Bernard Membe: Nina maadui 11, ikifika 2016 watakimbilia Kenya!

Mh. Membe ndani ya ITV ktk kipindi cha dak 45, akilalamika jinsi maadaui wake walivyomsingizia kuwa kaiba pesa za walibya. Amesema ana wabaya wake 11 ambao ndani yake yupo Mohammed Enterprises, wahariri wawili na baadhi ya vigogo wa CCM. Amesema kuwa aliwasaidia chakula vijana wa CHADEMA waliokuwa na njaa, lakini akatafsiriwa vibaya na maadui zake. Kuhusu urais 2015 amemtaka mtangazaji amsalie sana. Ameomba wanachi wasimlalamikie rais kwa hali mbaya ya nchi (ingawa hajasema ni nani wa kulalamikiwa). Anaamini CCM itaimarika baada ya uchaguzi wa Chama mwaka huu. Amewabeza wabunge hasa wa upinzani kwa kusema sana bungeni wakati bajeti bi ya CCM. Amewasifu baadhi ya madaktari kwa kurudi kazini na akasema huo ni wito, na watumikie wito huo walioitiwa na Mungu kwani malipo yao yapo Mbinguni. ndo anamalizia mahojiano kwa kututaka tuheshimu mamlaka ya nchi.
 
Yawezekana Mh Membe akaiokoa CCM, kama hataenda upinzani, he is a great thinker. Nimependa sana mazungumzo ya kipindi hiki cha Dk 45, Mh Membe amenigusa sana, ingawa si kila kitu ninakubaliana nae, ila mwenye hekima hatapingana nami. Kuna mengi vyama vingine kujifunza kwa Mh Membe.
 
Mh anasema wabunge wapinzani ni wasemaji hodari wa kusema bungeni lakini kwenye majimbo yao hawajafanya chochote?

sasa yeye mtama amefanya nini????halafu serikali ndo ina wajibu wa kufanya chochote,,,wabunge wao wanapeleka kero,,,,MEMBE HAJUI AU ???????
 
Pesa ya wa libya kala yeye na hao waarab meis!kiwanda kipo wapi cha fedha iliyotolewa?ushahidi upo wa mgao wa hiyo fedha
 
Kama yeye amefanya ni kwa pesa ya ufisadi, na kanisa walikataa kusalia kanisa la milion 600 walisema aseme kapata wapi hiyo pesa mpaka leo hajajibu.
 
Ningeruhusiwa kumwuliza maswali Membe angekimbia kama Rage na Ndolanga enzi zile za FAT. Kuna vitu vingi sana ambavyo alitakiwa avitolee maelezo siyo hizo simple questions..za kuoteshwa kugombea Urais..
 
meis wakashinda nini?maana ni pesa za kujenga kiwanda cha cement lindi,jee kiwanda kimejengwa?mimi nina ushahidi membe na meis wamegawana pesa hiyo!atueleze pesa zipo wapi kwa sasa?zinafanya nini?

mwaga hapa ushaidi
 
Naomba Mheshimiwa Membe aelewe kuwa kila mtanzania kwa majimbo yote ya nchi hii analipa kodi, kodi hii inakwenda serikalini, mwisho wa siku serikali inagawa kwa maendeleo ya maeneo tofauti kulingana na utashi wa viongozi wa wizara husika. Kauli ya Membe kupitia kipindi cha DK 45 ITV kuwa tuwapime wabunge wa upinzani kwa kuangalia maendeleo ya majimbo yako haina maana kabisa. Tuwe wa kweli Membe na Mnyika waende wizara ya ujenzi kuomba fedha za ujenzi wa barabara jimboni NANI ATAPEWA UMUHIMU? Tuache ujinga wa kufikiri eti tuwapime kimajimbo. Walahi kakiyamungu Kiama chenu kimefika.
 
Huyu muoteshwa njozi/ndoto ameanza kuweweseka, labda anakaribia kuoteshwa...
 
Katika Kipindi cha dak 45 (ITV) Membe kashauri eti Bunge lianzishe utaratibu wa maswali ya papo kwa papo kwa kiongozi wa Upinzani Bungeni.

Hivi kiongozi wa kambi ya upinzani aulizwe maswali ganii kwani kambi hiyo haina serikali na kuwa na hela za walipa za walipa kodi!

Naanza kumdharau!
 
Membe leo ITV anasema eti wabunge waonyeshe umahiri majimboni na si bungeni kitu ambacho sio sahihi,Semunyu haulizi hata maswali.
 
Kashauri vizuri saana, naninampongeza kwani CDM inahitaji airtime ya kutosha kukamilisha mkakati makini wa kuingia ikulu, Hio nafasi ikitokea tutakufikia lengo hata kabla ya wakati,
 
It is a good idea............actually brilliant one

BUT Content ipi ataulizwa ndo swali langu..............au mbadala wa sera zilizopo?????
 
Hana akili za kujua adui yake namba 1 ni yeye mwenyewe na hii inatokana na ccm na membe kuasisi siasa za makundi yasiyokufa ndani ya ccm,
 
Membe ataikoa ccm kama hatakwenda cdm, lkn nadhani anakosea kutaja wanaochafua, watanzania wanahtaji majina ya wezi wa fedha za Rada. Hebu nao wataje. Lkn member wa jf mmegundua membe ana bifu na lowasa, mengi na wote wenye watumiao vyombo vya habari kuhari mfumo wa uongozi? Karibu CDM Membe
 
Katika Kipindi cha dak 45 (ITV) Membe kashauri eti Bunge lianzishe utaratibu wa maswali ya papo kwa papo kwa kiongozi wa Upinzani Bungeni.

Hivi kiongozi wa kambi ya upinzani aulizwe maswali ganii kwani kambi hiyo haina serikali na kuwa na hela za walipa za walipa kodi!

Naanza kumdharau!

Hapa naona kama Membe ametumia nguvu kubwa sana kufikiria ili aonekane ni mwanasiasa mbunifu! Waziri mkuu ni kiongozi wa shughuli za serikali bungeni. Maswali kwa waziri mkuu ni kutoka kwa wawakilishi wa wananchi kwenda kwa mpokea/mtumia kodi (executive rep) ambaye ni waziri mkuu. Kupitia kwa wawakilishi wao wananchi wanauliza ukekelezaji wa miradi mbalimbali.

Sasa anataka mkuu wa kambi ya upinzani aulizwe nini kama si kutaka kutumia muda wa wananchi vibaya huko bungeni? Upinzani wanakusanya kodi? Upinzani wanaandaa sera? Upinzani wana-sign mikataba na makampuni ya nje au wanatoa misamaha ya kodi? Upinzani wanandaa sera? CCM wana tatizo gani?
 
shida ya huyo dogo wa ITV anauliza leading questions zaidi...anashindwa kuuliza maswali ya kumfanya mtu afunguke zaidi.

ana opportunity kubwa sana huyu dogo lakini haitumii...sorry for him.

Ni kweli mkuu, zamani alikuwa anauliza very technical and challenging questions, lakini siku hizi anauliza maswali dhaifu dhaifu tu!
 
Back
Top Bottom