Elections 2010 Benson bana anapoanza kujipendekeza kwa Dr Slaa na CHADEMA

Manyanza

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
8,881
12,540
MWENYEKITI mwenza wa Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (REDET) na mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Siasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, amesifu kampeni za aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, akisema zimetoa fundisho kubwa kwa vyama na wagombea wao.

Dk. Bana, ambaye amemmwagia sifa Dk. Slaa, alisema hayo jana alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Jambo kinachorushwa hewani na Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC).

Alisema kuna haja ya kujiuliza kwanini CHADEMA ambayo katika uchaguzi wa mwaka 2005 ilishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 668,756 sawa na asilimia 5.8, lakini katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu imepata kura zaidi ya milioni mbili, sawa na asilimia 26.5.

"Hili ni jambo zuri, linatufundisha nini, ukiwa na timu nzuri ya kampeni ukatembea maeneo mengi na kutoa sera zinazowagusa wananchi, utasikika na kuna uwezekano mkubwa wa kufanya vizuri kama tulivyoona kwa CHADEMA, hili ni fundisho kubwa hasa kwa wagombea na vyama vyao," alisema Dk. Bana.

Alisema Dk. Slaa alidhihirisha umahiri wake wakati akiwa bungeni, hasa aliposimamia kidete suala la ufisadi, ambalo wakati wa kampeni alilinadi pia kwa wananchi na kuahidi kulitatua iwapo atapewa ridhaa ya kuingia ikulu na wananchi.

Alibainisha kuwa kama wagombea wote wangekuwa kama alivyokuwa Dk. Slaa, uchaguzi wa mwaka huu ungekuwa na ushindani mkubwa na hata rais angepatikana kwa tofauti ya kura chache kama ilivyotokea Zanzibar.

Alisema miongoni mwa sera za CHADEMA zilioonekana kuwagusa wananchi ni utoaji wa elimu bure, ambayo hata hivyo ilikuwa ikibezwa na baadhi ya wagombea na makada wa vyama Fulani, kwa madai kuwa haitekelezeki, bali ni hadaa ya Dk. Slaa na chama chake ili wapate kura.

Alisema matokeo ya uchaguzi ambayo yaliipa CHADEMA viti visivyopungua 22 na Chama cha Wananchi (CUF) viti 24 yatachangia kwa kiasi kikubwa kuleta upinzani wa hoja bungeni na kulifanya Bunge litakaloanza kesho mkoani Dodoma kuwa la uwajibikaji zaidi, tofauti na ilivyozoeleka kipindi cha nyuma.

"Profile ya wabunge hasa wa CHADEMA na NCCR Mageuzi ni nzuri, inavuta na kutia moyo, tunatarajia Bunge lenye mvuto na ushindani mkali wa hoja ," alisema Dk. Bana.

Katika hatua nyingine, Dk. Bana alielezea kukerwa na tabia ya baadhi ya watendaji wa serikali kutumia magari ya umma kuendesha kampeni za aliyekuwa mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete.

"Vyombo vya serikali kutumika katika kampeni si jambo zuri katika uwanja wa siasa, hili linawanyima fursa wagombea wa vyama vingine kushiriki kwenye uwanja ulio sawa," alisema Dk. Bana.

Alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu mwamko mdogo wa wananchi kujitokeza kupiga kura, alisema jambo hilo linatakiwa kufanyiwa utafiti wa kina ili kubaini chanzo cha watu kutojitokeza kupiga kura, licha ya kuwapo idadi kubwa ya waliojiandikisha.

Alibainisha kuwa pamoja na wagombea kuzunguka maeneo mbalimbali ya hapa nchini kwa kutumia usafiri tofauti ukiwamo wa magari, helikopta, ndege, pikipiki na vifaa vinginevyo ili mradi kuwafikia wananchi, bado wahusika wameshindwa kujitokeza kwa wingi wakati wa zoezi la upigaji kura.

Dk. Bana pia alitumia fursa hiyo kuzungumzia suala la uharibikaji wa kura za urais, ambapo alisema kuwa uchaguzi wa mwaka huu tatizo hilo limepungua kwa kiasi kikubwa tofauti na chaguzi zilizopita.

