Benki ya walimu, ya vijana, ya wanawake ya jeshi la JWTZ ...and what else?

The Boss

JF-Expert Member
Aug 18, 2009
49,063
115,461
hivi hii ya serikali kuanzisha benki ya vijana,
ya wanawake....,na ya jeshi ....
na sijui ni nani huyu anaeanzisha ya walimu.....

hivi.....hiii yote ni nini hasa???????

na hiyo benki ya walimu itaathiri vipi nmb??????

watanzania wanaotumia benki hawafiki millioni mbili....

kuna mtaalamu humu anaweza kutufafanulia kuna faida kwa yote haya?
 
Bado hazitoshi mkuu wacha ziwe nyingi..kuna village bank vilevile...

Watakuja ku-merge mbele ya safari..hazitoshi mkuu wacha zije as many as possible..
 
Bado hazitoshi mkuu wacha ziwe nyingi..kuna village bank vilevile...

Watakuja ku-merge mbele ya safari..hazitoshi mkuu wacha zije as many as possible..

hakuna hatari yeyote huko mbele ya safari?

je is it fair kwa commercial bank????
 
hakuna hatari yeyote huko mbele ya safari?

je is it fair kwa commercial bank????
Sioni hatari yeyote mkuu

Hatuhitaji kuwa fair to commercial bank..ila kwa clients

Ninachoona ziwepo nyingi ili watupe products nyingi zenye unafuu kwetu...

Besides, labda watafika village level wakiwa wengi..
 
angalia TBC RAIS WA WALIM MKOBA ANANADI BANKI YA WALIM SASAHIVI,HII NCHI IMEKWISHA KILA TASISI WANAANJISHA BIASHARA,TUNASUBIRI BANKI YA WANAFUNZI TANZANIA
 
hivi hii ya serikali kuanzisha benki ya vijana,
ya wanawake....,na ya jeshi ....
na sijui ni nani huyu anaeanzisha ya walimu.....

hivi.....hiii yote ni nini hasa???????

na hiyo benki ya walimu itaathiri vipi nmb??????

watanzania wanaotumia benki hawafiki millioni mbili....

kuna mtaalamu humu anaweza kutufafanulia kuna faida kwa yote haya?

zitakuja bank za mikoa na za ukabila sasa
 
Katika sababu zilizofanya mtikisiko wa uchumi Duniani mojawapo ni the mushrooming of financial institutions like banks,long term loans na watu kushindwa kulipa mikopo yao ila watu wanaweza wakafurai sana kwa mfumo ule tuliozoe wa to ignore history.
 
Mgonjwa anapokaribia kufariki huwa anaomba omba na kusema mambo mengi bila mpangilio. Huo ni mkakati wa magamba wanadhani ni mtaji wa kupatia kura za hayo makundi ktk chaguzi zijazo huko mbeleni.
 
hii banki ya walimu ita colapse very soon.....

Mkuu hii bank huenda ikaiathiri NMB. Kumbuka walimu karibu wote kama si wote ni wateja wa NMB na waalimu ni wengi wapo kama 240,000 hivi. Kwa hiyo ikianzishwa bank hii na kufungua matawi sehemu nyingi itakuwa na hazina ya wateja kama 240,000 hivi!! Kwa hiyo principle ya cannibalism itaimaliza NMB. Acha zianzishwe nyingi ili supply ya fiancial services iwe juu na hii inaweza kupunguza interest rates ambazo mibenk ya leo inawatoza wateja na rates ndogo ambazo zinalipwa. Najua benki nyingi si suluhisho pekee la interest rates lakini huenda ikawa changamoto kwa mabenki mengine.
 
Hivi hamna mpango wa kuanzisha bank ya CCM?

JK hana mpango wa kuanzisha bank ya watu wa Bagamoyo ama Chalinze?
 
Mkuu hii bank huenda ikaiathiri NMB. Kumbuka walimu karibu wote kama si wote ni wateja wa NMB na waalimu ni wengi wapo kama 240,000 hivi. Kwa hiyo ikianzishwa bank hii na kufungua matawi sehemu nyingi itakuwa na hazina ya wateja kama 240,000 hivi!! Kwa hiyo principle ya cannibalism itaimaliza NMB. Acha zianzishwe nyingi ili supply ya fiancial services iwe juu na hii inaweza kupunguza interest rates ambazo mibenk ya leo inawatoza wateja na rates ndogo ambazo zinalipwa. Najua benki nyingi si suluhisho pekee la interest rates lakini huenda ikawa changamoto kwa mabenki mengine.

Kwa maelezo ya wale wazee wa jana TBC inaonekana jamaa wana kama bil 2 au 3 zilizotokana na kodi ya jengo lao la Mwalimu House na wanazungumzia kuhusu walimu kuchukua hisa ili benki hiyo iweze kuwa na mtaji tosha kujianzisha. BOT wana regulations za bil 15 capital kwa banks, sasa kama ni hivyo hii hela nyingine itatoka wapi? Au kuna mdhamini kapatikana, na soon baada ya kuanza utasikia imeshindwa kujiendesha na hivyo kuuziwa mtu kuiendesha.
 
Kwa maelezo ya wale wazee wa jana TBC inaonekana jamaa wana kama bil 2 au 3 zilizotokana na kodi ya jengo lao la Mwalimu House na wanazungumzia kuhusu walimu kuchukua hisa ili benki hiyo iweze kuwa na mtaji tosha kujianzisha. BOT wana regulations za bil 15 capital kwa banks, sasa kama ni hivyo hii hela nyingine itatoka wapi? Au kuna mdhamini kapatikana, na soon baada ya kuanza utasikia imeshindwa kujiendesha na hivyo kuuziwa mtu kuiendesha.

Mkuu wewe mwenyewe umesema kwamba wana kiasi cha kama 3 billioni na wanataka waalimu wachukue share. Kwa maana hiyo nadhani difference ya 12 billion ili kufikisha 15 billion itatokana na share ambazo waalimu watanunua.
 
Mkuu wewe mwenyewe umesema kwamba wana kiasi cha kama 3 billioni na wanataka waalimu wachukue share. Kwa maana hiyo nadhani difference ya 12 billion ili kufikisha 15 billion itatokana na share ambazo waalimu watanunua.

Mkuu hiyo ni sawa lakini nilikuwa najaribu kuangalia kama kweli bil 12 inaweza kutoka kwenye mifuko ya walimu wenye kipato hiki cha chini, wanaoishi kwa mikopo. Labda ipatikane bil 1 au 2, sasa hili gepu ndio hilo litahitaji kufadhiliwa.
 
Benki zinakuja nyingi sana,
Kuna Benki ya wanafunzi,
Ya watoto,
Ya polisi,
Ya walemavu,
Ya madaktari,
Ya madereva,
Ya wenyenyumba,
Ya wapangaji,
Listi ni ndefu sana kweli:
Benki ya wapigadebe,
Ya wabunge,
Ya majambazi,
Ya wapiga kura,
Ya wauza genge,
Benki ya mama ntilie,
Ya ya wavuvi,
Ya wacheza kamari,
Ya vibaka,
Ya waigizaji movie,
Ya waimba kwaya,
Benki ya member wa Jf,
Ya wauza sura,
Ya wapita njia,
Ya fundi ujenzi,
Ya walinzi,
Ya matapeli,
Ya mafundi mafriji,
Zote hizi benki zinakuja soon!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom