi ni ndege au wanyama?

Tunaongoza chama bila Katibu Mkuu,hii si "kanuni" na "utamaduni" ya vyama vya kikomunist kama CCM.Katibu muenezi wa Itikadi na yeye hajui vizuri misingi na utamaduni wa chama,anatakiwa apelekwe nchi walimu wa CCM kujifunza "uhafidhina" wa vyama vya kikomunisti.

Maelezo ya Membe,yanahitimisha fununu za muda mrefu,kwamba wenye chama wanakitaka chama chao,kama ni mabadiliko,basi hukohuko serikalini...Lakini katika chama,wenye chama chao wanakitaka.Wanataka warudi kulekule kwenye uchama wao,kama hutaki,basi waachie chama chao we uendelee na urais wako.

Hiki chama kina wenyewe,wenyewe ndio hao wako nyuma ya kauli za Membe...Ni ngumu kutenganisha matamanio ya Membe na JK!!

Chama kina wenyewe jamani....
 
Uchambuzi Murwa..je aliwahi kuyasimamia? alipochukua billion 40 kutoka kw aGaddafi kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha cement Lindi na badala yake akajenga hotel za NAF beach na NAF apartment na Kuanzisha NAF security lakini pia akaagiza macontainer ya nguo za campaign kutoka china akijua tashinda..alikuwa anatekeleza falsafa ipi? Je alipotangaza Lowassa na wenzake ni Adui no moja alikuwa anatekeleza falsa ipi? Je alipodiverjisha pesa za mradi wa maji Lindi nakusababisha waziri Eng Lwenge kuachwa kwenye mbadiliko ya uwaziri unadhani alikuwa anatumia falsafa ipi?
 
Andiko zuri, lilijaa ubobevu. Nashawisha kuamini kuwa kwa level ya kufikiri inafana na mtu aliyewahi kuwa Mwanadiplomasia mzoefu na mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM. Lakini bado sijawashawisha na source ya hilo andiko.
 
Nafikiri Membe anajaribu "kukosoa" mabadiliko ya kichama yanayotaka kufanywa na Mwenyekiti mpya chini ya mtekelezaji na mpaza sauti wa Itikadi ya Chama ndugu Polepole.

Membe anajua namna walivyoikwepa Morocco kwa muda mrefu katika urafiki utakaoiathiri Souther Sahara,ndio maana wakati ule,Kiongozi au "Rais" wa Southern Sahara alifanya ziara ya kuja Tanzania chini ya uratibu wa Membe ili kusaruji msimamo wa Tanzania kuitambua Southern Sahara na kuikanya Morocco kuikalia S.Sahara.

Juhudi zile za Membe,zimefifishwa na JPM...Kwa madoido tumemleta Mfalme wa Morocco,tukampa na eneo la kujenga uwanja,na pale AU-Addis Ababa tulimuhakikishia kumuunga mkono ili apate uanachama wa AU,kule Mashariki ya Kati tulikuwa upande wa Palestina,Mwalimu na Yasser Arafat walikuwa marafiki wa itikadi ya kupinga uonevu,sasa tumefungua ubalozi wa Israel Tanzania,huu ni ujumbe kwa Wapalestina kuwa CCM ya Mwalimu hadi JK si ile ya JPM...Hatujulikani kama popo,je sisi ni ndege au wanyama?

Tunaongoza chama bila Katibu Mkuu,hii si "kanuni" na "utamaduni" ya vyama vya kikomunist kama CCM.Katibu muenezi wa Itikadi na yeye hajui vizuri misingi na utamaduni wa chama,anatakiwa apelekwe nchi walimu wa CCM kujifunza "uhafidhina" wa vyama vya kikomunisti.

Maelezo ya Membe,yanahitimisha fununu za muda mrefu,kwamba wenye chama wanakitaka chama chao,kama ni mabadiliko,basi hukohuko serikalini...Lakini katika chama,wenye chama chao wanakitaka.Wanataka warudi kulekule kwenye uchama wao,kama hutaki,basi waachie chama chao we uendelee na urais wako.

Hiki chama kina wenyewe,wenyewe ndio hao wako nyuma ya kauli za Membe...Ni ngumu kutenganisha matamanio ya Membe na JK!!

Chama kina wenyewe jamani....

Mkuu ni Western Sahara na siyo Southern Sahara.

Siasa ni unafiki tuu. Kila mtu anataka kula. Leo Membe angekuwa kwenye cabinet, believe me you, asingelalamika kwamba utaratibu unakiukwa. Again, all politics IS local.

Mwisho wa siku losers ni waTanzania wanaopiga makofi wakati wanaangamia kwa uzembe wa hawa hawa CCM.

Kama signature yangu inavyosema: Poverty is a crime!
 
Uchambuzi wa Waziri wa Mashauri ya Kigeni Mstaafu Bernard Kamilius Membe juu ya mwenendo wa CCM chini ya Mwenyekiti Rais Magufuli na Katibu wa Itikadi na Uenezi H.Polepole.

1. VYAMA BORA.

Sanctity(usafi, utakatifu) Ideology (Itikadi, dira) na Organization( Mfumo.) Cold War iliigawa Dunia kwenye Makundi Mawili. East and West, yaani Wakomunist/ Wajamaa(East) vis a vis Capitalism.(West)(1) Vyama vya nchi za kibepari ni tofauti kabisa na vyama vya Kikomunist/ Kijamaa. Vyama vya kibepari vipo pale kwa ajili ya kuandaa kampeni na fedha kwa ajili ya kushinda uchaguzi ujao.

Mwenyekiti wa Chama hawi Rais. Ni Mtu anachaguliwa na mkutano Mkuu (Congress). Kazi zake ni tatu. 1. Kuandaa mkutano ujao wa Uchaguzi. 2. Kukusanya fedha za uchaguzi.3. Kuendesha mikutano ya Primaries(ya mchujo ).

Wanachama ni mashabiki wowote wa kadi tu wa mrengo huo. Mashabiki ndiyo wanatoa fedha za kumsaidia Mbunge ashinde uchaguzi. Mbunge hatoi fedha ili kupata Ubunge.Ndiyo maana husikii sana maneno ya rushwa.Kwa kifupi vyama vya kibepari havina mifumo kama ya vyama vyetu vya mrengo wa Kikomunist/ Kijamaa. Ni kwenye Mabunge yao tu ndiko vyama vyao huo na mfumo wa Party Caucus na vinajitokeza kupambana na wenzao. Na hata huko Bungeni, Mbunge anaweza ku- cross the party line yaani akaunga hoja ya upande mwingine na bado akabaki kwenye Chama chake.

Wabunge hao huitwa "rebels."(waasi)Hawafukuzani. Vyama cha kibepari havina mfumo unaolingana na Serikali wala kuwa na structure za Politburo, Central Committee au NEC. Wana mikutano ya Congress tu. Vyama cha havishiki hatamu za Uongozi. Rais akichaguliwa wanachama hawana lao tena. Wanawaachia wanachama wao Bungeni. Kwenye ngazi za Mikoa hivyo hivyo.Vyama havishiki hatamu. Hii ni part one.

Part two ndiyo inayotuhusu sisi. Hapa nitachambua sanctity, ideology na organisation na ubora wa vyama vyetu.

2. Vyama Vyetu. Ubora wa vyama vyetu vyenye uasilia wa Ukomunisti/ Ujamaa unategemea ushindi wake kwenye vigezo vitano vifuatavyo:

1. Clarity kwenye Itikadi yake. 2. Historia yake iliyotukuka. 3. Mfumo wake. 4. Wanachama wake. 5. Alama/ nembo za utambulisho wake. 1.Je Chama na Serikali yetu inafuata Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea? Ni kitendawili. Azimio la Arusha lipo? Wenzetu Wachina, Wacuba, Warusi, Wa Algeria, Waangola, wapo very clear! Ni Wajamaa kwa maneno na vitendo na Dunia inawatambua hivyo. Sisi tumeandika siasa yetu ni ya Ujamaa lakini tuna practise Free Market Economics ( soko huria)na Azimio la Arusha ni historia. Tunawashindaje hao vingunge kwa hili. 2. HISTORIA. Hapa ndipo penye nguvu ya CCM. Chama chetu kina historia ya Ukombozi kwa nchi yetu na nchi zinazotuzunguka. Heshima yetu ipo kwenye historia. Yaani Uzamani wetu. Huwezi kufuta Uzamani huo ukaleta Upya. Kufanya hivyo ni kujiua.Hapo tumewapiku wengi isipokuwa Cuba. 3.MFUMO. Wenzetu wana Politburo, Central Committee, NEC na Congress.Na wengi wa wanachama wana kofia mbili mbili.

Wajumbe wa Kamati juu kwa mfano, kuna mawaziri, Mabalozi na makatibu wakuu. Balozi Lukoki wa Angola nchini Tanzania kwa mfano, ni mjumbe wa Kamati juu ya MPLA. Wanafanya hivyo ili kuziongoza na kuzishauri Serikali zao ndani kwa ndani. Hawasubiri vikao. Sisi tunauondoa utaratibu huo. Nafasi yetu ya pili inatokana na nini? Mfumo wetu wa kutenganisha kofia? Aidha wenzetu wana utaratibu wa kusimamisha wagombea bila ya kuwashindanisha na wenzao wa Chama hicho hicho kwa baadhi ya majimbo wanayoamini wabunge wao wanafanya vizuri. Ni yale tu ambayo yana Wabunge lege lege ndiyo wanashindanisha wagombea kutoka Chama kimoja. Faida ya utaratibu huo ni kuleta Umoja ktk Chama, kutambua Wabunge wanaofanya vizuri na utaratibu huo unapunguza tuhuma au vitendo vya rushwa. Sisi hatufanyi hivyo. Tunapambanisha wagombea wetu ktk kila jimbo, vitendo vya rushwa vinakithiri,na wengine wanafitinishwa hata kama hawatoi rushwa n.k. Je hiki ni kigezo kinachotupa sifa Duniani? Wenzetu hawakubaliani nasi kwa hili.

4. WANACHAMA.

Sisi Chama chetu ni Mass party. Yaani "kumbakumba", ni Chama cha wengi na ili uwe mwanachama, wala jina lako haliendi Central Committee kuchunguzwa na kisha kupewa kadi ya Uanachama. Sisi ni matakwa yako. Hata mtu wa chama cha Upinzani kwa kutumwa au kujituma anaweza kujiunga na Chama chetu siku yoyote tena kwa sherehe na nderemo.Wenzetu kamwe hawafanyi hivyo. Utakuwa vetted ( kuchunguzwa kwa kina) kabla ya ombi lako la kutaka kujiunga na Chama kukubaliwa. Je hii ndiyo sifa inayotupa nafasi ya Ubora Duniani? Wenzetu hawakubali.

5. MAVAZI/ NEMBO. Kila Chama hujitambulisha kwa Mavazi na Nembo. Vitu hivi ni muhimu lakini hatushindanishwi navyo. La muhimu hapa ni kujua kuwa upya wa Chama hauwi kwenye mavazi, wala nembo wala watu wapya. Upya wa Chama chochote Duniani upo kwenye Historia yake, Itikadi yake na mfumo wake. Kama vitu hivyo vitatu ni constant ( yaani havibadiliki) badala yake tunabadilisha nembo, mavazi na watu, Chama chetu kitakuwa bado ni kile kile. Hakiwi kipya. Uzamani wa Chama ni kama mvinyo. Mvinyo wa zamani ni mtamu sana na una bei kubwa kuliko mpya. Nirudi kwenye hoja na nimalizie. Chama chetu lazima kiwe clear na Historia yake, Itikadi yake na Mfumo wake.

Historia yetu ipo clear lakini lazima tuiishi! Tukasema nini kuhusu Palestine, na Western Sahara kwa mfano. Vinginevyo tutakuwaje wa pili kwa Ubora? Tumejiondoa kwenye Open Government Forum ya Umoja wa Mataifa. Yaani hatutaki tufuatwe fuatwe kuhusu Good Governance na haki za binadamu. Tutasifiwaje? Pili Itikadi yetu haijawa clear. Tupo kama popo! Hatueleweki kama sisi ni ndege au Wanyama! Siasa ya Ujamaa kwenye vitabu na Soko huria kwenye maisha ya kila siku.Wapi na Wapi? Tukitangaza kuwa sisi tunafuata Siasa ya Ujamaa na tunarudisha Azimio la Arusha, Investors wote watakimbia kama bado hawajaanza. Ni itikadi gani tunayosifiwa nayo? Wenzetu China, Urusi, N.Korea, Cuba, Algeria,Ethiopia na Angola wana resources ambazo zipo tapped tayari na wanajitegemea. Ndiyo maana wametamka na kuyaishi matamko yao ya kufuata itikadi ya kikomunisti. Sisi hatujawa clear! Hatuwezi kuwashinda.

Mfumo wetu lazima uendane na maamuzi ya pamoja. Ni kikao gani kimeamua nini, lini, na kwa nini. Hakuna uamuzi wa mtu mmoja wala usio na kikao cha kikatiba. Kule Nje kwa hao wenzetu, kama Party Secretary General Hayupo kwa sababu yoyote ile, Central Committee haifanyiki siku hiyo.

The Party Secretary General is indispensable. Baada ya yote hayo, najiuliza ni kipi kinachofanya CCM iwe na Ubora wa pili baada ya China? Chama chetu lazima kipeleke vijana viongozi kama ndugu yetu Polepole Urusi, Cuba, N.Korea, Algeria, Angola, na Ethiopia ili kujifunza zaidi kwa faida ya Chama chetu na Taifa kwa ujumla.

Kidumu Chama cha Mapinduzi.
Katibu Mkuu anauguliwa na mtoto wake huko South Africa ulitakaje sasa?
 
Benard Membe wakati akiishi angani na kubadilisha mabegi uwanja wa ndege hakuwahi kuona mapungufu ya CCM ili kuishauri CCM.

Leo yuko kwenye kijiwe ameanza kuona mapungufu ya CCM!

Ukichunguza utagundua kuwa msingi wa andiko lake lipo kwenye maneno haya' Tumejiondoa kwenye Open Government Forum ya Umoja wa Mataifa. Yaani hatutaki tufuatwe fuatwe kuhusu Good Governance na haki za binadamu''. Haya mengine ni porojo tu za kuficha lengo lake kuu.

Katiba ya CCM katika Ibara ya 122(4) inasema, ‘’Manaibu Katibu Mkuu wa CCM watakuwa ndio wasaidizi wakuu wa Katibu Mkuu wa CCM na watafanya kazi zozote za CCM watakazopangiwa na Katibu Mkuu wa CCM’’.

Maneno ya msingi katika ibara hii ni watafanya kazi zozote za CCM watakazopangiwa na Katibu Mkuu wa CCM.

Tanzania bila unafiki haiwezekani!
Msome vizuri Membe katikati ya mistari. Sidhani kama Membe hajui hizo ibara, anazijua kabisa.

Hapo kuna sauti ya "wenye chama". Imesemwa kupitia "Mtu wa chama". Ukimsoma zaidi utaona ni kama katibu Mkuu ana baraka za hayo aliyoandika.

Huwezi kupuuza historia na tamaduni za uendeshaji. Ndivyo alivyoelezea komredi
 
Heshima yako komredi.


Nafikiri Membe anajaribu "kukosoa" mabadiliko ya kichama yanayotaka kufanywa na Mwenyekiti mpya chini ya mtekelezaji na mpaza sauti wa Itikadi ya Chama ndugu Polepole.

Membe anajua namna walivyoikwepa Morocco kwa muda mrefu katika urafiki utakaoiathiri Souther Sahara,ndio maana wakati ule,Kiongozi au "Rais" wa Southern Sahara alifanya ziara ya kuja Tanzania chini ya uratibu wa Membe ili kusaruji msimamo wa Tanzania kuitambua Southern Sahara na kuikanya Morocco kuikalia S.Sahara.

Juhudi zile za Membe,zimefifishwa na JPM...Kwa madoido tumemleta Mfalme wa Morocco,tukampa na eneo la kujenga uwanja,na pale AU-Addis Ababa tulimuhakikishia kumuunga mkono ili apate uanachama wa AU,kule Mashariki ya Kati tulikuwa upande wa Palestina,Mwalimu na Yasser Arafat walikuwa marafiki wa itikadi ya kupinga uonevu,sasa tumefungua ubalozi wa Israel Tanzania,huu ni ujumbe kwa Wapalestina kuwa CCM ya Mwalimu hadi JK si ile ya JPM...Hatujulikani kama popo,je sisi ni ndege au wanyama?

Tunaongoza chama bila Katibu Mkuu,hii si "kanuni" na "utamaduni" ya vyama vya kikomunist kama CCM.Katibu muenezi wa Itikadi na yeye hajui vizuri misingi na utamaduni wa chama,anatakiwa apelekwe nchi walimu wa CCM kujifunza "uhafidhina" wa vyama vya kikomunisti.

Maelezo ya Membe,yanahitimisha fununu za muda mrefu,kwamba wenye chama wanakitaka chama chao,kama ni mabadiliko,basi hukohuko serikalini...Lakini katika chama,wenye chama chao wanakitaka.Wanataka warudi kulekule kwenye uchama wao,kama hutaki,basi waachie chama chao we uendelee na urais wako.

Hiki chama kina wenyewe,wenyewe ndio hao wako nyuma ya kauli za Membe...Ni ngumu kutenganisha matamanio ya Membe na JK!!

Chama kina wenyewe jamani....
 
Back
Top Bottom