Bendera ya Taifa

Mlenge

R I P
Oct 31, 2006
2,125
2,291
Nianze na swali: Hivi unaweza kupeperusha bendera ya taifa mahali uishipo hata ikiwa wewe si kiongozi mtaani?

Nakumbuka wimbo ufuatao tuliimba chekechea, ile iliyoko pale karibu na 'Holofea' kama tulivyozoea kupatamka:

Bendera ya Tanzania,
Ndio ya kujivunia,
Ilianza kupepea,
Mwaka sitini na moja.

Hapo tunashuhudia,
Tunavyojitegemea,
Hapa kwetu Tanzania,
Uhuru umechanua,
Mola wetu Rabuka,
Ijaze yako fanaka!

Mwezi wa kumi na mbili
Saa sita kamili.
Siku ya tarehe tisa
Yalikuwa mambosasa!

Kilele Kilimanjaro
Bendera yatwitwitika
Hapa kwetu Tanzania
Uhuru umechanua
Mola wetu Rabuka
Ijaze yako fanaka!


Ilikuwa ni furaha tele kuimba wimbo huu.

Hivi naweza kuweka pazia lenye rangi za bendera?
Soksi?
Penseli?
Dekio?
Nguo za ndani?
Kilemba?

Naweza kuweka bendera ya taifa kabisa ya ukweli sebuleni? Jikoni? Bafuni? Sitaonekana nadhalilisha bendera?

Watanzania wengi hatujihisi kuwa huru kuitumia bendera ya taifa tupendavyo. Ukiangalia bidhaa zenye bendera za nje, mfano, bendera ya Marekani, utazikuta ni aina nyingi hapa Tanzania kuliko bendera ya Tanzania. Ukikatiza mitaani utakuta 'masela' wanapeperusha bendera ya Marekani kwenye kijiwe chao. Usiombe ukutwe unapeperusha bendera ya taifa, ilhali huna madaraka yoyote ya kiserikali, ni dhana ambayo pengine ni potofu. Hivyo, bendera ya taifa ukiiona inapeperushwa, ujue hiyo ni ofisi ya serikali. Baadhi ya wananchi wanaweza kudhani bendera ya taifa ni kwa ajili ya serikali tu. Wananchi wanaruhusiwa siku mojamoja kujidai nayo, hasa Taifa Stars ikiwa inacheza.

Ili kupunguza sintofahamu, ni vema:

1. Serikali iwe na bendera yake (kama haina bado) tofauti na bendera ya taifa. Ofisi za serikali zipepee bendera ya serikali.
2. Bendera ya taifa isiwe inashushwa saa 12 jioni.
3. Mtu yeyote, popote, iwe ruksa kupeperusha na kuitumia apendavyo, bendera ya taifa.
 
...kuna mada ya uzalendo iliongelea suala hili na uzi wako umetoa mapendekezo mazuri sana na hasa kuwa na bendera ya serikali ili wazalendo wa Tanzania tuifurahie bendera yetu ya taifa.

Majuzi ninaingia wizara ya mambo ya ndani pale ukaguzi, kijana alizuiliwa kuingia ndani ya jengo kisa kavaa jezi ya taifa stars (jersey hii ina rangi zinazopatikana kwenye bendera yetu), afande alikuwa kazini na hakutaka kabisa majadiliano.
Hii si sawa, uzalendo utoke kwenye chama na mapenzi ya mtawala (micro setting) kwenda katika uzalendo wa kweli, Utanzania bila kujali serikali iko chini ya nani
 
Nyuzi zako huwa zimeshiba haswaa. Ndiyo maana unakuta view 4k wakati reply 4.Hongera /Kongole.
====
hii sijaelewa
---

Majuzi ninaingia wizara ya mambo ya ndani pale ukaguzi, kijana alizuiliwa kuingia ndani ya jengo kisa kavaa jezi ya taifa stars (jersey hii ina rangi zinazopatikana kwenye bendera yetu), afande alikuwa kazini na hakutaka kabisa majadiliano.
===
Mimi nilidhani Askari anazuia raia kuvaa nguo/sare ya kiaskari. Hili la jezi ya timu yetu ya Taifa ni jipya, hata hivyo zipo dress codes kwenye ofisi ya Umma. Kuna uwezekano askari alinukuliwa vibaya!
 
Nyuzi zako huwa zimeshiba haswaa. Ndiyo maana unakuta view 4k wakati reply 4.Hongera /Kongole.
====
hii sijaelewa
---

Majuzi ninaingia wizara ya mambo ya ndani pale ukaguzi, kijana alizuiliwa kuingia ndani ya jengo kisa kavaa jezi ya taifa stars (jersey hii ina rangi zinazopatikana kwenye bendera yetu), afande alikuwa kazini na hakutaka kabisa majadiliano.
===
Mimi nilidhani Askari anazuia raia kuvaa nguo/sare ya kiaskari. Hili la jezi ya timu yetu ya Taifa ni jipya, hata hivyo zipo dress codes kwenye ofisi ya Umma. Kuna uwezekano askari alinukuliwa vibaya!

Asante mkuu. Hiyo ya wizarani siyo mimi niliyeiandika.
 
Majuzi ninaingia wizara ya mambo ya ndani pale ukaguzi, kijana alizuiliwa kuingia ndani ya jengo kisa kavaa jezi ya taifa stars (jersey hii ina rangi zinazopatikana kwenye bendera yetu), afande alikuwa kazini na hakutaka kabisa majadiliano.
Mimi nilidhani Askari anazuia raia kuvaa nguo/sare ya kiaskari. Hili la jezi ya timu yetu ya Taifa ni jipya, hata hivyo zipo dress codes kwenye ofisi ya Umma. Kuna uwezekano askari alinukuliwa vibaya!
 
Back
Top Bottom