"Kura zilizoharibika kwa mwaka huu ni 227,889 ambazo ni sawa na asilimia 2.64, tofauti na mwaka 2005, ambapo asilimia ya kura zilizoharibika ilikuwa 4.9, nawapongeza wahusika kwa hatua hii," alisema Dk. Bana.

Alibainisha kuwa kuna haja ya elimu ya uraia na ya uchaguzi kuwa endelevu ili kuwafanya wananchi kupata uelewa wa kutosha badala ya elimu hiyo kutolewa kwa mtindo wa zimamoto kila unapofika wakati wa uchaguzi.

Aliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kurekebisha kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika uchaguzi huu, pia kuwataka wananchi kutosubiri kusukumwa hasa katika kufanya jambo lenye maendeleo.
 
MWENYEKITI mwenza wa Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (REDET) na mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Siasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, amesifu kampeni za aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, akisema zimetoa fundisho kubwa kwa vyama na wagombea wao.

Dk. Bana, ambaye amemmwagia sifa Dk. Slaa, alisema hayo jana alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Jambo kinachorushwa hewani na Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC).

Alisema kuna haja ya kujiuliza kwanini CHADEMA ambayo katika uchaguzi wa mwaka 2005 ilishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 668,756 sawa na asilimia 5.8, lakini katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu imepata kura zaidi ya milioni mbili, sawa na asilimia 26.5.

"Hili ni jambo zuri, linatufundisha nini, ukiwa na timu nzuri ya kampeni ukatembea maeneo mengi na kutoa sera zinazowagusa wananchi, utasikika na kuna uwezekano mkubwa wa kufanya vizuri kama tulivyoona kwa CHADEMA, hili ni fundisho kubwa hasa kwa wagombea na vyama vyao," alisema Dk. Bana.

Alisema Dk. Slaa alidhihirisha umahiri wake wakati akiwa bungeni, hasa aliposimamia kidete suala la ufisadi, ambalo wakati wa kampeni alilinadi pia kwa wananchi na kuahidi kulitatua iwapo atapewa ridhaa ya kuingia ikulu na wananchi.

Alibainisha kuwa kama wagombea wote wangekuwa kama alivyokuwa Dk. Slaa, uchaguzi wa mwaka huu ungekuwa na ushindani mkubwa na hata rais angepatikana kwa tofauti ya kura chache kama ilivyotokea Zanzibar.

Alisema miongoni mwa sera za CHADEMA zilioonekana kuwagusa wananchi ni utoaji wa elimu bure, ambayo hata hivyo ilikuwa ikibezwa na baadhi ya wagombea na makada wa vyama Fulani, kwa madai kuwa haitekelezeki, bali ni hadaa ya Dk. Slaa na chama chake ili wapate kura.

Alisema matokeo ya uchaguzi ambayo yaliipa CHADEMA viti visivyopungua 22 na Chama cha Wananchi (CUF) viti 24 yatachangia kwa kiasi kikubwa kuleta upinzani wa hoja bungeni na kulifanya Bunge litakaloanza kesho mkoani Dodoma kuwa la uwajibikaji zaidi, tofauti na ilivyozoeleka kipindi cha nyuma.

"Profile ya wabunge hasa wa CHADEMA na NCCR Mageuzi ni nzuri, inavuta na kutia moyo, tunatarajia Bunge lenye mvuto na ushindani mkali wa hoja ," alisema Dk. Bana.

Katika hatua nyingine, Dk. Bana alielezea kukerwa na tabia ya baadhi ya watendaji wa serikali kutumia magari ya umma kuendesha kampeni za aliyekuwa mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete.

"Vyombo vya serikali kutumika katika kampeni si jambo zuri katika uwanja wa siasa, hili linawanyima fursa wagombea wa vyama vingine kushiriki kwenye uwanja ulio sawa," alisema Dk. Bana.

Alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu mwamko mdogo wa wananchi kujitokeza kupiga kura, alisema jambo hilo linatakiwa kufanyiwa utafiti wa kina ili kubaini chanzo cha watu kutojitokeza kupiga kura, licha ya kuwapo idadi kubwa ya waliojiandikisha.

Alibainisha kuwa pamoja na wagombea kuzunguka maeneo mbalimbali ya hapa nchini kwa kutumia usafiri tofauti ukiwamo wa magari, helikopta, ndege, pikipiki na vifaa vinginevyo ili mradi kuwafikia wananchi, bado wahusika wameshindwa kujitokeza kwa wingi wakati wa zoezi la upigaji kura.

Dk. Bana pia alitumia fursa hiyo kuzungumzia suala la uharibikaji wa kura za urais, ambapo alisema kuwa uchaguzi wa mwaka huu tatizo hilo limepungua kwa kiasi kikubwa tofauti na chaguzi zilizopita.

"Kura zilizoharibika kwa mwaka huu ni 227,889 ambazo ni sawa na asilimia 2.64, tofauti na mwaka 2005, ambapo asilimia ya kura zilizoharibika ilikuwa 4.9, nawapongeza wahusika kwa hatua hii," alisema Dk. Bana.

Alibainisha kuwa kuna haja ya elimu ya uraia na ya uchaguzi kuwa endelevu ili kuwafanya wananchi kupata uelewa wa kutosha badala ya elimu hiyo kutolewa kwa mtindo wa zimamoto kila unapofika wakati wa uchaguzi.

Aliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kurekebisha kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika uchaguzi huu, pia kuwataka wananchi kutosubiri kusukumwa hasa katika kufanya jambo lenye maendeleo.

Tanzania hakuna Tume huru. Inatakiwa kuvunjwa na kuundwa upya. Kasoro zilizojitokeza zilikuwa za kutengenezwa (za makusudi). Kama ingekuwa ni bahati mbaya, wangerekebisha!
 
SINA CHA KUCHANGIA SABABU HUYO DR BANA NAONA HATA KINYAA KUMSIKIA. PUMBAVU KABISA HUYO.:rip:
 
Apeleke huko nani anataka tafiti zake,, baada ya kuona kuwa nchi inapelekwa pabaya na baada ya kupewa hela ndiyo anaponda mbona asingefanya hivyo siku za nyuma????
 
Anazungumza mambo ya msingi lakin ts too late sasa maana wamefanya tafiti za kifisadi tayar na zikatumika kussuport uchakachuaji wa kura.. kwani ripot yao si ilisema 61% na nani hajui kwamba na matokeo yamekuja kwa 61%!!

Dr Bana amepoteza credibility kwa wananchii!!
 
huyu nae anajiita Dokta wa sociology. Kweli Tz shamba la bibi. Huyu jamaa I am sure atakufa kwa pressure siku sii nyingi. He is packed with everykind of frustrations.
 
Nilitegemea azungumzie ni kwa nini matokeo halisi ya Uraisi yalitofautiana na yale makadirio yao.............na kwa nini afikiri yale ya SYNOVATE yalishahibiana kwa ya JK katika Uraisi lakini yalimwonea Dr. Slaa......................au kwa nini wote Redet na Synovate hawakumtendea haki Dr. Slaa na kushusha hivyo....................ukiachilia mbali mchezo mchafu ambao tunaamini NEC walicheza katika kumsimika JK Uraisi isivyo halali na kinyume cha sheria..........
 
Hebu punguzeni kidogo! Mtu hata akitoa comments basi ataambiwa anajipendekeza, sasa munataka watu wanyamaze?
 
Dr banna ni mnafiki wa kutupwa anakimbia kivuli chake mnafiki mkubwa mchakachuaji hatumtaki aende kulamba kikwete
 
Hebu punguzeni kidogo! Mtu hata akitoa comments basi ataambiwa anajipendekeza, sasa munataka watu wanyamaze?

huyu ni mnafiki mkubwa,hartupunguzi kitu ni kumpa vidonge vyake tu,kwa nini hakusema hivyo kabla hajapewa hela ya kuandaa utafiti feki?
hana maana kwani ndio wasomi tulio nao miaka hii.
pumbafu zao
 
Hebu punguzeni kidogo! Mtu hata akitoa comments basi ataambiwa anajipendekeza, sasa munataka watu wanyamaze?

hao ni wafa maji kila mtu hata akitoka comment wanajifanya kuponda. Tunajua wanachadema wamechanganyikiwa muda si mrefu wataanza kuokota makopo barabarani. Afterall Dr. Bana hana cha kupoteza kwa slaa. So their comment are non sense. Trust me.
 
