Benki ya Dunia yaitaka serikali ipunguze posho, marurupu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Nora Damian
Mwananchi
20/2/2010

BENKI ya Dunia (WB) imeitaka serikali ihakikishe kuwa inaacha matumizi mabaya fedha za maendelelo, kwa kupunguza posho na marupurupu mbalimbali kwa watumishi wake, ili kuimarisha sekta nyingine.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati wa mkutano wa mapitio ya matumizi ya umma, Mchumi wa benki hiyo, Emmanuel Mungunasi alisema pesa nyingi zimekuwa zikielekezwa kwenye posho na marupurupu, huku sekta muhimu kama za barabara zikikosa pesa za kutosha.

Alisema kati ya mwaka wa 2008/09 serikali ilitumia Sh523 bilioni kama posho na marupurupu mbalimbali hasa katika sekta zinazohusiana na Mkakati wa Kupunguza na Kuondoa Umaskini (Mkukuta).

Alisema posho nyingi zimeelekezwa kwenye wizara mbalimbali, Bunge, Hazina na Mahakama huku pesa hizo zikitolewa kwa kushiriki kwenye mkutano au kuandaa mradi fulani.

Alisema suala la marupurupu kuongezeka kwa kasi si nzuri, kwani linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya nchi husika na hivyo wananchi wake kuzidi kuwa maskini.

"Fedha nyingi zinakwenda kwenye allowance (posho) tujaribu kujibana ili tuweze kupata maendeleo," alisema Mungunasi na kuongeza:

Nchi zenye mifumo ya fedha iliyoendelea vizuri hukua haraka kuliko zenye mifumo duni ya aina hiyo.

Mchumi huyo alisema Benki ya Dunia imekuwa ikifanya tathmini kila mwaka kuhusu mapato na matumizi ya serikali ili kuweza kujua kama fedha zao na zinazotolewa na wafadhili wengine zinatumika ipasavyo.

Hata hivyo, alisema kwa kiasi kikubwa serikali imekuwa ikijitahidi kwa kuhakikisha pesa zilizopangwa zinaenda vizuri hasa katika sekta za elimu, afya na kilimo.

Mchumi huyo aliitaka serikali kuongeza bajeti hasa katika kuimarisha miundombinu kama ya barabara, reli na bandari kwa sababu sekta ya usafirishaji inachangia kukua haraka kwa uchumi na kuongeza kasi ya maendeleo.

Benki hiyo pia imeishauri serikali kuimarisha uwezo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kubuni na kutumia sera endelevu ili kuongeza ukusanyaji wa mapato bila kukwaza shughuli za sekta binafsi.

Katika hatua nyingine, benki hiyo imesema inatarajia kutoa Sh1,000 bilioni katika bajeti ya mwaka 2010/11 zitakazoelekezwa katika sekta za barabara, elimu, afya na maji.

Kwa mujibu wa Mchumi huyo, mdororo wa uchumi uliozikumba nchi nyingi umesababisha kuongezeka kwa msaada huo kutoka Sh800 bilioni katika bajeti iliyopita hadi Sh1,000 bilioni.

Mara kwa mara nchi wahisani ambao huchangia bajeti ya nchi wamekuwa wakitoa malalamiko kuhusu matumizi mabovu ya fedha hizo na wakati mwengine hufikia hatua ya kutishia kutochangia bajeti hizo iwapo serikali itashindwa kudhibiti matumizi yake.
 
Wanampigia mbuzi guitar?!! There is a lot more the WB can do, if they are really serious and mean/stand by their statements. But of course...they like and 'fund' mafisadis to keep Africa undeveloped...in order for the western countries to remain on top!!!
 
Uwii, wouldn't waste my breath if I were them. All their words are falling on deaf ears!
Labda na wao wapunguze funding kwa serikali ndio watasikika
 
Uwii, wouldn't waste my breath if I were them. All their words are falling on deaf ears!
Labda na wao wapunguze funding kwa serikali ndio watasikika

Nakubaliana kabisa na wewe. Hawa nchi za wafadhili na mashirika yao (IMF na WB) mwaka jana walipiga sana kelele na kutishia kutotoa fungu lao katika bajeti ya Tanzania kutokana matumizi mabovu na wizi mkubwa unaofanywa wa pesa hizo toka nchi za Wafadhili.

Imefika wakati sasa wa hawa kuacha kutoa vitisho vyao na kusimamisha kabisa kutoa pesa hizo mpaka watapoona Serikali inapambana na wahusika wote wa ufisadi na pia kupunguza kwa kiasi kikubwa matumizi makubwa ambayo hayaleti maendeleo yoyote kwa Watanzania.
 
- Kuna kiongozi mmoja mzito wa serikali ya sasa aliwahi kuniambia "...kijana hizi safari safari ndio EPA yetu sisi tusio marafiki wa Rais....dawa ni kusafiri tu Rais anasafiri na sisi tunasafiri tu..tunakusanya marupupu" sasa naona hata wakubwa wa dunia wameshitukia, hapo wamegusa pabaya maana umaarufu wa uongozi wa kisiasa ulianza under Mkapa ndio kwa mara ya kwanza marupu rupu ya ajabu yalipoanza kwenye siasa, ninakumbuka under Mwinyi ilikuwa kichekesho sana mambo ya kugombea nafasi za siasa.

- Wallahi hapo World Bank wamegusa pabaya sana, subiri uwasikie watakavyolia na maneno mengi ya ujanja ya kwamba Tanzania ni nchi huru haiwezi kuamuliwa mambo yake na Benki ya Marekani, watch! Walipouziana nyumba zetu za serikali walsiema wameambiwa na hiyo hiyo benki ya dunia sasa tizama watakavyobadilika hapa!

- I do not care what hapo wamegusa pabaya sana, wewe subiri sasa hivi Membe atawaita mabalozi wa nje waache kuingilia mambo ya bongo, watch my words!

Respect


FMEs!
 
Asante babu ila kwa hawa jamaa zetu,......kazi ipo, hawawezi kusikiliza ukizingatia wameingia ili wavune!
 
Sasa wewe unatarajia nini wakati mshahara wenyewe Serikalini ni mkia wa mbuzi? Haidhuru mshahara ungekuwa mdogo lakini social services zikawa nafuu, leo mambo yamekuwa tofauti kabisa. Kila kitu kulipia hospitali, elimu na kadhalika lakini hako kamshahara mhhhhhh!

Sasa munatushauri vipi wajameni? Visafari ndio vinapunguza ile gap pale. Wangetulipa mishahara mikubwa kama ya hiyo Benki hapo tungeweza kuwasikia vyema kabisa.
 
Sasa wewe unatarajia nini wakati mshahara wenyewe Serikalini ni mkia wa mbuzi? Haidhuru mshahara ungekuwa mdogo lakini social services zikawa nafuu, leo mambo yamekuwa tofauti kabisa. Kila kitu kulipia hospitali, elimu na kadhalika lakini hako kamshahara mhhhhhh!

Sasa munatushauri vipi wajameni? Visafari ndio vinapunguza ile gap pale. Wangetulipa mishahara mikubwa kama ya hiyo Benki hapo tungeweza kuwasikia vyema kabisa.

Binti Mkongwe, ukiangalia majirani zetu kama Kenya, Uganda, Rwanda Viongozi wao na hata Mawaziri wao hawana safari nyingi za nje kama kwetu na sidhani mishahara ya viongozi wao wa juu wa Serikali ina tofauti kubwa sana na ya kwetu. Je, kulikoni hawa hawana safari nyingi na ilhali na wao wanalipia kila kitu!? au wao hawapendi pochi kama viongozi wa Tanzania?
 
...viongozi wa Tanzania wanatudharau wananchi. Wanajua hatuwezi kufanya chochote. Wanavurunda, na wataendelea kuvurunda. Sisi kimya tu. Hadi jamaa wa world bank na imf watusemee. Shame on all of us!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom