Elections 2010 Benno Malisa azomewa Geita kwa kuhusisha maisha binafsi ya Dr Slaa

Reyes

Senior Member
Sep 1, 2010
188
2
ZOMEA zomea kwenye mikutano ya kampeni ya CCM jana ilimgeukia mpigadebe aliyejaribu kuingiza masuala ya maisha binafsi ili kumponda mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa baada ya wananchi kumzomea mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama tawala, Benno Malisa.

Zomeazomea hiyo imeshawakumba wagombea ubunge wa majimbo tofauti ambao waliteuliwa kugombea nafasi hiyo kwa tiketi ya CCM baada ya washindi kwenye kura za maoni kuchakachuliwa.

Jana ilikuwa zamu ya Malisa kwenye mkutano wa kampeni wilayani Geita ambako alikuja kumnadi mgombea ubunge wa Geita Mjini, Donald Max. Malisa, ambaye ni mmoja wa vijana walioteuliwa kuzunguka nchi nzima kufanya kampeni za CCM, alitaka kuwapa wananchi hao maana ya neno "fisadi".

“Huyu (Dk Slaa) anapita na kuomba achaguliwe, ameshindwa kwenye uparoko sasa ataweza kuongoza nchi," alihoji Malisa. "Kule Kenya ukielezea neno fisadi maana yake ni mtu anayetembea na wake za watu, sasa Slaa amechukua mke wa mtu yeye si ndiye fisadi namba moja?” Lakini wananchi walianza kuguna na baadaye kuzomea huku wakinyoosha mikono juu kuonyesha vidole viwili, ambayo ni alama ya Chadema.
Kutokana na kelele hizo, Malisa aligeuza uelekeo wake wa mazungumzo na akaamua kumuita mgombea wa udiwani wa Kata ya Kalangalala, Daudi Ntinonu na kumnadi.


Mgombea udiwani huyo aliposimama, alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya wananchi kueleza kuwa wamchague mgombea huyo na wengine wa CCM kwa vile tatizo la maji kwenye mji wa Geita limetatuliwa.
Kauli hiyo iliamsha kelele tena na ndipo ilipomlazimu kurekebisha na kueleza kuwa fedha zimepatikana umebaki utekelezaji wa kufikisha maji kwenye mji huo.

Baadaye ndipo Malisa, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo wa kampeni, alipomsimamisha Max kujinadi kuhusu atakachowafanyia wananchi hao iwapo atachaguliwa kuwa mbunge wao.
Max aliwataka wananchi wamchague mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete kwa madai kuwa amekubali serikali kutoa Sh6 bilioni kwa ajili ya kukamilishia mradi wa maji.

Max, ambaye alidai kuwa amekuwa akiitwa Bubu katika kampeni za upinzani, aliwataka wananchi kuchagua wagombea wa CCM na kwa kuwa wana imani naye, atasimamia mradi huo wa maji hadi ukamilike na kusisitiza kuwa walimtaka awe mbunge sasa ameshakuwa.
Alisema sasa hakuna madiwani ambao watampiga chenga na kukwamisha maendeleo kwa vile wote watakuwa wa CCM.

Kigogo wa CCM azomewa mkutanoni
 
Back
Top Bottom