Wewe bana ungekuwa karibu na mimi ningekupiga kofi!!!!!!Wewe mnafiki CDM hatuhitaji support yako maana imejaa unafiki na kujipendekeza!!!!!!!!!!!
 
Sasa ndio anajitia kuwa nyutro..bwe he he..

BTW<> mbona hajagusia suala la kumboresha tume ya uchaguzi, ili iwe huru na ya haki zaidi?
 
WANANCHI TUJIHADHARI NA WASOMI MATAWI YA UFISADI WANAOTUCHUUZA KILA KUKICHA:

Umma wa Tanzania, ITAFAKARINI KWA MAKINI TAARIFA HII:

Kae mkijua ya kwamba mbali na wasomi wachache kama vile Prof Baregu, Chachage (Senior / Marehemu), Haroub Othman (marehemu) Drs Mvungi, Rwaitama, Slaa, Lissu, Marando, Sitta, Mama Malechela, Dr Mwakyembe, Tairo (Tumaini University), Prof Maina, Mama Nkya, Regnald Mengi, Kubenea, Tido Mhando, Mgaya wa TUCTA, Mch Mtikila, Zitto Kabwe, Mnyika, Kitila Mkumbo na wengine wachahe ambao sijawataja ambao wamekua WAKIDHUBUTU kuharisha maisha yao na kujinyima anasa za dunia huku wakitumia uwezo wa AKILI walizojaliwa nazo KUWATETENI Maslahi ya Wote, Wasomi wetu wengine waliowengi HAWANA TOFAUTI WAFANYABIASHARA MNADANI ambapo kila mmoja wao anagombania nafasi ya KUMTUMIKIA FISADI kwa dau la juu zaidi kuliko wengine.

Kwa Ujuzi zaidi wanawasaidia zaidi MAFISADI namna ya kutengeneza MIKATABA ya kutuibia rasilmali zetu kwa faida ya wachache. Wasomi haya waliofaidi kodi zetu wamegeuza akili zao kuwa ni TAWI na MILIKI rasmi ya MAFISADI. Ukitaka kuamini haya ninayoyasema, basi subiri uje ukawasome vizuri zaidi wasivyoeleweka pindi tunapoanza mchakato wa kuandika upya KATIBA tunayoitaka.

Kila kukicha wanabanana mlangoni kwa MAFISADI, tena hata wale wa darasa la saba tu wakienda wachotea familia na mahara zao mifedha tulizoporwa huku wakichukulia sisi sote ni mazezeta mbele yao.

Hapa tulipofika tunasema BASI - HAKI na FEDHA za KIFISADI zitenganishwe, Katiba mpya na Tume Huru ya uchaguzi ni sasa hivi hata kwa uwezo wa elimu zetu za ngumbaru tu endapo WASOMI wa nchi hii wataendelea kugomea kuchukua nafasi zao sahihi kuongoza MABADILIKO YA KWELI wakiwa katika MSTARA wa mbele.

Kwani, kama dawa ya SUBILI, MABADILIKO YA KWELI hayaonjwi yananywewa mara moja!! Mawazo mazuri tu hayasaidi kama hatuna mwenye utayari wa kuyatumikia mpaka matunda yaonekane na wakati mwingine hata kuyatetea hadi kufa!!! Vijana Tanzania sisi tumeshaamua, na wala haturudi nyuma sisi vijana mpaka kieleweke!!!!!!!!!!! Machungu ya umasikini wa kupindukia siku zote bila ajira, kwa kutwishwa na MAFISADI na baadhi ya WASOMI WALAFI, yanang'ata kuliko rungu la polisi la siku mbili.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom