Benki ya NMB yaja na huduma ya mkopo ya "NMB Salary Advance" kwa wafanyakazi

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Kwanza kabisa napenda kuwapongeza sana NMB kwa kuleta huduma hii ambapo mfanyakazi anakuwa na uwezo wa kukopa mpaka asilimia 40 ya mshahara wake(take home bila shaka)

Huduma hii ya mkopo ambayo mfanyakazi atalipa mkopo huo kwa kukatwa mshahara wake mara utakapoingia Benki, utawasadia sana wafanyakazi wanaopata dharura na kulazimika kukopa mitaani kwa riba kubwa.

NMB wao wanasema hawatozi riba bali unatozwa asilimia 6 tu ya kiwango cha mkopo unaochukua kama gharama ya ku-process mkopo husika.

UKweli ni kwamba hata kama hiyo 6% ingekuwa ndio riba bado ni ndogo sana ukilinganisha na riba wanazotozwa wafanyakazi huku mitaani ambapo mtu akikopa kwa mfano shilingi 100,000 anatakiwa kurudisha shilingi 120,000 na wengine mpaka 130,000 mwisho wa mwezi akipata mshahara.

Huduma hii itaokoa wafanyakazi wengi ambao wengi huishi kwa kukopa kwani mishahara ni midogo na matatizo ni mengi huku siku 30 za kusubiri mshahara utoke zikiwa ni nyingi mno.

Huduma hii ambayo imeanza kutolewa kuanzia tarehe 13/03/2018 kwa mujibu wa kipeperushi chao, inapatikana kwa kupiga *150*66# then unachagua "mkopo" ambayo ni option number 5.

Mkopo unaingizwa kwenye akaunti yako ya mshahara wa NMB moja kwa moja.

Kwa maelezo zaidi ikiwa ni pamoja na kujua mashariti na vigezo ingia:
www.nmbbank.co.tz.

Huduma hii nasikia hata CRDB nao wanayo.

Ushauri:
Kama NMb wameweza ni wazi hata serikali nayo inaweza kuangalia kuanza utaratibu wa kulipa watumishi nusu mshahara kila ifikapo nusu ya mwezi ili kupunguzia watumishI wake ugumu wa maisha maana sasa hivi hata ukijiongeza ukafanya biashara ili uongezi kipato biashara nazo zimekuwa ni ngumu hivyo unajiongeza lakini bado inakuwa haisadi sana.

Vile vile nawashauri NMB malezo kuhusu mashariti na vigezo vya kupata mkopo yatolewe kwa lugha ya kiswahilI pia ili watu waweze kuelewa vizuri na kwa urahisi zaidi terms za mkopo huu kwani kujua mashariti na vigezo kabla ya kuchukua mkopo ni jambo la muhimu sana.
 
Sio huduma mpya CRDB ndio ameianzisha muda mrefu hao wameiga tu.Naona Baada ya walimu kukopa kwenye Benk yao sasa wanahangaika
 
Moderator hamisheni huu uzi jukwaa hili ni la siasa sio biashara
 
Copy and Paste kutoka CRDB na CRDB tunalipa 5%. Hivi wenzangu huwa mnapokea shillings ngapi mpaka mnaishiwa kiasi hicho?
 
Advance salary ni kumdanganya mfanyakazi; ukali wa maisha ni uleule.
Nani anakudanya mbona iko wazi bank wanataka kukulamba 6% ya mshahara wako ni 950,000 watakulamba kama 57,500 hivi So Mwisho wa mwezi utakua una deduction ya 6% katika salary njia nzuri ya kutatua matatizo yako ni kua na utamaduni wa Ku save mwenyewe na siyo kukopa
 
Nani anakudanya mbona iko wazi bank wanataka kukulamba 6% ya mshahara wako ni 950,000 watakulamba kama 57,500 hivi So Mwisho wa mwezi utakua una deduction ya 6% katika salary njia nzuri ya kutatua matatizo yako ni kua na utamaduni wa Ku save mwenyewe na siyo kukopa
Husiongelee jambo husilolijua ndugu. 6% kwa mkopo wowote ni riba ndogo sana. Mtaani ukikopa shs laki moja, mwisho wa mwezi unalipa shs 120,000. Hii ni zaidi ya 18% riba. Kwa NMB kama wanatoza 6% kwa mkopo wa shs 100,000 mwisho wa mwezi utalipa shs 106,000 ambayo ni nafuu sana kwa wafanyakazi wetu hasa kada ya walimu.
 
6% TU kwa mwezi? What a deal!
Ina maana ni equivalent ya 72% kwa mwaka. Hii si kusaidia wafanyakazi bali ni kuwaongezea umasikini. Kwa akili zako timamu utawezaje ku survive na 60% ya net salary yako after all the deductions? Nilitegemea wangesema hiyo pay slip loan italipwa ndani ya miezi mitatu tungeweza kuwafahamu. Lakini those types of loans zinatakiwa ziwe discouraged rather than encouraged na financial institutions zetu kwa sababu hazitowi picha nzuri na ni ishara ya kudidimia kwa uchumi. Kama uchumi unakuwa basi tungeona banks wanashindana katika kuja na njia mpya ya kuwa encourage watu wafanye savings na sio kukopa.

The way I see it, we are moving dowhill at supersonic speed and soon no one will not even see the numbers let alone read them!
 
Back
Top Bottom