Benki ya Kilimo Tanzania haina faida yoyote kwa Mkulima

Mtondoli

Member
Nov 9, 2021
70
174
Wadau wenzangu wakilimo hiki kinachoitwa benki ya kilimo naona Kama hakina tija yoyote kwa mkulima halisi,najua mkulima yupo kijijini Lyazumbi, Katonto,Muze,Mtowisa,Chikumbulu huku au Ngulugulu huko Ileje ndani na vijiji vyote vinavyohusika na kilimo hawana taarifa na namna ya kunufaika na benki hii,na ninahisi kuna upigaji mkubwa kupitia benki hii.Na ninahisi wanaonufaika na benki hii sio wakulima halisi huenda kuna wajanja tu wanaojuana na familia zao ndio wanufaika.

Wajitokeze wakulima Mia tu wa vijijini walionufaika na mikopo ya benki hii ninauhakika hakuna, naona hivi ni vitu vinavyochelewesha maendeleo ya jumla ya kilimo naona waifute tu haina faida kwetu.
 
Hii benk niliiona mbeya na sikubahatika kumuona hata mkulima mmoja akiingia na kutoka. Serikali kwa sasa haipo serious kabisa na kilimo hasa katika kuwakwamua wakulima wadogo. Tupo msimu wa kulima bei ya mbolea ni laki moja na hakuna anayestuka huko serikalini tunaendelea kudemka tu.
 
hiyo sio benki ya kilimo ni benki ya wafanya biashara na vigogo huko! Walisha sema kumkopesha mkulima ni kupoteza fedha
Sio kweli. Nafahamu Mwaka 2017 TADB iliikopesha Saccos moja ipo Kilolo. Saccos iliorodhesha majina ya wakulima na mahitaji Yao ya mkopo ukafika million 29. Wakapewa. Nakumbuka riba ilikuwa milioni 1 na kidogo kwa miezi 10.
Na Kuna microfinance company hapo Madibira, imekuwa recommend kupewa mkopo kutoka TADB ili iwakopeshe wakulima.
So yes TADB ina finance miradi mikubwa lakini pia inawakopesha wakulima na hata kujenga maghala ya AMCOS kwa mkopo.
 
Back
Top Bottom