saed kubenea
Member
- Dec 13, 2010
- 11
- 4
Wale vijana wanywa damu sasa wanajiandaa kumywa Martin Shigella kada yule aliyekuwa mkuu wa wilaya wilaya ya Mama Salma na akaletwa UVCCM kulinda maslahi ya kundi hilo. Hatua hii inakuja leo baada ya kummwaga Masauni wakisaidia na Bwana mkulu JK kwa kutumia taarifa feki kuwa alikuwa akisaliti kufanikisha kushinda safari ya pili kwa JK. Kipindi hiki inaelezwa jambo linalowaumiza ni mslahi huku Shigella akituhumiwa kubeba mabintikibao katika misafara yake ya kampeni ambao katika matukio tofauti walikunjana mashati baada ya kugundua kuwa wote wanavunjwa amri ya kumi na Shigella. Tuhuma hizi zinazoandaliwa na Ridhwan na Beno zinapangwa kwa umakini mkubwa ikiwa ni mkakati wa kumpachika binti mmoja jina nalitunza kwanza katika nafasi ya ukatibu wa UVCCM kwa kigezo kuwa nafasi hiyo inahitaji jenda ya kike. Taarifa hizi za ndani kutoka kwa watendaji wa UVCCM ambao wapo makao makuu na ambao nao walikuwa wakifanya ziara mikoani huku wakifanya haya haya wanayomtuhumu Shigella zinakuja wakati bwana mkubwa hajapewa majibu ya kwa nini asilimia zake zilipungua kwa kiwango hicho wakati yeye alifahamu angeopandisha kura kwa kuwa eti tafiti zilikuwa zikimuonyesha kuwa ni maarufu.
Nitazidi kuwapatia nyuzi kadri chanzo changu kilichoko karibu na Ridhwan kitakavyokuwa kikinipatia!!!
Nitazidi kuwapatia nyuzi kadri chanzo changu kilichoko karibu na Ridhwan kitakavyokuwa kikinipatia!!!