Bernard Membe haitaki Dodoma

Nikupateje

JF-Expert Member
Dec 22, 2009
1,334
988
Mnaokumbuka sakata la Hans Kitine kuhusu madai ya hongo ile mwaka 2002 lilipigwa msumari na Bernard Membe alivyotos ushahidi mzito wa jinsi Kitine alivyohusika na madai yale.

Baada ya wiki moja Membe alipata nafasi a mahojiano na gazeti moja kuhusu suala hilo na pia kuhusu masuala mbalimbali ya Wizara ya mambo ya nje ambayo wakati huo ilikuwa chini ya Waziri Jakya Kikwete.

Katika masuala ya nyongeza mwandishi akataka kujua maoni ya Membe kuhusu suala la serikali kuhamia Dodoma ambako ni TAMISEMI tu walioko kule.

Mambe alijibu kwamba yeye kwa maoni yake anaona kwamba suala hilo limebaki kama porojo la kisiasa na utekelezaji wake ni dhahiri umedorora. Akaongeza kwamba "inatubidi tukiri na kukubali kwamba tumeshidwa kuhamia Dodoma".

Hivyo, Membe huo ndiyo msimamo alioutoa kuhusu kuifanya Dodoma kuwa makazi ya serikali.

Bahati mbaya Membe si raisi wa Tanzania. Angepata au akipata huo ndiyo msimamo wake. Kuachana na suala la Dodoma.

Wadau mnasemaje ukizingatia mbio za urais wa 2015 ndani ya CCM
 
Mnaokumbuka sakata la Hans Kitine kuhusu madai ya hongo ile mwaka 2002 lilipigwa msumari na Bernard Membe alivyotos ushahidi mzito wa jinsi Kitine alivyohusika na madai yale.

Baada ya wiki moja Membe alipata nafasi a mahojiano na gazeti moja kuhusu suala hilo na pia kuhusu masuala mbalimbali ya Wizara ya mambo ya nje ambayo wakati huo ilikuwa chini ya Waziri Jakya Kikwete.

Katika masuala ya nyongeza mwandishi akataka kujua maoni ya Membe kuhusu suala la serikali kuhamia Dodoma ambako ni TAMISEMI tu walioko kule.

Mambe alijibu kwamba yeye kwa maoni yake anaona kwamba suala hilo limebaki kama porojo la kisiasa na utekelezaji wake ni dhahiri umedorora. Akaongeza kwamba "inatubidi tukiri na kukubali kwamba tumeshidwa kuhamia Dodoma".

Hivyo, Membe huo ndiyo msimamo alioutoa kuhusu kuifanya Dodoma kuwa makazi ya serikali.

Bahati mbaya Membe si raisi wa Tanzania. Angepata au akipata huo ndiyo msimamo wake. Kuachana na suala la Dodoma.

Wadau mnasemaje ukizingatia mbio za urais wa 2015 ndani ya CCM


Sasa hapo unamuataki membe kwa lipi, yeye kasema ukweli uliopo. Dodoma ni ya leo? tangu enzi za muasisi wa Dodoma hakwenda, mwinyi hakwenda,mkapa hakwenda,kikwete hakwenda, sasa akwende nani? Dodoma haikaliki/hailipi labda CDM.
 
Kama Membe alisema hivyo then he is right. Suala la kuhamia Dodoma ni porojo tuu. Tena Bunge kuwa Dodoma linatugharimu sana. Fikiria ni kiasi gani cha fedha tunapoteza kwa mawaziri na watumishi wengine wa serikali kwenda Dodoma kwa ajili ya vikao vya bunge. Kwa vile wizara bado zipo Dar ingekuwa bora kama bunge lingehamishiwa Dar. Ni cheaper kuhamishia bunge Dar kuliko kugharamia mawaziri na watumishi wa serkilali kwenda Dodoma kwa ajili ya vikao vya bunge.

Hata hivyo, kama Membe akiwa rais, hawezi kuongoza hii nchi kwa matakwa yake binafsi bali kwa matakwa ya Watanzania.
 
Mnaokumbuka sakata la Hans Kitine kuhusu madai ya hongo ile mwaka 2002 lilipigwa msumari na Bernard Membe alivyotos ushahidi mzito wa jinsi Kitine alivyohusika na madai yale.

Baada ya wiki moja Membe alipata nafasi a mahojiano na gazeti moja kuhusu suala hilo na pia kuhusu masuala mbalimbali ya Wizara ya mambo ya nje ambayo wakati huo ilikuwa chini ya Waziri Jakya Kikwete.

Katika masuala ya nyongeza mwandishi akataka kujua maoni ya Membe kuhusu suala la serikali kuhamia Dodoma ambako ni TAMISEMI tu walioko kule.

Mambe alijibu kwamba yeye kwa maoni yake anaona kwamba suala hilo limebaki kama porojo la kisiasa na utekelezaji wake ni dhahiri umedorora. Akaongeza kwamba "inatubidi tukiri na kukubali kwamba tumeshidwa kuhamia Dodoma".

Hivyo, Membe huo ndiyo msimamo alioutoa kuhusu kuifanya Dodoma kuwa makazi ya serikali.

Bahati mbaya Membe si raisi wa Tanzania. Angepata au akipata huo ndiyo msimamo wake. Kuachana na suala la Dodoma.

Wadau mnasemaje ukizingatia mbio za urais wa 2015 ndani ya CCM

Alisema kweli kuwa mchakato wa kuhamia dom unasuasua.
Lakini sio msimamo wake.
Umetumwa kumchafua inaonekana.
OTIS.
 
Namtetea Membe.

Mwinyi, Mkapa na Kikwete wote kwa wakati mbalimbali walisema kuwa serikali kuhamia Dodoma ni kipaumbele cha taifa, na kitatekelezwa wakati wa uongozi wao. Sasa ni miaka 26 toka Mwinyi alivyosema hivyo, ni miaka 16 toka Mkapa alivyosema hivyo, na ni miaka 6 toka Kikwete alivyosema hivyo. Na hakuna hata mmoja wao alihamia au amehamia Dodoma. Na wote watatu wametumia mabilioni kukarabati Magogoni, badala ya kujenga mpya Kizota.

Tukubali, tusikubali kuhamia Dodoma iliondoka na Mwalimu JKN na Membe kama akiwa Raisi hatafanya tofauti na waliomtangulia. Na pia kama taifa, ni lazima tulielewe na kulikubali hilo.
 
Dodma zaidi ya chakochako hamna cha maana cha kutufanya tuhamie huko. Check majengo ya ukweli yanavyooteshwa dar.
 
Namtetea Membe.

Mwinyi, Mkapa na Kikwete wote kwa wakati mbalimbali walisema kuwa serikali kuhamia Dodoma ni kipaumbele cha taifa, na kitatekelezwa wakati wa uongozi wao. Sasa ni miaka 26 toka Mwinyi alivyosema hivyo, ni miaka 16 toka Mkapa alivyosema hivyo, na ni miaka 6 toka Kikwete alivyosema hivyo. Na hakuna hata mmoja wao alihamia au amehamia Dodoma. Na wote watatu wametumia mabilioni kukarabati Magogoni, badala ya kujenga mpya Kizota.

Tukubali, tusikubali kuhamia Dodoma iliondoka na Mwalimu JKN na Membe kama akiwa Raisi hatafanya tofauti na waliomtangulia. Na pia kama taifa, ni lazima tulielewe na kulikubali hilo.

Kum link Membe na kutohamia dom ni makosa yaliyofanywa na mwandishi ndio maana inakuwa ngumu kujua nini agenda yake ya siri.
OTIS.
 
Alichoeleza ndio ukweli wenyewe. Au unataka adanganye kama Mkapa na Kikwete walivyofanya?
 
wazo la kuhamia dodoma lilikuwa zuri kwa wakati ule (1973), ila sababu za kuhamia hazikuwa za msingi. Serikali kupitia CCM ilianzisha mamlaka kwa ajili ya kuendeleza dodoma CDA(Capital Development Authority), zilichangwa fedha za lazima kutoka kwa kila mwananchi nchi nzima, pesa nyingi zilitumika katika matumizi yasiyo sahihi, utajiri mkubwa uliopo katika chama cha mapinduzi unatokana na fedha hizi, watendaji wengi wa iliyo kuwa CDA waliishia kuwa matajiri wakubwa, kwa miaka yote hakuna jambo la maana lililofanyika Dodoma, walifanikiwa kujenga magorofa mengi ambayo wala hayana wapangaji.

Baada ya ukombozi wa tanganyika hapo 2015, itabidi wote walio husika kuhujumu mpango wa CDA washitakiwe, ccm itaifishiwe mali yake, ambayo ilichuma kupitia serikali kutoka kwa wananchi ambao hata kama walikuwa hawaipendi ccm, walilazimishwa kuipenda.


Ajabu ni kuwa mpaka sasa japokuwa hakuna la maana linalofanyika lakini bado kuna menejimenti ya CDA na bado wanaendelea kula fuba tu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom