Benki ya NMB wamenifanya ombaomba baada ya kuibiwa pesa zangu nilizolimbikiza kwa miaka kadhaa

Status
Not open for further replies.

stujadiliane

Member
Jun 2, 2017
66
84
Ndugu wanaJF, Mimi ni mtanzania mzalendo na wa kipato cha chini ambaye Benki yangu ya NMB Tanzania imenifanya sasa ni wewe omba omba baada ya kuibiwa pesa zangu zote ambazo nimezilimbikiza kwa miaka kadhaa.

Nakumbuka niliamua kuweka pesa zangu benki ili ziwe salama. Nimezungushwa vya kutosha katika kujaribu kutafuta haki yangu lakini bado nimekuwa nikiwasiliana na meneja tawi la NMB Tanzania Kinyatta road bila kupata mafanikio kwa miaka kadhaa.Nimejaribu kuomba msaada NMB Tanzania makao makuu mpaka sasa sijapata msaada.

Naomba Msaada ili nirejeshewe pesa zangu kwani pesa zangu zilikuwa zikihamishwa kutoka kwenye account yangu na kuingizwa kwenye account nyingine bila idhini yangu.

Hivi punde nitaweka vielelezo vyote vya barua ya Polisi,barua ya meneja NMB Tanzania Tawi la Kinyatta jijini Mwanza na barua ya meneja makao makuu.

Nataka muone benki ya wazalendo NMB Tanzania ilivyoyafanya maisha yangu kuingia shimoni.

----------Update------------
Asante wadau, nitaweka vielelezo vyote ninavyo kwani kesi hiyo ilifika polisi.Vielelezo vyote vinavyoonesha pesa zilivyohamishwa ninavyo na account zilipokuwa zinahamishiwa ninazo pia.

Katika barua ambazo nilizituma nilipomwandikia Mkurugenzi Mkuu wa NMB Tanzania niliambatanisha na vielelezo vyote.

Niliweka
1. Barua ya kufungulia kesi
2. Niliweka bank statement inayoonyesha pesa zangu zilivyo kuwa zikihamishwa kwenda kwenye account mbili tofauti.

Nilisambaza nakala hizo kwa...
a) BoT Mwanza
b) BoT Taifa
c) Mwanasheria mkuu
d) Mwanasheria wa mkoa wa Mwanza
e) Waziri Mkuu
f) Waziri wa Katiba na Sheria
g) Mkuu wa Mkoa Mwanza
h) Meneja wa tawi la Kinyatta NMB Tanzania,
i) RCO mkoa wa Mwanza.

Kati ya hao ni Mwanasheria wa Mkoa angalau alionesha kujali kwa kuniita ofisini kwake.

Aidha nakiri kupokea barua kutoka makao makuu NMB Tanzania, lakini haikuonesha msaada zaidi ya kusema tuwasiliane.

Miaka kadhaa imepita sasa naendelea kuzunguka meneja wa Tawi NMB Tanzania Kinyatta Mwanza ameishanipa maelekezo ikiwemo kunitaka niandike barua ya kuomba nilipwe lakini hata baada ya kuandika ni miaka sasa hakuna majibu.

Naomba msaada kwa Waziri wa Fedha anisaidie kwani wale ambao pesa zangu zilihamishiwa kwenye account zao wapo na tulishakutana Polisi na wakadai account zao hazitumiki.

Sielewi na sielewi naomba msaada wa haraka.
 
Ndugu wanajamii form Mimi ni mtanzania mzalendo na wakipato cha chini ambaye Bank yangu ya NMB imenifanya sasa ni wewe omba omba baada ya kuibiwa pesa zangu zote ambazo nimezilimbikiza kwa miaka kadhaa. Nakumbuka niliamua kuweka pesa zangu bank ili ziwe salama. Ni mezungushwa vya kutosha katika kujaribu kutafuta haki yangu lakini bado .ni mekuwa nikiwasiliana na meneja tawi la NMB kinyatta road bila kupata mafanikio kwa miaka kadhaa .Ni mejaribu kuomba musaada NMB makao makuu mpaka sasa sijapata Musaada.

Naomba Musaada ili nirejeshewe pesa zangu.kwani pesa zangu zilikuwa zikihamishwa kutoka kwenye Account yangu na kuingizwa kwenye Account nyingine bila idhini yangu.Hivi punde nitaweka vielelezo vyote barua ya police.barua ya MENEJA NMB Tawi la Kinyatta jijini Mwanza na barua ya MENEJA makao makuu. Nataka Muone NMB bank ya wazalendo ilivyo ya Fanya maisha yangu kuingia shimoni
Sioni sababu ya wewe kuogopa kuweka hizo vielekezo kama ni ukweli,ili upate ushauri lazima uweke hizo vielelezo,sheria za benki ni ngumu sana,hata benki ikifilisika leo hata kama una millioni 100 kwenye akaunt yako utalipwa 250,000 pekee ndiyo yenye bima ingine imekula kwako.
 
Unaweza kutoa maelezo kuhusu mazingira ya kuibiwa kwako ili tufahamu imetokana na na uzembe wa bank au ni mwenyewe ndie umesababisha!!

Umejuaje pesa zilikuwa zinahamishwa kutoka kwenye akaunti yako na kwenda kwenye account nyingine?! Ni kwamba kuna hizo details kwenye statement; au?!
 
Ulifungua aina gani ya Account...?? Na hiyo account uloifungua masharti yake yalikuwaje..??
 
Kingozi NMB wana uzi wao malum jaribu kuwa pm jambo jingine watumie e mail wapo active sana watashirikiana tu na wewe bila tatizo
 
Pole sana mkuu ila pesa haiwez kupotea bure fungua kesi wakulipe na inawezekana wamezihamisha wakubwa ndo maan hawatilii maanani....
 
Ndugu wanajamii form Mimi ni mtanzania mzalendo na wakipato cha chini ambaye Bank yangu ya NMB imenifanya sasa ni wewe omba omba baada ya kuibiwa pesa zangu zote ambazo nimezilimbikiza kwa miaka kadhaa. Nakumbuka niliamua kuweka pesa zangu bank ili ziwe salama. Ni mezungushwa vya kutosha katika kujaribu kutafuta haki yangu lakini bado .ni mekuwa nikiwasiliana na meneja tawi la NMB kinyatta road bila kupata mafanikio kwa miaka kadhaa .Ni mejaribu kuomba musaada NMB makao makuu mpaka sasa sijapata Musaada.

Naomba Musaada ili nirejeshewe pesa zangu.kwani pesa zangu zilikuwa zikihamishwa kutoka kwenye Account yangu na kuingizwa kwenye Account nyingine bila idhini yangu.Hivi punde nitaweka vielelezo vyote barua ya police.barua ya MENEJA NMB Tawi la Kinyatta jijini Mwanza na barua ya MENEJA makao makuu. Nataka Muone NMB bank ya wazalendo ilivyo ya Fanya maisha yangu kuingia shimoni
Ungedokeza angalau kidogo ilikuwaje. Ushahidi mwingine baki nao na ndo utakufanya ushinde kesi. Mimi nilishalipwa pesa na jamaa,zikaingia NBC kwa akaunti ileile yangu ya NMB! Baada ya miezi kadhaa na kufuatilia sana,nikazipata. Hivyo,usikate tamaa.
 
Nadhani kabla ya kuegemea upande wowote ungeweka bayana mazingira ya kilichotokea..
 
Ndugu wanajamii form Mimi ni mtanzania mzalendo na wakipato cha chini ambaye Bank yangu ya NMB imenifanya sasa ni wewe omba omba baada ya kuibiwa pesa zangu zote ambazo nimezilimbikiza kwa miaka kadhaa. Nakumbuka niliamua kuweka pesa zangu bank ili ziwe salama. Ni mezungushwa vya kutosha katika kujaribu kutafuta haki yangu lakini bado .ni mekuwa nikiwasiliana na meneja tawi la NMB kinyatta road bila kupata mafanikio kwa miaka kadhaa .Ni mejaribu kuomba musaada NMB makao makuu mpaka sasa sijapata Musaada.

Naomba Musaada ili nirejeshewe pesa zangu.kwani pesa zangu zilikuwa zikihamishwa kutoka kwenye Account yangu na kuingizwa kwenye Account nyingine bila idhini yangu.Hivi punde nitaweka vielelezo vyote barua ya police.barua ya MENEJA NMB Tawi la Kinyatta jijini Mwanza na barua ya MENEJA makao makuu. Nataka Muone NMB bank ya wazalendo ilivyo ya Fanya maisha yangu kuingia shimoni
Kama akaunti hiyo ni halali ni yako na umeitumia kuwekea pesa yako na taarifa za kibank zionesha umekuwa ukiweka pesa na zimeamishwa na mwigine. Nenda mahakamani na usiweke wakili hiyo kesi utashinda mapemaaaa. Na utawafungulia charge
 
cha msingi weka hizo taarifa... tujue ni kwa namna ipi uliweza kuibiwa

ukiweka hizo taarifa hp, mosi utaelimisha wengine wasiibiwe, pili na ww utapata msaada ipaswvyo... au nmb wenyewe watakutafuta maana utakuwa umeharibu jina lao..

usipoweka hizo taarifa, ww utakuwa muongo
 
Kingozi NMB wana uzi wao malum jaribu kuwa pm jambo jingine watumie e mail wapo active sana watashirikiana tu na wewe bila tatizo
Keshaongea hadi na makao makuu kwa barua hakuna majibu Je? Kwa kuwa Pm na email ndo watamsaidia..

Hakuna benki naiogopa na kutobenki nayo tena daima kama NMB..
 
hebu tafuta mawakili nenda mahakamani, kuna nafasi kubwa sana ya wewe kutajirika kupitia nafasi hiyo. kuna kituo cha msaada wa kisheria ni bure kila kitu kwa dar kipo maeneo ya morocco. nitakupa mfano kuna taasisi ya fedha iliuza nyumba ya mdaiwa mkopo chini ya thamani iliyotakiwa 150M, jamaa alienda mahakamani akashinda akapewa fidia 600M . tafuta mawakili haraka sana
 
Pesa zimehamishwa vipi toka kwenye account yako kwenda account za watu wengine bila idhini yako?

Weka details kidogo tu, usiweke vielelezo vyote ili watu waone warakusaidiaje, lakini kama hukuhusika kuhamisha hizo pesa kosa kubwa wamefanya watendaji wa NMB.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom