Benki Kuu ya Tanzania, liangalieni Hili la D9 Club, Rwanda wamepigwa Marufuku

Laface77

JF-Expert Member
Jul 9, 2008
2,117
2,845
Jana nimesoma memo ya Benki Kuu ya Rwanda wakipiga marufuku utapeli wa kimtandao unaokwenda kwa jina la D9 Club kwa sababu wameeleza ni Pyramid Scheme/Ponzi Scheme ambapo wale waliotangulia huwa wananufaika kwa gharama ya wale watakaoingia kwa kuchelewa.

Kwa kweli naipongeza sana Benki Kuu ya Rwanda kwa hatua hii ya kulinda interests za wananchi wa Rwanda ili watu wengine wasinufaike kwa gharama za watu wengine. Tena wameenda mbali kwa kutaja hata jina la muanzilishi wa hiyo scheme nchini Rwanda pamoja na nchi ambazo huo mtandao umeenea sana ikiwepo Tanzania.

Sasa concern yangu ni kwa Benki Kuu ya Tanzania ambayo mpaka sasa iko kimya kuhusu utapeli huu. Hii hii benki kuu yetu iko kwa ajili ya kusimamia tu sekta ya mabenki na kuyapiga faini pale yanapoenenda kinyume na taratibu za uendeshaji wa mabenki au hata kulinda maslahi ya kifedha ya wanachi wa Tanzania. Ina maana mpaka leo hawajajua kuna utapeli wa aina hii unaendelea mpaka kanchi kadogo kama Rwanda kametuzidi katika hili? Nimeona baadhi ya Benki kama Tanzania Postal Bank na Equity bank zimetoa memo ya kuwaonya wafanyakazi wake wasije kushiriki katika scheme hii kwani ni utapeli na kinyume na maadili. Ifike mahali Benk Kuu ya Tanzania mfanye zaidi ya ku-regulate mabenki, muwalinde wanachi wa Tanzania ambao wengi wao hawana taarifa.

Angalia jinsi wananchi wengi wa Tanzania walivyopoteza fedha na mali zao wakati Benki Kuu ya Tanzania wakiwa kimya tuu. Kuna watu walipoteza hata nyumba zao kwa kuweka dhamana ili wapate fedha za kwenda kupand mbegu DECI. No wonder mkulu jana amewashangaa na kusema pale Benki Kuu kuna PhD 17 lakini hawalioni hili.
5af0c94f-a230-4d8e-8b47-66952dec027a.jpg
 
Ngoja watu waumizwee ndy bot wata wablock
Watz wanapenda slope cha ajabu watu waliyoingizwa kwenye hayo ma d9,onecoin etc
Wako madokta,wanasheria,wapo watu walioenda shule lkn wameingizwa humo na wenyewe wanakuambia hzo zote ziko salama

OvA
 
Waache watapeliwa watu hawajifunzi kutoka kwa DECI.
Wafanye kazi,biashara,kilimo nk , hakuna fedha za bure .
 
Hizo hela si za benki yoyote
fedha zinawekwa na wao member wa D9 waacheni wacheze kivyao
Mbona BiPesa, sportPesa BET zinatumia Kamari na hiyo Bitcoin hazifungiwi?
Huyo Abbas Tarimba msimamizi wa Michezo ya kubahatusha kaiingiza SportPesa hamumumuulizi aliupata wapi mchezo huo.
D9 inahusika na michezo na hasa mpira wa miguu. na ukiweka ni kimataifa, unahusiana na Hong-Kong Brasilia na Nchi baadhi km Uganda Kenya na Tanzania.
Kinachowauma ni huo ulipwaji ambao Benki zote hawawezi kulipa, pia ulimwengu umeshaingia kwenye Bitcoin ambayo ni currency isiyowea dhibitiwa na benki yoyote Duniani
ACHENI KASHFA NA MINENO YA KUBEZA HAMJALAZIMISHWA KUCHEZA
 
Hizo hela si za benki yoyote
fedha zinawekwa na wao member wa D9 waacheni wacheze kivyao
Mbona BiPesa, sportPesa BET zinatumia Kamari na hiyo Bitcoin hazifungiwi?
Huyo Abbas Tarimba msimamizi wa Michezo ya kubahatusha kaiingiza SportPesa hamumumuulizi aliupata wapi mchezo huo.
D9 inahusika na michezo na hasa mpira wa miguu. na ukiweka ni kimataifa, unahusiana na Hong-Kong Brasilia na Nchi baadhi km Uganda Kenya na Tanzania.
Kinachowauma ni huo ulipwaji ambao Benki zote hawawezi kulipa, pia ulimwengu umeshaingia kwenye Bitcoin ambayo ni currency isiyowea dhibitiwa na benki yoyote Duniani
ACHENI KASHFA NA MINENO YA KUBEZA HAMJALAZIMISHWA KUCHEZA
Hongera sana. Hongera zaidi kama upo on top of pyramid
 
Back
Top Bottom