BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,792
- 287,994
Nora Damian
Mwananchi
20/2/2010
BENKI ya Dunia (WB) imeitaka serikali ihakikishe kuwa inaacha matumizi mabaya fedha za maendelelo, kwa kupunguza posho na marupurupu mbalimbali kwa watumishi wake, ili kuimarisha sekta nyingine.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati wa mkutano wa mapitio ya matumizi ya umma, Mchumi wa benki hiyo, Emmanuel Mungunasi alisema pesa nyingi zimekuwa zikielekezwa kwenye posho na marupurupu, huku sekta muhimu kama za barabara zikikosa pesa za kutosha.
Alisema kati ya mwaka wa 2008/09 serikali ilitumia Sh523 bilioni kama posho na marupurupu mbalimbali hasa katika sekta zinazohusiana na Mkakati wa Kupunguza na Kuondoa Umaskini (Mkukuta).
Alisema posho nyingi zimeelekezwa kwenye wizara mbalimbali, Bunge, Hazina na Mahakama huku pesa hizo zikitolewa kwa kushiriki kwenye mkutano au kuandaa mradi fulani.
Alisema suala la marupurupu kuongezeka kwa kasi si nzuri, kwani linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya nchi husika na hivyo wananchi wake kuzidi kuwa maskini.
"Fedha nyingi zinakwenda kwenye allowance (posho) tujaribu kujibana ili tuweze kupata maendeleo," alisema Mungunasi na kuongeza:
Nchi zenye mifumo ya fedha iliyoendelea vizuri hukua haraka kuliko zenye mifumo duni ya aina hiyo.
Mchumi huyo alisema Benki ya Dunia imekuwa ikifanya tathmini kila mwaka kuhusu mapato na matumizi ya serikali ili kuweza kujua kama fedha zao na zinazotolewa na wafadhili wengine zinatumika ipasavyo.
Hata hivyo, alisema kwa kiasi kikubwa serikali imekuwa ikijitahidi kwa kuhakikisha pesa zilizopangwa zinaenda vizuri hasa katika sekta za elimu, afya na kilimo.
Mchumi huyo aliitaka serikali kuongeza bajeti hasa katika kuimarisha miundombinu kama ya barabara, reli na bandari kwa sababu sekta ya usafirishaji inachangia kukua haraka kwa uchumi na kuongeza kasi ya maendeleo.
Benki hiyo pia imeishauri serikali kuimarisha uwezo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kubuni na kutumia sera endelevu ili kuongeza ukusanyaji wa mapato bila kukwaza shughuli za sekta binafsi.
Katika hatua nyingine, benki hiyo imesema inatarajia kutoa Sh1,000 bilioni katika bajeti ya mwaka 2010/11 zitakazoelekezwa katika sekta za barabara, elimu, afya na maji.
Kwa mujibu wa Mchumi huyo, mdororo wa uchumi uliozikumba nchi nyingi umesababisha kuongezeka kwa msaada huo kutoka Sh800 bilioni katika bajeti iliyopita hadi Sh1,000 bilioni.
Mara kwa mara nchi wahisani ambao huchangia bajeti ya nchi wamekuwa wakitoa malalamiko kuhusu matumizi mabovu ya fedha hizo na wakati mwengine hufikia hatua ya kutishia kutochangia bajeti hizo iwapo serikali itashindwa kudhibiti matumizi yake.
Mwananchi
20/2/2010
BENKI ya Dunia (WB) imeitaka serikali ihakikishe kuwa inaacha matumizi mabaya fedha za maendelelo, kwa kupunguza posho na marupurupu mbalimbali kwa watumishi wake, ili kuimarisha sekta nyingine.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati wa mkutano wa mapitio ya matumizi ya umma, Mchumi wa benki hiyo, Emmanuel Mungunasi alisema pesa nyingi zimekuwa zikielekezwa kwenye posho na marupurupu, huku sekta muhimu kama za barabara zikikosa pesa za kutosha.
Alisema kati ya mwaka wa 2008/09 serikali ilitumia Sh523 bilioni kama posho na marupurupu mbalimbali hasa katika sekta zinazohusiana na Mkakati wa Kupunguza na Kuondoa Umaskini (Mkukuta).
Alisema posho nyingi zimeelekezwa kwenye wizara mbalimbali, Bunge, Hazina na Mahakama huku pesa hizo zikitolewa kwa kushiriki kwenye mkutano au kuandaa mradi fulani.
Alisema suala la marupurupu kuongezeka kwa kasi si nzuri, kwani linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya nchi husika na hivyo wananchi wake kuzidi kuwa maskini.
"Fedha nyingi zinakwenda kwenye allowance (posho) tujaribu kujibana ili tuweze kupata maendeleo," alisema Mungunasi na kuongeza:
Nchi zenye mifumo ya fedha iliyoendelea vizuri hukua haraka kuliko zenye mifumo duni ya aina hiyo.
Mchumi huyo alisema Benki ya Dunia imekuwa ikifanya tathmini kila mwaka kuhusu mapato na matumizi ya serikali ili kuweza kujua kama fedha zao na zinazotolewa na wafadhili wengine zinatumika ipasavyo.
Hata hivyo, alisema kwa kiasi kikubwa serikali imekuwa ikijitahidi kwa kuhakikisha pesa zilizopangwa zinaenda vizuri hasa katika sekta za elimu, afya na kilimo.
Mchumi huyo aliitaka serikali kuongeza bajeti hasa katika kuimarisha miundombinu kama ya barabara, reli na bandari kwa sababu sekta ya usafirishaji inachangia kukua haraka kwa uchumi na kuongeza kasi ya maendeleo.
Benki hiyo pia imeishauri serikali kuimarisha uwezo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kubuni na kutumia sera endelevu ili kuongeza ukusanyaji wa mapato bila kukwaza shughuli za sekta binafsi.
Katika hatua nyingine, benki hiyo imesema inatarajia kutoa Sh1,000 bilioni katika bajeti ya mwaka 2010/11 zitakazoelekezwa katika sekta za barabara, elimu, afya na maji.
Kwa mujibu wa Mchumi huyo, mdororo wa uchumi uliozikumba nchi nyingi umesababisha kuongezeka kwa msaada huo kutoka Sh800 bilioni katika bajeti iliyopita hadi Sh1,000 bilioni.
Mara kwa mara nchi wahisani ambao huchangia bajeti ya nchi wamekuwa wakitoa malalamiko kuhusu matumizi mabovu ya fedha hizo na wakati mwengine hufikia hatua ya kutishia kutochangia bajeti hizo iwapo serikali itashindwa kudhibiti matumizi yake.