Benki ya Dunia: Vikwazo 12 vya kufanya biashara Tanzania

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
LICHA ya serikali kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini, Ripoti ya Benki ya Dunia (WB) imetaja vikwazo 12 vya ufanyaji biashara nchini.

Katika ripoti hiyo ya mwaka 2019/20 imeonyesha kuwa Tanzania imeboresha baadhi ya mambo kiasi ya kuifanya kushika nafasi ya 141 kati ya 190 mwaka huu ikilinganishwa na nafasi ya 144 iliyoshika mwaka uliopita.

Maboresho hayo yameifanya Tanzania kushika nafasi ya nne katika nchi za Afrika Mashariki baada ya Rwanda, Kenya na Uganda.

Ripoti hiyo imeitaja Rwanda kushika nafasi ya 29 kati ya 190 ikiwa imeboresha kutoka nafasi ya 41 iliyoshika mwaka jana, huku Kenya ikishika nafasi ya 80 ikitoka nafasi ya 61 hadi mwaka 2018 ikilinganishwa na nafasi ya 80 mwaka 2017. Uganda imeshika nafasi ya 127 na Burundi 168, huku New Zealand ikiongoza.

Baada ya kutoa ripoti hiyo mwaka jana, Tanzania iliboresha baadhi ya mazingira ya ufanyaji biashara mojawapo ikiwa ni kuondoa urasimu, kubadilisha baadhi ya sheria, kupunguza baadhi ya kodi zilizokuwa kero kwa wafanyabiashara, pamoja na kupambana na rushwa.

Baadhi ya mabadiliko yaliyofanyika ni majukumu ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na kuwa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA).

Pia Tanzania imeanzisha kitabu cha maboresho kwa wafanyabiashara (Brueprint) ikiwa na dhumuni la kuweka mazingira wezeshi ya ufanyaji biashara kwa wafanyabiashara.

Ripoti hiyo ilitaja vikwazo 12 ambavyo ilikuwa inaviangalia katika nchi husika ambavyo wafanyabiashara wanakumbana navyo.

Vikwazo hivyo ni mazingira ya kuanzisha biashara, kupata kibali cha ujenzi, upatikanaji wa umeme, usajili wa bidhaa, kuwalinda wawekezaji, makato katika kodi, uingizaji wa bidhaa mipakani, uingiaji wa mikataba, kuajiri wafanyakazi, pamoja na mikataba kati ya wawekezaji na serikali.

Ripoti hiyo ilieleza kuwa kipengele cha uanzishaji wa biashara walikuwa wakiangalia utaratibu, muda na gharama za uanzishaji wa biashara katika nchi husika.

Kwenye kigezo cha kibali, waliangalia utaratibu, muda, gharama za kumaliza ujenzi wa maghala ya kuhifadhi bidhaa, kwenye kigezo cha umeme waliangalia upatikanaji wa umeme wa kutosha kuwezesha viwanda kufanya kazi kwa wakati wote.

Ripoti hiyo ilieleza kuwa kwenye usajili wa bidhaa, waliangalia utaratibu wa kusajili biashara, muda na gharama za kukamilisha taratibu zote hadi mfanyabiashara anaanza kufanya biashara.

Kuwalinda wawekezaji, ripoti hiyo ilieleza kuwa waliangalia namna serikali husika inavyolinda haki za wawekezaji, kwenye ulipaji wa kodi na muda wanaopewa wafanyabiashara wa ulipaji kodi.

Kwenye kipengele za uingizaji bidhaa mipakani, ripoti hiyo ilieleza kuwa iliangalia muda na gharama za kuingiza bidhaa kutoka ndani na nje ya nchi.

“Togo ni miongoni mwa nchi zilizoboresha mazingira ya kufanya biashara kwa mwaka wa pili sasa, wameboresha ada ya kibali cha ujenzi, pamoja na usajili wa bidhaa. Nigeria ipo katika marekebisho ya baadhi ya viashiria,” ilieleza ripoti hiyo.

Aidha, ilieleza kuwa baadhi ya nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kama Afrika Kusini, Liberia, Burundi, Afrika ya Kati na Namibia zimeendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara ikiwamo upatikanaji wa umeme wa kutosha, mfano wafanyabiashara wanalipa zaidi ya asilimia 3,100 ya wanachoingiza kwa siku ili waunganishwe katika gridi.

Ripoti hiyo ilieleza kuwa katika kipengele za kufanya biashara mipakani pamoja na ulipaji wa kodi, wafanyabiashara wanatumia zaidi ya saa 96 kushughulikia nyaraka zao ili kuingiza bidhaa.

Alipotafutwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa, kuzungumzia ripoti hiyo, simu yale ilikuwa ikiita bila majibu.
 
Double cost. Kabla ya kufungua biashara unapewa leseni Halmashauri na unalipia , unalipa na TRA kabla ya kupewa leseni ya biashara
Ukianza tu biashara Halmashauri wanakuja wanakudai Service leavy ,shilingi elfu sitini . Ukiuliza vigezo vya kupata kiwango hicho ni nini ,unaambiwa ni mauzo. Mtu una mwezi mmoja tu kwenye biashara unalipa tozo ambayo base yake wanasema ni mauzo- hiki ni kikwazo-case study kahama mji. hiki ni kikwazo ambcho benki ya dunia hawakijui
Hujakaa sawa wanapita watu wanataka mchango wa mwenge na kiwango unapangiwa kabisa. hiki nacho ni kikwazo ambacho hao benki ya dunia hawakijui
 
Summary:

5. Burundi nafasi ya 168 kati ya nchi 190.

4.Tanzania nafasi ya 141 kati ya 190 mwaka huu ikilinganishwa na nafasi ya 144 iliyoshika mwaka uliopita.

3..Uganda imeshika nafasi ya 127 kati ya 190.

2..Kenya nafasi ya 80 ikitoka nafasi ya 61 hadi mwaka 2018 ikilinganishwa na nafasi ya 80 mwaka 2017.

1.Rwanda Nafasi ya 29 kati ya 190 ikiwa imeboresha kutoka nafasi ya 41 iliyoshika mwaka jana.

Mdogo mdogo tutafika tu,last year tulikua wa 144,this year wa 141.Kuna improvements.
 
Mheshimiwa rais naomba uifanye Tanzania kimbilio la wafanyabiashara/wawekezaji.
Kwenye ripoti hii hakuna rushwa, naomba uisome ripoti halafu waambie watendaji wako kwamba mwaka ujao tuwe nafasi na 100.
Umeme bado utabaki kuwa tatizo kama hakuna ongezeko lingine la uzalisha. 2100 MW za Stiglers bado sana kwa sababu kadiri unavyozalisha umeme ndivyo watumiaji wanaongezeka zaidi. Kwahiyo Mwaka ujao tutakuwa na uhitaji mkubwa zaidi wa umeme Tanzania. Nashauri toeni nafasi wawekezaji binafsi wawekeze kwenye umeme wa jua na upepo kama chanzo mbadala kuelekea kwenye nafasi 100.
Kwenye suala la kulinda wawekezaji bado tuko nyuma sana, bahati mbaya Tz tunawaza kwamba wawekezaji wote wezi na mafisadi
 
Ndyo maana tuna innovative business ideas ila foreign investors wanakwama kuinvest in tanzania. Wanakimbilia kenya na nigeria.
 
Mheshimiwa rais naomba uifanye Tanzania kimbilio la wafanyabiashara/wawekezaji.
Kwenye ripoti hii hakuna rushwa, naomba uisome ripoti halafu waambie watendaji wako kwamba mwaka ujao tuwe nafasi na 100.
Umeme bado utabaki kuwa tatizo kama hakuna ongezeko lingine la uzalisha. 2100 MW za Stiglers bado sana kwa sababu kadiri unavyozalisha umeme ndivyo watumiaji wanaongezeka zaidi. Kwahiyo Mwaka ujao tutakuwa na uhitaji mkubwa zaidi wa umeme Tanzania. Nashauri toeni nafasi wawekezaji binafsi wawekeze kwenye umeme wa jua na upepo kama chanzo mbadala kuelekea kwenye nafasi 100.
Kwenye suala la kulinda wawekezaji bado tuko nyuma sana, bahati mbaya Tz tunawaza kwamba wawekezaji wote wezi na mafisadi
ukiangalia vigezo vinavyotumika kuzigrade nchi sio deal sana kuwa namba za chini.
 
Kagame anampango na mikakati ya kuifanya Rwanda kua Dubai ya Afrika mashariki, Anajitahidi kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.
 
Kipindi hiki cha uchaguzi mwenyekiti wa mtaa naye kapita anaomba mchango, usiku police wa doria wanapita na kuomba waongezewe mafuta gari imewasha taa.
Double cost. Kabla ya kufungua biashara unapewa leseni Halmashauri na unalipia , unalipa na TRA kabla ya kupewa leseni ya biashara
Ukianza tu biashara Halmashauri wanakuja wanakudai Service leavy ,shilingi elfu sitini . Ukiuliza vigezo vya kupata kiwango hicho ni nini ,unaambiwa ni mauzo. Mtu una mwezi mmoja tu kwenye biashara unalipa tozo ambayo base yake wanasema ni mauzo- hiki ni kikwazo-case study kahama mji. hiki ni kikwazo ambcho benki ya dunia hawakijui
Hujakaa sawa wanapita watu wanataka mchango wa mwenge na kiwango unapangiwa kabisa. hiki nacho ni kikwazo ambacho hao benki ya dunia hawakijui
 
Hata kwa wazawa tu hali ni ngumu mno kuna msururu wa ushuru, kodi, tozo, leseni & vibali
 
Hata
LICHA ya serikali kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini, Ripoti ya Benki ya Dunia (WB) imetaja vikwazo 12 vya ufanyaji biashara nchini.

Katika ripoti hiyo ya mwaka 2019/20 imeonyesha kuwa Tanzania imeboresha baadhi ya mambo kiasi ya kuifanya kushika nafasi ya 141 kati ya 190 mwaka huu ikilinganishwa na nafasi ya 144 iliyoshika mwaka uliopita.

Maboresho hayo yameifanya Tanzania kushika nafasi ya nne katika nchi za Afrika Mashariki baada ya Rwanda, Kenya na Uganda.

Ripoti hiyo imeitaja Rwanda kushika nafasi ya 29 kati ya 190 ikiwa imeboresha kutoka nafasi ya 41 iliyoshika mwaka jana, huku Kenya ikishika nafasi ya 80 ikitoka nafasi ya 61 hadi mwaka 2018 ikilinganishwa na nafasi ya 80 mwaka 2017. Uganda imeshika nafasi ya 127 na Burundi 168, huku New Zealand ikiongoza.

Baada ya kutoa ripoti hiyo mwaka jana, Tanzania iliboresha baadhi ya mazingira ya ufanyaji biashara mojawapo ikiwa ni kuondoa urasimu, kubadilisha baadhi ya sheria, kupunguza baadhi ya kodi zilizokuwa kero kwa wafanyabiashara, pamoja na kupambana na rushwa.

Baadhi ya mabadiliko yaliyofanyika ni majukumu ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na kuwa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA).

Pia Tanzania imeanzisha kitabu cha maboresho kwa wafanyabiashara (Brueprint) ikiwa na dhumuni la kuweka mazingira wezeshi ya ufanyaji biashara kwa wafanyabiashara.

Ripoti hiyo ilitaja vikwazo 12 ambavyo ilikuwa inaviangalia katika nchi husika ambavyo wafanyabiashara wanakumbana navyo.

Vikwazo hivyo ni mazingira ya kuanzisha biashara, kupata kibali cha ujenzi, upatikanaji wa umeme, usajili wa bidhaa, kuwalinda wawekezaji, makato katika kodi, uingizaji wa bidhaa mipakani, uingiaji wa mikataba, kuajiri wafanyakazi, pamoja na mikataba kati ya wawekezaji na serikali.

Ripoti hiyo ilieleza kuwa kipengele cha uanzishaji wa biashara walikuwa wakiangalia utaratibu, muda na gharama za uanzishaji wa biashara katika nchi husika.

Kwenye kigezo cha kibali, waliangalia utaratibu, muda, gharama za kumaliza ujenzi wa maghala ya kuhifadhi bidhaa, kwenye kigezo cha umeme waliangalia upatikanaji wa umeme wa kutosha kuwezesha viwanda kufanya kazi kwa wakati wote.

Ripoti hiyo ilieleza kuwa kwenye usajili wa bidhaa, waliangalia utaratibu wa kusajili biashara, muda na gharama za kukamilisha taratibu zote hadi mfanyabiashara anaanza kufanya biashara.

Kuwalinda wawekezaji, ripoti hiyo ilieleza kuwa waliangalia namna serikali husika inavyolinda haki za wawekezaji, kwenye ulipaji wa kodi na muda wanaopewa wafanyabiashara wa ulipaji kodi.

Kwenye kipengele za uingizaji bidhaa mipakani, ripoti hiyo ilieleza kuwa iliangalia muda na gharama za kuingiza bidhaa kutoka ndani na nje ya nchi.

“Togo ni miongoni mwa nchi zilizoboresha mazingira ya kufanya biashara kwa mwaka wa pili sasa, wameboresha ada ya kibali cha ujenzi, pamoja na usajili wa bidhaa. Nigeria ipo katika marekebisho ya baadhi ya viashiria,” ilieleza ripoti hiyo.

Aidha, ilieleza kuwa baadhi ya nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kama Afrika Kusini, Liberia, Burundi, Afrika ya Kati na Namibia zimeendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara ikiwamo upatikanaji wa umeme wa kutosha, mfano wafanyabiashara wanalipa zaidi ya asilimia 3,100 ya wanachoingiza kwa siku ili waunganishwe katika gridi.

Ripoti hiyo ilieleza kuwa katika kipengele za kufanya biashara mipakani pamoja na ulipaji wa kodi, wafanyabiashara wanatumia zaidi ya saa 96 kushughulikia nyaraka zao ili kuingiza bidhaa.

Alipotafutwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa, kuzungumzia ripoti hiyo, simu yale ilikuwa ikiita bila majibu.
Hata ufanyeje huwezi kumfurahisha mwamerka kwa asilimia mia
 
Inasikitisha sana, ndio maana maendeleo yetu ni mwendo wa Kinyonga. Biashara ndio kila kitu kwenye nchi.
Double cost. Kabla ya kufungua biashara unapewa leseni Halmashauri na unalipia , unalipa na TRA kabla ya kupewa leseni ya biashara
Ukianza tu biashara Halmashauri wanakuja wanakudai Service leavy ,shilingi elfu sitini . Ukiuliza vigezo vya kupata kiwango hicho ni nini ,unaambiwa ni mauzo. Mtu una mwezi mmoja tu kwenye biashara unalipa tozo ambayo base yake wanasema ni mauzo- hiki ni kikwazo-case study kahama mji. hiki ni kikwazo ambcho benki ya dunia hawakijui
Hujakaa sawa wanapita watu wanataka mchango wa mwenge na kiwango unapangiwa kabisa. hiki nacho ni kikwazo ambacho hao benki ya dunia hawakijui
 
Back
Top Bottom