Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Benki ya Posta (TPB) inayomilikiwa na serikali na iliyopo nchini ya uongozi wa wazalendo, imeripoti kupata mabilioni ya faida (3.8bn/-, ongezeko la asilimia 338). Benki hiyo ilikuwa ndogo sana wakati Mkapa ameshika bango la kubinafsisha NBC hadi kuwatukana wabunge waliokuwa wakipinga suala hilo. TPB imekua taratibu chini ya uongozi wa kizalendo hadi kuwa na rekodi iliyopo.
NBC ilikuwa moja wapo ya taasisi za serikali zenye ufanisi sana na kuweza kufikisha huduma karibu sana kwa wananchi, katika maeneo fulani hadi ngazi ya kata. Matawi mengi ya NBC yaliyokuwa karibu na wananchi yalifungwa baada ya NBC kubinafsishwa.NBC ilitoa riba kubwa kwa wateja iliyokuwa juu ya kiwango cha inflation, na haikuwa ikitoza "bank fees". Hili lilionekana kikwazo kikubwa kwa kampuni zilizotaka kuwekeza benki nchini, ambazo zinatoza ada (bank fees) kila uchukuapo fedha na pia kutoa riba ndogo sana iliyo chini ya kiwango cha inflation. Wawekezaji walikataa kuanzisha bank nchini katika mazingira haya ya kuwapo kwa NBC kwa kuwa wasingepata wateja, na wakamshawishi Mkapa aibinafsishe NBC kwanza.
Wabunge na Nyerere walipinga sana kitendo cha kubinafsisha NBC. Inasemekana kiongozi wa ngazi ya juu nchini alipewa zawadi ya hoteli huko Afrika Kusini baada ya kufanikisha ubinafsishaji wa NBC.
Original source (with edits): IPP Media
NBC ilikuwa moja wapo ya taasisi za serikali zenye ufanisi sana na kuweza kufikisha huduma karibu sana kwa wananchi, katika maeneo fulani hadi ngazi ya kata. Matawi mengi ya NBC yaliyokuwa karibu na wananchi yalifungwa baada ya NBC kubinafsishwa.NBC ilitoa riba kubwa kwa wateja iliyokuwa juu ya kiwango cha inflation, na haikuwa ikitoza "bank fees". Hili lilionekana kikwazo kikubwa kwa kampuni zilizotaka kuwekeza benki nchini, ambazo zinatoza ada (bank fees) kila uchukuapo fedha na pia kutoa riba ndogo sana iliyo chini ya kiwango cha inflation. Wawekezaji walikataa kuanzisha bank nchini katika mazingira haya ya kuwapo kwa NBC kwa kuwa wasingepata wateja, na wakamshawishi Mkapa aibinafsishe NBC kwanza.
Wabunge na Nyerere walipinga sana kitendo cha kubinafsisha NBC. Inasemekana kiongozi wa ngazi ya juu nchini alipewa zawadi ya hoteli huko Afrika Kusini baada ya kufanikisha ubinafsishaji wa NBC.
Original source (with edits): IPP Media