Benki ya CRDB yapunguza viwango vya riba ya mikopo na kuongeza muda wa marejesho kwa watumishi

Watumishi wa umma msiogope kukopa kopeni kwa sababu uwezo wa kila mwezi kusave kidogo ajiri ya maendeleo binafsi ni vigumu kopa pesa asilimia ishirini ya mkopo wako wekeza ili upate japo mia mbili ya nyanya nyumbani, alafu asilimia 80 fanya maendeleo yako binafsi

Mfano kijana uliyeanza ajira una uhitaji wa kujijenga ndani fenicha nk, usisikilize maneno ooh unakopa unanunua kitanda kopa mkopo wa mda mfupi let say miaka miwili, kamilisha zoezi la fenicha nk, tulia acha pesa kidogo bank kama akiba ili ukiwa na shida jikope mwenyewe wewe tulia wenzako watakubeza watakucheka achana nao

Miaka miwili utaisha fasta utajikuta ushahama katika zoezi la fenicha za ndani, utaanza kupanga malengo mengine wale waliokucheka utaona wapo vile vile na ujuaji wao wengine hata kikombe cha maji hawana

Kwakua mkopo wa awali umeisha jipange tena jilipue tena miaka miwili, kama eneo ulipo aridhi ni cheap usiogope nunua kiwanja, pesa nyingine anza izungusha mdogo mdogo unachokipata endeleza kiwanja usianze ujnzi kusanya materials mdogo mdogo bila presha,

Miaka miwili itaisha tena tayali unakiwanja na materials unayo, kumbuka hapo tayali una miaka minne kazini ila tayali ushajijenga ndani na tayali una kiwanja na materials unayo

Baada ya hapo sasa jilipue parefu kama hivi unakutana na CRDB miaka saba jitundike, chukua pesa yako kwakua materials yapo nenda site inua nyumba yako kamilisha kabisa ingia, pesa inayobakia zungusha

Kumbuka hapo una miaka mitano kazini tayali upo kwako basi hapo anza sasa kucheza na fursa anza kuonyesha njaa ya pesa komaa itafuta pesa ajiri ya kutoboa sasa

NB
Watumishi wengi hukopa pesa ndefu kwa lengo la biashara uku biashara hawazijui matokeo yake biashara hufa, pesa upotea na hakuna lolote la maana walilofanya matokeo yake huchukia kazi na mikopo
 
Hivi hili punguzo la riba linawahusu na wale waliokopa kabla ya tangazo hili kutolewa? Yani nao rate zao zitashuka?
 
Absolutely right! Rejea jedwali la BancABC (BancABC) mikopo ya mwaka 1, 2, na 3 (miezi 12, 24, 34). Kwa mfano, ukichukua mkopo wa TZS. 35,000,000 hesabu yake inakuwa kama ifuatavyo:-

Kwa miezi 36: 1,282,960.70 x 36 = 46,186,585.20 (benki inachukua 46,186,585.2 - 35,000,000 = 11,186,585.20)
Kwa miezi 24: 1,764,301.60 x 24 = 42,343,238.40 (benki inachukua 42,343,238.40 - 35,000,000 = 7,343,238.40)
Kwa miezi 12: 3,225,480.24 x 12 = 38,705,762.88 (benki inachukua 38,705,762.88 - 35,000,000 = 3,705,762.88)

I have now got the concept; mikopo ya muda mrefu ni balaa. Na walivyo, they never clarify this to customers! Some sort of utapeli fulani.
@gui1 kwa mujibu wa hii comment anayenufaika ni bank...
 
pic+crdb.jpg

Dar es Salaam. Benki ya CRDB imeongeza muda wa marejesho kutoka miezi 60 hadi 84 huku ikishusha riba kwa asilimia nne kwa wateja wake, hasa wafanyakazi.

Benki hiyo imeshusha riba kutoka asilimia 21 mpaka 17 huku muda wa marejesho ukitofautiana kati ya wafanyakazi wa sekta binafsi na watumishi wa umma.

Wateja wa benki hiyo wameanza kunufaika na punguzo hilo tangu wiki iliyopita pindi menejimenti iliporidhia kufanya mabadiliko hayo.

Akizungumza na Mcl Digital leo Mei 13, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Dk Charles Kimei amesema mabadiliko hayo yanalenga kumpa mteja unafuu wa kukamilisha malengo yake kwa wakati.

“Punguzo hili linatolewa kwenye matawi yetu yote. Tangu wiki iliyopita huduma hiyo imeanza kupatikana,” amesema Dk Kimei.

Watumishi wa umma ambao awali walikuwa wanafanya marejesho mpaka miaka sita ambayo ni sawa na miezi 72, sasa wanaruhusiwa kufanya hivyo mpaka miezi 84 au miaka saba wakati wafanyakazi wa sekta binafsi waliokuwa na miaka mitano wameongezewa mpaka miaka sita.

Hatua ya CRDB imekuja baada ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kushusha riba ya mikopo inayotoa kwa benki za biashara mara mbili mfululizo.

Machi mwaka jana, ilipunguza riba hiyo kwa asilimia nne kutoka asilimia 16 mpaka 12.

Mwaka mmoja baadaye, BOT ilipunguza tena kwa asilimia moja na kushusha kiwango cha akiba ambacho benki hizoa zinatunza kwake kutoka asilimia 10 mpaka nane ili kuzipa uwezo zaidi wa kuikopesha sekta binafsi.

Chanzo: Mwananchi
NMB kukoje ,Riba haijapungua! nataka chukua milioni nane kwa miaka 6
 
Ila niwambieni kitu,kama umepata buss ya kufanya nashauri kopeni kwa hiyo miaka 7 ambapo total interest haitazidi 60% na hivyo kwa kanuni ya reducing balance inakua poa.Mathalani umekopa 10m na urejeshe ndani ya miaka 7 ambayo itakuwa kama 10.6m,hiyo 10m uliyoikopa,ukiizungusha ndani ya miaka miwili ukapata 10m nyingine tena,nakushauri warudishie ile ulioichukua na tena na hakika utalipa hata 8m kwa kesh.
 
Hii
HAKUNA KILICHOPUNGUZWA HAPO... NI UHUNI TU.. MIAKA IMEONGEZWA 7 TOKA 6.. NA RIBA WAMEPUNGUZA TO 17% KITU NI KILE KILE.. FANYA MATHS UTAONA AT THE END UNALIPA KILE KILE AU ZAIDI. Riba bado kubwa mno mnoooo... mnoooooo... 17% kwa 7 yrs..? Banks zingeweza toa kwa 11% na kupata faida kubwa kwa sbb:

1: watapata wateja wengi sana wakishusha riba to 11%

2: kama BOT wamewashushia banks riba hadi 8% na banks binafsi ikamkopesha mwananchi kwa 11% ana faida ya 3%... Hiyo 3% ni kubwa sana sanaaaa sbb wakishusha to 11% watapata wateja wengi sana na faida yao ya 3% itakuwa kubwaa ..

17% bado kubwa mnoo mnoooooo... Hakuna kitu hapo
Hii ni biashara kama biashara nyingine sio msaada.
Mfano MTU akope anunue labda tata bus kwa million 95.
Kwa siku mapato yawe 200000. Hii laki mbili igawanye Mara nne. Nikimaanisha baada ya kupewa mauzo na dereva wako, itabidi uweke akiba ya service, insurance,kodi na kadhalika. Pia na siku ambazo hutafanya kazi unazifidia kwenye huo mgawanyo. Utajikuta kwa siku unabaki na 50000. Ukizidisha kwa siku 30 unajikuta unapata kitu kama 1500000. Ukiizidisha kwa miezi 84 ambayo ndo miaka saba, utapata 126mil ukitoa 95mil unabaki na 31mil.je unaweza je ulilinganisha we na bank nan kagain zaid. Maana bank ungeenda ulipokuwa unakopa hii 95mil, marejesho kwa miaka saba ni total interest ni 68mil, total payment ni 163mil, faida ya bank ni kama 68 wakati wewe ukitoa asset n zaid ya 50mil.
OK tuchukue umekopa 100mil ukanunua machine ya kusaga na kukoboa kwa ajili ya kutengeneza sembe.
Mil 20 machine,umeme mil 80 kwenye mahindi. Kwa milio80 kwa sasa utapata tani 160.
Kwa kila tani kumi weka faida ya 300000 na kwa mwez ukawa na uwezo Wa tan 160, unajikuta kwa mwez unaingiza kama mil4.8 ukizidisha kwa miezi84 unapata karibia mil400. Je nan anapata faida kama sio mkopaji.
Wengi wetu tunaziona riba kubwa sabab tunakopa ili tununue magari au kujengea ilihali dhumuni LA mkopo ni kuwekeza
 
Tatizo Masharti yamekua mengi, unakuta unatakiwa uende na Wakili/mwanasheria akakugongee muhuri wake(utalipa pesa), unatakiwa uweke stamp duty(utalipia pesa) hii yote inahusika vip kwenye Mkopo wa Mfanyakazi?
Wakati mwingine ni heri uende NMB ambapo hakuna masharti mengi ILA tatizo la NMB ni moja tu. LOAN PROCESSING FEE yao ni kubwa mnoinaweza kufika hadi Milion 1.5 kwa mkopo wa Milioni 18
Ushauri wangu NMB punguzeni iyo Gharama ya Loan processing fee inakimbiza wateja
na
CRDB punguzeni masharti hasa hili la muhuri wa Wakili na stamp duty
 
Absolutely right! Rejea jedwali la BancABC (BancABC) mikopo ya mwaka 1, 2, na 3 (miezi 12, 24, 34). Kwa mfano, ukichukua mkopo wa TZS. 35,000,000 hesabu yake inakuwa kama ifuatavyo:-

Kwa miezi 36: 1,282,960.70 x 36 = 46,186,585.20 (benki inachukua 46,186,585.2 - 35,000,000 = 11,186,585.20)
Kwa miezi 24: 1,764,301.60 x 24 = 42,343,238.40 (benki inachukua 42,343,238.40 - 35,000,000 = 7,343,238.40)
Kwa miezi 12: 3,225,480.24 x 12 = 38,705,762.88 (benki inachukua 38,705,762.88 - 35,000,000 = 3,705,762.88)

I have now got the concept; mikopo ya muda mrefu ni balaa. Na walivyo, they never clarify this to customers! Some sort of utapeli fulani.
Hii hesabu ya riba unaipataje kwa miezi 12,24 au 36
 
Mi sirudii tena kukopa mikopo ya bank ya muda mrefu....
Nilichukua mkopo WA nyumba ktk bank moja, wakati huo sikuwa hata na elimu Sana ya mikopo na wao hawakunielewesha kivilee...

Sasa ni mwaka WA tisa naingia mwaka WA kumi, mkopo WA 35 mil, Nikihesabu hadi 2020 nitakua nimelipa jumla ya 80 mil! Roho imeniuma ila Sina jinsi...ila tena nikifikiria ingekua Si huu mkopo labda nisingekuwa na hiyo nyumba pia hapo ndo napata kamoyo kidogo ila kiukweli sio poa kabisa hiyo mikopo, ni shida! ..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi sirudii tena kukopa mikopo ya bank ya muda mrefu....
Nilichukua mkopo WA nyumba ktk bank moja, wakati huo sikuwa hata na elimu Sana ya mikopo na wao hawakunielewesha kivilee...

Sasa ni mwaka WA tisa naingia mwaka WA kumi, mkopo WA 35 mil, Nikihesabu hadi 2020 nitakua nimelipa jumla ya 80 mil! Roho imeniuma ila Sina jinsi...ila tena nikifikiria ingekua Si huu mkopo labda nisingekuwa na hiyo nyumba pia hapo ndo napata kamoyo kidogo ila kiukweli sio poa kabisa hiyo mikopo, ni shida! ..

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana.. vp huwezi pambana ili ulipe kiasi kilichobaki bila riba kama utamudu lakini.. kama ishalipiwa 20millions unalipa 10 fasta bila riba
 
Hizi benk huwa wanatoa Mikopo ya biashara
Sasa raia anakopa anaenda kujenga nyumba ya kukaa au ananunua gari la kutembelea na familia as if wao ni biashara halafu anaanza kulialia humu
Kama kushauri ningemshauri mtu usiokope mkopo wa biashara kama hana biashara. Kopa mkopo wa biashara kuiendeleza biashara yako ambayo una uzoefu nayo na umeshaona gap lipo wapi
 
Back
Top Bottom