Benki Kuu (BoT), yasitisha leseni za maduka ya kubadilishia fedha za kigeni Tanzania

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,269
Gavana wa Benki Kuu (BoT), Prof. Luoga atazungumza na vyombo vya habari mchana huu, kuanzia saa nane, kutokea jijini Arusha
==========
Gavana wa Benki Kuu amethibitisha kuwa oparesheni ya kufanya ukaguzi katika baadhi ya maduka ya kubadilishia fedha jijini Arusha iliendeshwa na Benki yake kwa kushirikisha vyombo mbalimbali vya dola ili kubaini watuhumiwa wa uhalifu wa kutakatisha fedha.

Gavana Luoga amesisitiza kuwa watuhumiwa walipkamatwa katika zoezi hilo wanahojiwa na hatua za kisheria zitachukua mkondo wake.

Gavana Luoga amesisitiza kuwa kufuatia askari wengi wa Jeshi la Polisi kuwa katika usimamizi wa mitihani ya kidato cha pili, taasisi yake ilihusisha askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wasio na silaha ili kuongeza nguvu katika kufanikisha zoezi hilo.

Dscr66kXcAAXbFC.jpg
2.jpg
3.jpg
4.png


Habari zaidi, soma=>Arusha: Maduka yote ya kubadilishia fedha za kigeni(Forex) yasimamiwa na JWTZ, wananchi watakiwa kwenda Benki Kuu - JamiiForums

Zaidi soma hapa ARUSHA: Huduma za kubadilisha fedha sasa kupatikana Benki na Hoteli kitalii - JamiiForums
 

Attachments

  • TAARIFA YA BENKI KUU KWA UMMA 201118.pdf
    86.2 KB · Views: 80

Similar Discussions

Back
Top Bottom