Benjamin William Mkapa nimjuaye...

Aliruhusu mke wake aibe mchana na usiku hata hela za ngo ya kusaidia yatima na wamama wa kimaasai - "sawa kwa wote" so help us god.
 
Mkapa alifanya kitu ambacho kama tungekuwa tunasapoti juhudi hai na endelevu basi tusingemsahau kwa mambo mazuri aliyoyafanya huyu jamaa.

JK anaonekana kutofanya kitu kwa sababu mapengo yanayohitaji kuonekana kama yamefanywa na kiongozi yalizibwa tayari na Mkapa.

Kinachotushinda saa hizi ni sisi wenyewe hakuna wa kumlaumu, matatizo yote ni sisi wenyewe wala hakuna wakulaumiwa, kwanza tujinyoshee vidole sisi wenyewe, sisi tuna matatizo makubwa ambayo hatutaki kuyakubali
 
Unajua kuna uwezekano mkubwa sana vizazi vijavyo vikafukua makaburi yetu ili kufanyia uchunguzi mafuvu yetu na kuangalia tulikuwa wapumbavu kiasi gani mpaka mambo yote haya tuliweza kuyaacha tu. KIWIRA Coal Mine na Mkapa ni ndugu moja lakini wabunge wetu wamekaa kimya tu wa hawachukui hatua yoyote ile ya kisheria dhidi ya Mkapa.
 
Rais bora wa TZ next to Mwl. J. Nyerere

Aliingia madarakani kwa haki bila rushwa wala kununua vyombo vya habari. Alikuwa na hoja na alieleza WAZI nia yake ya kugombea urais.

Alianza kazi kwa kasi hakungoja wiki mbili au zaidi kupanga baraza la mawaziri.

Aliunda serikali ndogo kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.

Alikuwa na falsafa binafsi, dira na msomi aliyependa kusoma na kujifunza.

Akapambana kijemedari kwelikweli na misukosuko ya Reli, MV Bukoba, Elnino na majanga mengine. Akapunguza mfumuko wa bei toka 48% 1994 na kubakia single digit enzi zote za utawala wake.

Akaboresha utumishi wa umma; kapunguza wafanyakazi hewa na kuboresha maslahi.

Akapunguza deni la nje na kuipa Tanzania heshima.

Akajenga miundo mbinu hususan barabara kwa kasi kubwa

Akavutia wawekezaji wenye tija kama TBL, NBC n.k

Akajenga EPZ alipanga zijengwe 22 nchi nzima

Akaimarisha majeshi yetu kwa kuwapatia motisha vitendea kazi na makazi.

Akajenga Uwanja wa Taifa

Akajenga Benki kuu Twin towers na kule Zanzibar. Twin Towers kama Bank of Canada, Toronto (kwa wanaojua)

Alikuwa na hoja zenye mashiko.

Alikuwa kiongozi kweli jasiri, mwenye kujiamini na hakuogopa mihadhara: iwe ya vyama vya siasa, vyuo vikuu au kimataifa. Alikuwa full of substance.

Ujasiri wake hata vita ingetokea enzi zake angetuongoza vyema sana kumshinda adui.

Hakuwa mwongo katika kauli na ahadi zake.

Alikuwa na maadili na na hekima na aliheshimu mamlaka na taratibu zilizopo.

Akawapa nguvu na haki zaidi wanawake.

Alipigania utandawazi kuwanufaisha wengi.

Alikuwa mchapakazi hakuwa mvivu.

Alikuwa makini na alipinga na kukwepa sana matumizi yasiyo lazima ya serikali.

Alisafiri ng’ambo pale tu ilipobidi. Alikaa ofisini na kufanya kazi.

Alijiheshimu hakuwa Fataki.

Hakuwa ombaomba, bali alipenda kujenga uwezo, kujitegemea na kuwasaidia ombaomba.

Akanunua ndege bora ya Rais, mafisadi wakaipinga.

Akanunua rada ya nguvu, mafisadi wakaipinga.

Alikuwa na vyeti vya nguvu na alifuzu vyema masomo yake. Alionyesha uwezo. Alikuwa na speech za kisomi.

Alihakikisha nchi inakaribia kupaa ndio akaikabidhi kwa JK. Tukadhani itapaa.

Na mengine mengi.

Huyo ndiye Benjamin William Mkapa, Rais ninayemkubali na kumrank second. Angekuwepo mpaka leo Tanzania ingekuwa emerging economy I am sure.

Mnaomsema vibaya mshindwe ka kulegea. Hamna shukrani. Ni kiongozi ambaye wanaokumbuka, tunamshukuru sana.


mkapa ni stainles steel spoon...haipati kutu ikichafuliwa unaosha ..then twende kazi...kila siku tunatumia na kuichafua lakini inasafishika!!!

wanaompinga mkapa walikuwa na ajenda ya siri ...na walifikiri kazi ya kuongoza nchi ni rahisi...wamegundaa kuwa hafunikiki kwa hila wanaaza kujikomba kwake...tunawajuwa..na kila kitu kinajulikana ....MUNGU ANAMSIMAMIA!!!...hapo ieleweke wazi kuwa mkapa pia si malaika ni mtu ..anayo makosa na alikiri alipoaga...lakini asilani hastahili kusutwa na wajinga wasiojuwa kazi zaidi ya kuongea....ukitaka kumsuta mkapa fanya kazi zaidi yake .....msute kwa kujenga uchumi na miundombinu na maendeleo kwa ujumla .....zaidi ya hapo ni mikingamo isiyokwisha....ukweli utasimama!!...

HONGERA MKAPA ..TUPO NYUMA YAKO WENGI KAMA PISHI LA MCHELE!!!

NAUNGA MKONO HOJA!!
 
Ben Mkapa,

Alimkabidi mkewe mama Mkapa aka first lady funguo za ikulu yetu akawaenzi akina Maro, akutuibia kwa kutumia mifuko ya kiserilikali, akawapa nduguze tender za kiwizi, akajenga majumba ya kifahari kwa kodi zetu.

umenikumbusha ile kampuni ya S.Africa iliyokuwa inaendesha TANESCO ambapo Maro anasadikiwa kuwa Mkurugenzi. E Bana e
 
Alikuwa ana uwezo wa kufikiria na kurusha makombora kwa wapinzani wake kuwa wana wivu wa Kike, Japo Mkapa alikuwa kiongozi mzuri ana mapungufu yake na haya matatizo yote yanamtoa kuwa Kiongozi hodari na kuwa kiongozi mla rushwa na ufisadi, madudu yote
1 Anben, fonisick, Bank M, Meremeta, EPA, Kuuza nyumba za Serikali, na Madudu mengine kibao ndio yanamtoa Mkapa katika ulingo wa Siasa,
Jamani WanaJF, Hivi wakati ule walitoa watu walikuwa wanamsifu Mkapa kuwa Kiongozi safi mara baada ya kutoka haohao wanaanza kusema kuwa alikuwa Mla Rushwa mkubwa?? Najua hata Mzee mzima wa Kaya JK atakapotoka Madarakani watakuja kusema alikuwa mla rushwa kwasababu serikali katika kipindi hicho iliangushwa na ufisadi wa Richmond, Sisi tunataka watoke sasa na sio Kesho. tuache kuwa Wanafiki kiasi hicho katika siasa zetu
 
Tatizo la nchi hii hakuna hata kiongozi mmoja mwenye vision. Hakuna ambaye anawaza kwenye akili yake tunataka kujenga Tanzania ya namna gani! Hakuna kiongozi ambaye anafikiria Nitaifanyia nini nchi yangu!! Wanachofikiria ni nini nitapata katika muda nitakaokuwa madarakani!!

Hivyo kampeni za sasa za kujaribu kufunika mabaya yake zinazofanywa na watawala ni njia ya wao vile vile kufunika mabaya yao ili ionekane ni utaratibu wa kawaida na halali kuiibia nchi wakati ukiwa madarakani!!!
 
Jamani WanaJF, Hivi wakati ule walitoa watu walikuwa wanamsifu Mkapa kuwa Kiongozi safi mara baada ya kutoka haohao wanaanza kusema kuwa alikuwa Mla Rushwa mkubwa?? Najua hata Mzee mzima wa Kaya JK atakapotoka Madarakani watakuja kusema alikuwa mla rushwa kwasababu serikali katika kipindi hicho iliangushwa na ufisadi wa Richmond, Sisi tunataka watoke sasa na sio Kesho. tuache kuwa Wanafiki kiasi hicho katika siasa zetu

If you win a hundred times people will keep showering prise on you. If you loose once the same people will forget they ever know you
 
Wengi wetu tuna mtupia Mkapa lawama nyingi mno,ni kweli amefanya mengi mazuri sana ya kukumbukwa,na amefanya mengi ambayo sasa ndio tunaona hadhari zake.kwangu binafsi naona Mkapa ni rais ambae ametutoa kwenye hali mbaya ya umaskini na kutufikisha hapa tulipo sasa.Mkapa uwezi kumlinganisha na JK.Jamani tusiwe wachoyo wa fadhila,tuangalie ni uhuzo alioufanya mkapa kwenye kipindi chake cha miaka kumi,na tuangalie uhozo uliofanyika kwa kipindi cha miaka 4 ya JK.Hapo ndipo utakapo pata jibu sahihi.
 
Last edited:
Pamoja na matatizo yote ya Mkapa, kuna mtu anaweza kutupa walau mambo 10 tu ambayo rais wetu mpendwa JK amelifanyia taifa hili tunapoelekea kufikisha mwaka wa tano?

Binafsi nasema JK is a failure compared to Mkapa. Hata kina Mpendazoe ambao Phillemon Mikael anawakandia wanatumiwa na JK kumwandama Mkapa ili kuficha mapungufu ya JK.

Nipende au nichukie lakini binafsi sifurahishwi na utendaji wa serikali ya JK ambayo ilikuwa inatafuta namna zote za kumpunguza Magufuli lakini Mungu wa Israel na Mungu wa Yakobo bado anamsimamia mtumishi wake Pombe Magufuli.
 
Wengi wetu tuna mtupia Mkapa lawama nyingi mno,ni kweli amefanya mengi mazuri sana ya kukumbukwa,na amefanya mengi ambayo sasa ndio tunaona hadhari zake.kwangu binafsi naona Mkapa ni rais ambae ametutoa kwenye hali mbaya ya umaskini na kutufikisha hapa tulipo sasa.Mkapa uwezi kumlinganisha na JK.Jamani tusiwe wachoyo wa fadhila,tuangalie ni uhuzo alioufanya mkapa kwenye kipindi chake cha miaka kumi,na tuangalie uhozo uliofanyika kwa kipindi cha miaka 4 ya JK.Hapo ndipo utakapo pata jibu sahihi.
Mkapa alikuwa Hodari na Kiongozi makini hata kuliko mzee mzima wa kaya Jk, huwezi kumfananisha na Jk hata kidogo, kama angekuwa Jk ndio mkapa kipindi kile basi sisi Watanzania tungeelekea KUzimu maana MKapa alikuwa na moyo japo haya madudu yote kwasababu ya mfumo wetu ulikuwa corrupt hasa katiba, lakini Mkapa alikuwa kiongozi mzuri.Labda hii ndio janja ya Mzee mzima wa kaya kwa kufanya watu waseme Ben ni mbaya na kuona yeye ni safi
 
Pamoja na matatizo yote ya Mkapa, kuna mtu anaweza kutupa walau mambo 10 tu ambayo rais wetu mpendwa JK amelifanyia taifa hili tunapoelekea kufikisha mwaka wa tano?

Binafsi nasema JK is a failure compared to Mkapa. Hata kina Mpendazoe ambao Phillemon Mikael anawakandia wanatumiwa na JK kumwandama Mkapa ili kuficha mapungufu ya JK.

Nipende au nichukie lakini binafsi sifurahishwi na utendaji wa serikali ya JK ambayo ilikuwa inatafuta namna zote za kumpunguza Magufuli lakini Mungu wa Israel na Mungu wa Yakobo bado anamsimamia mtumishi wake Pombe Magufuli.


hureee ...well said ..magufuli for presidency 2010!!!... mnajuwa magufuli alikuwa kwa sumaye .na alikuwa awe waziri mkuu wa sumaye...ndio maana alifungwa kweli kweli ...akapewa wizara ya ardhi ambayo ...wanaiita wizara ya kifo...akafurukuta ..., wakaunda wizara maalum ya samaki ...ambayo haina public interest ...akafurukuta...hadi juzi jk imebidi amvulie kofia[jk knows ..if you cannot fight them ..join them...].......
 
Nipende au nichukie lakini binafsi sifurahishwi na utendaji wa serikali ya JK ambayo ilikuwa inatafuta namna zote za kumpunguza Magufuli lakini Mungu wa Israel na Mungu wa Yakobo bado anamsimamia mtumishi wake Pombe Magufuli

Maneno yako karibu yanitoe machozi.Ni kweli kabisa kume kuwepo njama nyingi sana za kujaribu kumuondoa Magufuli kwenye serikali ya JK,Amemuamisha wizara nyingi sana ili afanye vibaya lakini mungu yupo upande wake, na kila wizara anayopelekwa amekuwa anafanya vizuri sana,na ana aminika sana na wanachi kitu ambacho kina mfanya JK kuchindwa kumuondoa.

Juzi tu hapa tumeona matunda ya Magufuli alipoitwa kule Busanda kuongeza nguvu ya uchanguzi,na kama sio yeye kuitwa kule Busanda nina hakika kile kitu CCm wengekuwa wanakisikia tu.
 
.Labda hii ndio janja ya Mzee mzima wa kaya kwa kufanya watu waseme Ben ni mbaya na kuona yeye ni safi

personal intelligence system ya jk ..tangu mwanzo ...ilikuwa na nia ya kuwafanya watu wawe pre occupied kumkandia mkapa muda wote ili wakose muda wa kumchambua yeye ...

na kwa hilo kiasi kafanikiwa...kidogo sasa watu wameanza kuelewa kuwa mkapa pamoja na makosa yake ..lakini he was fa a good leader....which i would say it is an insult to mkapa to compare with jk...time will tell!!..wajanja kuanzia day one jk anakuwa nominated ..tuliwaambia hapa kuwa hili bomu la nuclear...bora salim ,sumaye ,malecela au mwandosya waliogombea naye..he was worst l!!

hatimaye tumemaliza miaka mitano tunapiga umbeya kuhusu mkapa ....kwa kuchezewa akili na system fulani...sasa tunarudi kwa wapiga kura!!
 
personal intelligence system ya jk ..tangu mwanzo ...ilikuwa na nia ya kuwafanya watu wawe pre occupied kumkandia mkapa muda wote ili wakose muda wa kumchambua yeye ...

na kwa hilo kiasi kafanikiwa...kidogo sasa watu wameanza kuelewa kuwa mkapa pamoja na makosa yake ..lakini he was fa a good leader....which i would say it is an insult to mkapa to compare with jk...time will tell!!..wajanja kuanzia day one jk anakuwa nominated ..tuliwaambia hapa kuwa hili bomu la nuclear...bora salim ,sumaye ,malecela au mwandosya waliogombea naye..he was worst l!!

hatimaye tumemaliza miaka mitano tunapiga umbeya kuhusu mkapa ....kwa kuchezewa akili na system fulani...sasa tunarudi kwa wapiga kura!!
Ni kweli kabisa.. maana hata vitu vingine vya kusema kuwa Rushwa wakati yeye alikuapo huko ni kitu kibaya sana. Wanamtandao walikuwa wanavujisha siri nyingi sana za Mkapa na madudu mengine ili yamjenge Mzee Mzima wa Kaya (Jk) wakati mwingine napata shida sana kuona haya mambo na kujua kuwa Jk alikuwa makini?? Tazama hata ile kesi ya Mahalu kama naye alikuwa Waziri alikuwa wapi kushughurikia matatizo hayo??
 
1.Alivunja hosia wa J.K.Nyerere kwa kumpa uwaziri EL.
2. Alijijengea ikulu binafsi huko Lushoto, Tanga.
3. Alijijengea Hotel ya Kitalii huko Lushoto, Tanga.
4. Alizembea na kuruhusu mtandao katika kugombe Urais 2005.

n.k. endelea.............................
 
personal intelligence system ya jk ..tangu mwanzo ...ilikuwa na nia ya kuwafanya watu wawe pre occupied kumkandia mkapa muda wote ili wakose muda wa kumchambua yeye ...

na kwa hilo kiasi kafanikiwa...kidogo sasa watu wameanza kuelewa kuwa mkapa pamoja na makosa yake ..lakini he was fa a good leader....which i would say it is an insult to mkapa to compare with jk...time will tell!!..wajanja kuanzia day one jk anakuwa nominated ..tuliwaambia hapa kuwa hili bomu la nuclear...bora salim ,sumaye ,malecela au mwandosya waliogombea naye..he was worst l!!

hatimaye tumemaliza miaka mitano tunapiga umbeya kuhusu mkapa ....kwa kuchezewa akili na system fulani...sasa tunarudi kwa wapiga kura!!
Kumbe mkuu tupo pamoja sio?

Ebana mi namkubali Magufuli sana, ila sitamani awe rais bali Waziri mkuu... Naamini kutakuwa na changes kubwa sana!

Hivi nyakati za 2005 Magufuli na Pinda walikuwa kambi ipi? Ya JK au ya Salim? Mkuu naamini wewe unaweza kunitoa tongotongo
 
hureee ...well said ..magufuli for presidency 2010!!!... mnajuwa magufuli alikuwa kwa sumaye .na alikuwa awe waziri mkuu wa sumaye...ndio maana alifungwa kweli kweli ...akapewa wizara ya ardhi ambayo ...wanaiita wizara ya kifo...akafurukuta ..., wakaunda wizara maalum ya samaki ...ambayo haina public interest ...akafurukuta...hadi juzi jk imebidi amvulie kofia[jk knows ..if you cannot fight them ..join them...].......
Hahahaha... Mitizamo inapofanana tutashindwa kujadili hoja... Mi ngoja nikae kimya kwa sasa nisije nikapewa kambi ya Salim sasa hivi!
 
Kumbe mkuu tupo pamoja sio?

Ebana mi namkubali Magufuli sana, ila sitamani awe rais bali Waziri mkuu... Naamini kutakuwa na changes kubwa sana!

Hivi nyakati za 2005 Magufuli na Pinda walikuwa kambi ipi? Ya JK au ya Salim? Mkuu naamini wewe unaweza kunitoa tongotongo

Haha Mkuu nadhani wengi sasa tunatambua hilo. Ila inashangaza sana kama wewe ungependa Magufuli awe PM, huenda na wewe ulipata mshituko baada ya kusikia EL ameteuliwa. Yeye mwenyewe alitarajjia kuwa atakuwa PM aliposikia kuwa EL ameteuliwa kuwa PM hakuweza kuvumila na akazirai. Teh teh teh.
Lakini ukweli ni kuwa Pinda ni better kuliko Pombe na EL. NInavyofahamu mimi Pinda na Pombe hawakuonekana sana kwenye kambi hizo, walikuwa low profile sana. Ila for sure tuombe Mungu 2010.
 
Mkapa alifanya kazi kubwa sana katika kila nyanja ya uchumi, jamii, miundombinu n.k.

Pia alirudisha heshima ya elimu na kuweka nidhamu ya kazi. Kipindi chake (awamu ya 3) ndicho kilichokuwa cha mafanikio kuliko kipindi chochote katika historia ya Tanzania. Naweza kusema alikuwa Rais aliefanya mengi, magumu na kwa ufanisi mkubwa, kwa kutumia akili na utaalam kuliko Rais yeyote aliewahi na anaeendelea kuongoza nchi.

Hata mapungufu aliyoyafanya mengi yamefanyika wakati akijiandaa kutoka. Yalifanyika kwa pressure kubwa kutoka kwa waliokuwa wakijiandaa kuingia madarakani. Kama Rais aliekuwa akisubiri kustaafu, hakuweza kuwa na nguvu ya kukinzana na watawala wanaoingia. Ndio maana mengi yalitokea kati ya Oct 2005 na Dec 2005. Japokuwa si sahihi kusema kuwa hana makosa kuruhusu hali hiyo kujitokeza.
 
Back
Top Bottom