Benki Kuu ya Rwanda yaipiga marufuku kampuni ya D9 Club

njeeseka

JF-Expert Member
Oct 19, 2012
1,371
976
Tayari kuna zuio la hii club kufanya shughuli zake Rwanda.
Ni wakati sasa Tanzania kuchukua hatua haraka, yale ya Deci yasijirudie.
Nitawaletea nakala ya zuio hapa.

IMG-20170613-WA0000.jpg
 
D9, One Coin na nyinginezo ni utapeli wa hali ya juu.

Watanzania acheni kupenda vitu vya bure, hakuna maisha rahisi hivyo kwamba unampa mtu hela kisha wewe unaenda kuchota tu, mwishowe utaishia kuchotwa.

Watu wanakuahidi faida kubwa wakati hata hawajawekeza hata kwenye kuuza nyanya, usijiulize hiyo faida unayopata inatoka kwenye biashara gani? Kuna faida inaweza kua inadondoka tu bila kufanya biashara?

Anyway, siku zote wajinga ndio waliwao.
 
Inadaiwa kuwa piramidi..yaani upatu. Akaunti zake za benk pia zazuiliwa
Tuwe makini maana wametaja biashara hii ya upatu kusambaa mpaka Tanzania.
Wasalaam, Kirerenya

WhatsApp Image 2017-06-13 at 10.03.46.jpeg
 
Watanzania wanapenda kitongaa .....kwenye kupanda mlimaaa hawataki

Ova
 
Ni bahati mbaya sana wale wanaojiita "walokole" ndio waathirika wakubwa sana wa mitandao ya kitapeli kiasi hichi kwani wameathiriwa na mahubiri ya mafanikio wakitaka Mungu awape fedha pasipo kufanya kazi ili waweze kutoa ushuhuda kuwa "Mimi mnayeniona sikuwa nastahili ila ni Mungu ndio aliniwezesha"! Angalia zaidi ya 50% ya waathirika wa DECI walitokea kwenye madhehebu ya kilokole, hata waanzilishi wao walikuwa wachungaji wa kilokole ambao wanaamini kuwa Mungu kazi yake kubwa ni kuwapa hela, nyumba magari na wake/wame!
 
Wadau wenzangu wa BI, leo kuna rafiki yangu alinialika kwenye Mkutano mmoja a So Called D9 Tanzania Group, Pale Kebbys Hotel Bamaga. Nikaingia kwenye Darasa na Kusikiliza, Mafunzo niliyoyapata ni Mazuri mpaka nikahamisika Kujiunga, sasa tukiwa katika Hatua za Mwisho kumaliza Darasa, Kumbe Miongoni mwa wanafunzi wenzangu Kama Sita hivi, Kumbe walikua ni Maafisa wa Usalama, na wamekua wakihudhuria hayo Mafunzo karibia Week 2. Sasa kilichotokea wakawakamata Viongozi wa hiyo D9 akiwemo mwanzilishi wa hapa Tanzania, ambaye ni Kijana tu mdogo anaitwa Benny, kiukweli kwa alivyo tueleza Jamaa ana hela na Amefanikiwa sana. Mara tukaambiwa tushuke Chini, Jamaa wakaanza kuzozana wakatiwa Nguvuni Mpaka kwenye Magari ya Polisi pale chini, Moja ya vitu jamaa walivyoulizwa ni, Waonyeshe Ofisi zao, Usajili wa hiyo D9 kwa hapa Tanzania, Account za Bank vyote jamaa Hana, kumbe pesa anaingiziwa kwenye personal account, halafu hana Usajili, watu tukabaki tumeraharuki hapo hatujui nn tufanye, Jamaa wakaondoka nae. Sasa nikabaki na maswali Mengi hivi inakuaje mtu unafanya Biashara ya Mamilioni yote hayo mpaka $ 60,000/= Kila week anaingiza kama faida na zinaingia kwenye accounts yake halafu Fedha nyingine anatuma kwa huyo Mwanzilishi wa D9 Africa ambaye ni Mganda, nae anatumiwa kwa personal account. Sasa watu wamebaki hapo hawajui hatma yao, na mm kesho nilikua nategemea Kuanza ila Nimesita kutokana na hili lililotokea Leo. Najua kama kuna mwana BI humu na ni Member atakua amesikia hii ishu Jioni hii. Nimetoa tu hii taarifa kwa nia Njema wala si kuwakatisha tamaa ila nimeshuhudia kwa macho na Masikio yangu. Asanteni(COPPIED FROM MAIN SOURCE)
 
Wadau wenzangu wa BI, leo kuna rafiki yangu alinialika kwenye Mkutano mmoja a So Called D9 Tanzania Group, Pale Kebbys Hotel Bamaga. Nikaingia kwenye Darasa na Kusikiliza, Mafunzo niliyoyapata ni Mazuri mpaka nikahamisika Kujiunga, sasa tukiwa katika Hatua za Mwisho kumaliza Darasa, Kumbe Miongoni mwa wanafunzi wenzangu Kama Sita hivi, Kumbe walikua ni Maafisa wa Usalama, na wamekua wakihudhuria hayo Mafunzo karibia Week 2. Sasa kilichotokea wakawakamata Viongozi wa hiyo D9 akiwemo mwanzilishi wa hapa Tanzania, ambaye ni Kijana tu mdogo anaitwa Benny, kiukweli kwa alivyo tueleza Jamaa ana hela na Amefanikiwa sana. Mara tukaambiwa tushuke Chini, Jamaa wakaanza kuzozana wakatiwa Nguvuni Mpaka kwenye Magari ya Polisi pale chini, Moja ya vitu jamaa walivyoulizwa ni, Waonyeshe Ofisi zao, Usajili wa hiyo D9 kwa hapa Tanzania, Account za Bank vyote jamaa Hana, kumbe pesa anaingiziwa kwenye personal account, halafu hana Usajili, watu tukabaki tumeraharuki hapo hatujui nn tufanye, Jamaa wakaondoka nae. Sasa nikabaki na maswali Mengi hivi inakuaje mtu unafanya Biashara ya Mamilioni yote hayo mpaka $ 60,000/= Kila week anaingiza kama faida na zinaingia kwenye accounts yake halafu Fedha nyingine anatuma kwa huyo Mwanzilishi wa D9 Africa ambaye ni Mganda, nae anatumiwa kwa personal account. Sasa watu wamebaki hapo hawajui hatma yao, na mm kesho nilikua nategemea Kuanza ila Nimesita kutokana na hili lililotokea Leo. Najua kama kuna mwana BI humu na ni Member atakua amesikia hii ishu Jioni hii. Nimetoa tu hii taarifa kwa nia Njema wala si kuwakatisha tamaa ila nimeshuhudia kwa macho na Masikio yangu. Asanteni(COPPIED FROM MAIN SOURCE)
Acha uongo wewe hapo mwanzoni unasema ulihamasika hadi ukajiunga afu mwishoni mwa uzi huu unasema umestuka kwamba hujajiunga na hii inshu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom