Ringo Edmund
JF-Expert Member
- May 10, 2010
- 4,879
- 1,125
kweli mnada wa maili mbili ulirudi kwa style ya aina yake.
Kama Baba lao liliingia Ikulu kwa EPA na Kagoda, nani atamnyoshea mwenzie kidole?
Pamoja na Makonda kuadhibiwa kutokana na kuungwa mkono na watu flani ila vile vile ilionekana kuwa kauli ya Raisi wakati akitoa hotuba yake kwamba "vijana wasichague watu wenye ndimi 2" ilimlenga Makonda na ilimgharimu vile vile kwani amekuwa akisikika na kuonekana akitoa kauli tata mara nyingi dhidi ya Chama chake.
Niwapongeze walioshinda hasa huyu dada Mboni Mhita kwa kuwa kama vita hii ya kwake ilikuwa kama ile ya Iraq...... Hongereni sana mkajipange sasa kuendelea kuijenga Jumuiya kama ambavyo wenzenu walijitahidi na kuifikisha hapo ilipo! Msije mkawa vichaa kwa kuchukua mabaya na kuacha mema.......... Kubwa achaneni na makundi