Mgambilwa ni mntu
JF-Expert Member
- May 30, 2017
- 2,869
- 3,188
Siasa za korosho zimemuinua zaidi Rais Magufuli na kumdhohofisha zaidi Bernard Membe katika ngome yake.
Kumekuwepo na tetesi kuwa, Bernard Membe, pamoja na mtandao wa watu wake wakiwemo, Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, Mbunge wa Mtwara Vijijini, Hawa Ghasia na wengine wanaotokea Mikoa ya Ukanda wa Pwani; hawakufurahishwa na uamuzi wa Serikali ya Awamu ya Tano, chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli wa kununua korosho kwa wakulima tena kwa bei ya juu kuliko iliyokuwa imepangwa hapo awali.
Maneno aliyoongea Nape Nnauye bungeni yanaonyesha wazi kuwa bado hawakufurahishwa na uamuzi wa Serikali kununua korosho kwani Nape badala ya kufafanua uamuzi wa Serikali kuamua kununua korosho tena kwa bei ya juu, yeye:
- Aliwasifia wakulima kwa kuwa wavumilivu na watulivu.
- Kukosoa Serikali kuwa, haikutumia busara kushughulikia sakata la korosho.
- Kuitaka Serikali inunue haraka korosho ili wakulima wasipate hasara zaidi.
- Halmashauri kuingia hasara kutokana na kutegemea korosho.
Aidha, akiwa ziarani mkoani Arusha, Rais Dk. John Pombe Magufuli aliwatuhumu baadhi ya wanasiasa kwa kutaka kuihujumu Serikali katika uuzaji wa zao la korosho. Alisema kuwa, baadhi yao walinunua korosho changa kwa wakulima katika mfumo wa kangemba na sasa wanataka kuiuza wakati hawana mashamba. Rais alisema korosho itakayonunuliwa ni ile ya wale watakaoonyesha mashamba yao na watakaoshindwa kuonyesha mashamba yao, korosho yao itataifishwa.
Hivyo, ni wazi kuwa, wanasiasa wa Mikoa ya Kusini anakotokea Membe na Nape, walijisikia vibaya sana kuona Serikali ikiamua kununua korosho tena kwa bei ya Tsh. 3,300.
So alichofanya Dk. Bashiru ni mwendelezo wa hatua za kisiri siri za kundi la Membe kuihujumu Serikali ya Awamu ya Tano, tena kwa kusaidiwa na baadhi ya Makada wa Chama, ambao wengi wao ndio waliokuwa Viongozi kwenye utawala uliopita na ambao wameachwa ama kutumbuliwa katika Awamu ya Tano.
Hata kujiuzulu nafasi ya uenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Hawa Ghasia ni kutokana kushindwa kwake kuishauri Serikali kwa kuwa, alikuwa katika kundi linalohujumu Serikali.
Kwa ujumla, kitendo cha Rais Dk. John Pombe Magufuli kuamua kununua korosho tena kwa bei ya juu ya Tsh. 3,300 kimewaacha Wapinzani wake ndani ya CCM midomo wazi kwani hawakutegemea kabisa kuwa, Serikali ingekuwa tayari kwenda that extra mile. Walijidai kumu-beep Magufuli, naye akawapigia - sasa wanaugulia mioyoni mwao.
Na ghafula Kanda ya Ziwa, Kanda Kati, Kanda ya Kusini na Kanda ya Magharibi zimeenda kwa Magufuli huku Nyanda za Juu yote (isipokuwa Mbeya) ikiwa pia kwa Omuzilankende. Kanda ipi imebaki? Huko Kaskazini baada ya CHADEMA kumkorofisha na kumdharau Lowassa, ni wazi 2020, itakuwa nusu kwa nusu.
Ngoja tuone!!