Bendera ya CCM yachomwa na Wamachinga

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,461
39,928
11w-chinga.jpg
na Godfrey God, Iringa (Tanzania Daima)

KATIKA hatua inayoonyesha kuchoshwa na kunyanyaswa kila mara na vyombo vya dola, kikundi cha wafanyabiashara ndogondogo mjini hapa, jana walishusha bendera kadhaa za Chama Cha mapinduzi (CCM) na kuzichoma moto mbele ya askari polisi.
Mbali ya kuzichoma bendera hizo za CCM, machinga hao walisikika wakipiga kelele wakimtaja Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) Kabwe Zitto, kwa madai kuwa ni mtetezi wa wanyonge na kumwomba aje Iringa kuona uonevui huo.

Machinga hao walichukua hatua hiyo majira ya asubuhi katika eneo la ofisi za CCM mkoa, wakipinga hatua ya uongozi wa Manispaa ya Iringa kuwavunjia vibanda vyao vya biashara.

Inadaiwa kuwa machinga hao ni wanachama wa CCM ambao walikuwa wamepandisha bendera hizo wakati wa ziara ya viongozi wa CCM taifa wakati wa ziara yao mkoani Iringa, waliyoifanya kwa lengo la kuelezea bajeti ya serikali na kukanusha madai ya ufisadi yaliyokuwa yametolewa na ushirika wa vyama vya upinzani dhidi ya viongozi kadhaa wa serikali.

Machinga hao walisema kuwa wameamua kuzichoma moto bendera hizo ili kuonyesha kuwa kuanzia wakati huo wao si wana CCM tena na wapo tayari kujiunga na upinzani kutokana na tabia ya CCM kuwageuka vijana baada ya uchaguzi kwisha.

Machinga hao walisema kuwa wamelazimika kuchoma moto bendera za CCM kutokana na unyanyasaji unaofanywa na viongozi hao wa manispaa.

Alisema yanayofanywa na manispaa hiyo, yanapingana na agizo la Rais Jakaya Kikwete, ambaye mara zote amekuwa akihimiza vijana kujiajiri katika sekta zisizo rasmi kama hizo, ambapo kwa kuwaunga mkono amekuwa akiwapa mikopo.

Walisema biashara hizo wanaziendesha kupitia mikopo kutoka kwa Rais Kikwete na kitendio cha kuvunjiwa mabanda yao wamekihesabu kama njama za kuwatafutia matatizo na serikali, hasa katika urejeshaji wa mikopo hiyo.

Kufuatia machinga hao kufanya fujo hizo kwa kuchoma moto bendera katikati ya barabara, magari yalilazimika kupita njia nyingine ili kukwepa moto huo, ambao ulikuwa umewashwa katikati ya barabara hiyo jirani kabisa na jengo la CCM mkoa na kufanya wanafunzi wanaosoma masomo ya ziada katika jengo la CCM kukatisha masomo na kutoka nje kushuhudia tukio hilo.

Eneo hilo ambalo Manispaa ya Iringa ilianza kuvunja vibanda jana ni lile ambalo viongozi wa vyama vinne vya upinzani wakiongozwa na Zitto walifanyia mkutano wao.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Albano Hokolola, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwa juhudi za kuwasaka waliohusika zinaendelea.

Ofisa Mipango Miji wa Manispaa ya Iringa, Godad Mwakalukwa, alipoulizwa na mwandishi wa habari hizi kuhusiana na zoezi hilo, hakuwa tayari kuzungumzia kwa wakati huo.

My Take:


Sikumbuki wakati wowote ambapo wananchi wamechoma bendera ya CCM au bendera yoyote ile ya chama cha siasa au ya Taifa. Kweli tumefikia hapa? Je, kuchoma bendera wakati Mkutano Mkuu unaendelea ni ujumbe au ni kutukana tu... tena mbele ya Polisi.. ?
 
Ndio CCM inazikwa hivyo wakati bado inajipigapiga. Kama umewahi kuchinja kuku kama mimi nilipokuwa mdogo ukishakata kichwa na kumwachia yule kuku atakuwa anatapatapa na kijipigapiga tu lakini kichwa hakipo tena.
 
Ndio CCM inazikwa hivyo wakati bado inajipigapiga. Kama umewahi kuchinja kuku kama mimi nilipokuwa mdogo ukishakata kichwa na kumwachia yule kuku atakuwa anatapatapa na kijipigapiga tu lakini kichwa hakipo tena.

Duuuh!!! wewe kweli siwezi kukusogelea... maana nikikuudhi tu kidogo unaweza kufanyiza 'kikatili' .... Huyo kuku haitaji kuomba dua tena asipatwe na mwewe, Dua yupo!! lol :)

...hoja;
Wananchi fulani kuchoma bendera (ya chama) ni ishara ya mengi, ila kikubwa kwa mazingira yaliyoongelewa ni dalili za uzembe wa manispaa waliyomo, pia uzembe wao wenyewe...kuchoma bendera ni ishara ya 'kuwa gaidi' lakini siyo ishara ya kuonyesha kuwa unajua haki zako na jinsi ya kuzidai zitekelezwe. Nina uhakika kuna mbinu nyingine wangetumia na kufikisha ujumbe wao bila kuchoma bendera. Na mbinu maradufu ni katika chaguzi, na ni kuhakikisha wameandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, ili siku nyingine wachague wanaowafaa zaidi.

SteveD.
 
11w-chinga.jpg
My Take:[/B]

Sikumbuki wakati wowote ambapo wananchi wamechoma bendera ya CCM au bendera yoyote ile ya chama cha siasa au ya Taifa. Kweli tumefikia hapa? Je, kuchoma bendera wakati Mkutano Mkuu unaendelea ni ujumbe au ni kutukana tu... tena mbele ya Polisi.. ?

This is critical! Mabadiliko huanza kwa watu kupata hasira!
 
Hapana jamani lazima tulitazame swala hili upande wa pili wa shilingi...
Hii ni mbaya sana ktk usalama wa nchi na yaonyesha wazi kuwa tunaenda kubaya.
Kuchoma bendera ya chama wakati swala halihusu chama ni kudharau/kususia mrengo,ilani na sera za chama.
Na kibaya zaidi ni pale wanapotumia jina la Zitto mtu mmoja against CCM hali sio Zitto aliyewaambia mabaya ya chama hiki. I think swala hili ni muhimu tulitazame impact yake hasa yanapofanywa na watu wasiokuwa na mwelekeo ili kuepuka message kama ya Zitto kutafsrika vibaya.
Kitendo cha kuchoma bendera ya CCM ni cha kihuni na ambacho hakiwezi kupokelewa kwa shangwe hata kidogo. NI kuvunja heshima ya chama hata kama baadhi tya viongozi wake (manispaa) wametumia vibaya madaraka yao.
 
Mawazo yaliyotolewa na SteveD na Mkandara kuhusu jambo hili ni ya maana sana.
Hawa wahuni hawajui wanachokifanya, na wala hawapiganii haki zao kwa njia hii. Inafaa waelimishwe njia mahsusi wanazotakiwa kuzitumia, moja wapo ikiwa ni hizo zilizotajwa na SteveD hapo chini.

hatuwezi kufurahia tendo kama hili.
 
Hapana jamani lazima tulitazame swala hili upande wa pili wa shilingi...
Hii ni mbaya sana ktk usalama wa nchi na yaonyesha wazi kuwa tunaenda kubaya.
Kuchoma bendera ya chama wakati swala halihusu chama ni kudharau/kususia mrengo,ilani na sera za chama.
Na kibaya zaidi ni pale wanapotumia jina la Zitto mtu mmoja against CCM hali sio Zitto aliyewaambia mabaya ya chama hiki. I think swala hili ni muhimu tulitazame impact yake hasa yanapofanywa na watu wasiokuwa na mwelekeo ili kuepuka message kama ya Zitto kutafsrika vibaya.
Kitendo cha kuchoma bendera ya CCM ni cha kihuni na ambacho hakiwezi kupokelewa kwa shangwe hata kidogo. NI kuvunja heshima ya chama hata kama baadhi tya viongozi wake (manispaa) wametumia vibaya madaraka yao.

Naungana na wewe kuangalia upande wa pili wa shilingi. Tujiulize mimi na wewe, kwa nini vijana hawa wameamua kuchoma moto bendera ya 'chama chao'?
Kumbuka kuwa wanaofungua matawi haya ya wakereketwa kwa sherehe murua ni viongozi wa vyama, kwa hiyo huenda ndio wanaotoa ahadi hewa kwa hawa wamachinga, kuwa watawapa maeneo ya kufanyia kazi zao, huku wakitelekeza ahadi hio. huenda ndio maana hawa vijana wameamua kuonyesha hasira zao kwa kuchoma moto bendera.
Tusubiri tuone, kuna mengi yaja!
 
swali la msingi, je wananchi katika kuonesha kuudhiwa na chama chochote cha siasa, wanayo haki ya Kikatiba ya kutoa maoni yao kwa kuchoma bendera ya chama, Katiba ya Chama n.k?
 
Hapana jamani lazima tulitazame swala hili upande wa pili wa shilingi...
Hii ni mbaya sana ktk usalama wa nchi na yaonyesha wazi kuwa tunaenda kubaya.
Kuchoma bendera ya chama wakati swala halihusu chama ni kudharau/kususia mrengo,ilani na sera za chama.
Na kibaya zaidi ni pale wanapotumia jina la Zitto mtu mmoja against CCM hali sio Zitto aliyewaambia mabaya ya chama hiki. I think swala hili ni muhimu tulitazame impact yake hasa yanapofanywa na watu wasiokuwa na mwelekeo ili kuepuka message kama ya Zitto kutafsrika vibaya.
Kitendo cha kuchoma bendera ya CCM ni cha kihuni na ambacho hakiwezi kupokelewa kwa shangwe hata kidogo. NI kuvunja heshima ya chama hata kama baadhi tya viongozi wake (manispaa) wametumia vibaya madaraka yao.

only thing i suggest serikali na polisi ni kwamba, let the people do all they want, from protesting to anything LEGAL as long as usalama wa nchi, manispaa, mkoa hautotiwa hatiani, if so in my suggestion they can do anything possible kutuliza hali ili tuwe na amani !

am with you on this !
 
Mawazo yaliyotolewa na SteveD na Mkandara kuhusu jambo hili ni ya maana sana.
Hawa wahuni hawajui wanachokifanya, na wala hawapiganii haki zao kwa njia hii. Inafaa waelimishwe njia mahsusi wanazotakiwa kuzitumia, moja wapo ikiwa ni hizo zilizotajwa na SteveD hapo chini.

hatuwezi kufurahia tendo kama hili
.

lakini mbaya wapinzani wanafurahia pale kuona wananchi wakifanya hivi, huku usalama wa nchi ukiwa mashakani, yaani kama hillary alivyosema, wanacheza "i gotcha kind of game",.

Swali langu moja tu: kama kweli wapinzani are for the people, na kweli wanapenda maslahi ya watanzania, je kuchomwa kwa bendera ya chama chochote cha siasa kunaashiria nini kwao ? inakuwaje inawawia vigumu wapinzani kuwatuliza wananchi pale wanapochoma moto bendera na kufanya fujo iwapo tunelewa fika kwamba fujo huleta mifarakano na sio maendeleo ?

tawi la JF naombeni mnijibu !
 
halafu mbaya ni kwamba, kuna watoto wengi sana hapo wa shule ya msingi na wengine akina dada ambao inaonekana sidhani kama wanajua wanachoprotest, bali hao vijana wawili watatu walioshikiria bendera ndio wakionekana kufanya huo ujinga/fujo !!
 
Naungana na waliosema hao wachoma moto bendera ni wahuni tu na hawawakilishi hisia za wanachama wa chama chochote.
 
Kuchoma bendera ya chama ni alama ya kutangaza uadui... na sidhani kama vijana hawa wako tayari kufanya hivyo kifikra ama kwa vitendo. Akija JK Iringa wao ndio wa kwanza kwenda kusikia hotuba zake kwa hiyo tujaribu kuelewa kuwa hawa vijana wamekosa mwongozo kabisa na hawafahamu nini maana ya bendera.
Binafsi hadi sasa sina matatizo na CCM kwani ilani, sera na katiba yake viko wazi na zinakubalika isipokuwa hawa waumini waongo viongozi -mitume wa Uongo ambao wamekuja badilisha agano.
CCM will always be there na ni chama kilichotukuza wengi kati yetu na katika misingi hiyo hiyo isipokuwa waliobadilika ni baadhi waumini wake.
Nadhani kwa hadhi ya JF inabidi tujiepushe kabisa na ushabiki wa vijana hawa wasojua kitu hata kama walipewa ahadi ni wana CCM -manispaa sasa bendera imehusu nini ktk ahadi hizo.
 
Kuchoma bendera ya chama ni alama ya kutangaza uadui... na sidhani kama vijana hawa wako tayari kufanya hivyo kifikra ama kwa vitendo. Akija JK Iringa wao ndio wa kwanza kwenda kusikia hotuba zake kwa hiyo tujaribu kuelewa kuwa hawa vijana wamekosa mwongozo kabisa na hawafahamu nini maana ya bendera.
Binafsi hadi sasa sina matatizo na CCM kwani ilani, sera na katiba yake viko wazi na zinakubalika isipokuwa hawa waumini waongo viongozi -mitume wa Uongo ambao wamekuja badilisha agano.
CCM will always be there na ni chama kilichotukuza wengi kati yetu na katika misingi hiyo hiyo isipokuwa waliobadilika ni baadhi waumini wake.
Nadhani kwa hadhi ya JF inabidi tujiepushe kabisa na ushabiki wa vijana hawa wasojua kitu hata kama walipewa ahadi ni wana CCM -manispaa sasa bendera imehusu nini ktk ahadi hizo.

wenyewe wanaita vita vya fikra, kwa watu wasiokuwa na mwelekeo (wachoma bendera)! na iwapo wataulizwa kwa nini walichoma bendera sidhani kama watatoa legitimate reason !
 
kuchoma bendera sisuluhu la tatizo lao, bali inaashiria kuchanganyikiwa kwao na maisha wanayopewa na ccm madarakani.

kwa vile watanzania wengi si wasomi na hawajui maana halisi ya vitendo vyao wanavyofanya, hawa vijana tunaweza kusema wamekosa muongozo wa taratibu za kuchukuwa ili tatizo lao kutatuliwa na kuamua kuchukua njia ya mkato bila ya kujua maana halisi ya kitendo chao hicho.
 
wenyewe wanaita vita vya fikra, kwa watu wasiokuwa na mwelekeo (wachoma bendera)! na iwapo wataulizwa kwa nini walichoma bendera sidhani kama watatoa legitimate reason !

vita vya fikra havipiganwi kwa kuchoma bendera, ila kwa kuziunguza na kuziharibu fikra zote mbovu, kwa kuonesha fikra bora zaidi!!
 
Mkandara.
Bendera walinunua wenyewe baada ya kudunduriza fedha zao kwa taabu.
Wangeamua kuzifanya Mashuka wakati wa usiku ingekuwa sawa tu.
Wakiamua kuzifanya leso za kufutia jasho pia ingekuwa sawa tu.
Wakiamua kuzifanya Vilemba ni sawa tu.

Nionavyo mimi hata kushona chupi ya bendera ya SISIEMU ni sawa tu, si ndo mapenzi yenyewe kwa chama?

Lakini MMm! Chupi ya kijani?!

Sijui sheria inasema nini juu ya kugeuza bendera ya chama shuka,leso au kilemba. Kuichoma je?

Hawa Wamachinga wamechoma Bendera wakiwa wanachama wa SISIEMU wenye nia na madhumuni ya kujiunga na upinzani.
Hawajachoma Bendera kama wapinzani taarifa iko wazi.

Mkandara unasema kuchoma Bendera ni kutangaza uadui?

Mimi nadhani si kweli. Kuchoma Bendera ya SISIEMU ni majibu ya wanachama wa SISIEMU juu ya uadui uliotangazwa na chama chao wenyewe.Bendera imechomwa kama ishara ya Fukuto lililozidi ndani ya nyumba.
Bendera kuchomwa ni matokeo ya Siasa zao za kuwafanya watu wajinga kwa kuwapa ahadi hewa, zenye kuvunja sheria kwa makusudi na zisizo tekelezeka.

Mimi nadhani kumwahidi Mmachinga kwamba akijiunga na SISIEMU, SISIEMU itamlinda yeye na kibanda chake lakini mara uchaguzi ukiisha ahadi zinayeyuka na kibanda chake kubomolewa ndiyo kutangaza uadui.

Acha Bendera kuchomwa, kuna siku hata ofisi zitachomwa moto kibaya zaid Polisi, FFU na mgambo watashiriki.

Watu wamechoka.
 
Gaijin na Madela-wa-Madilu wameongelea kitu muhimu sana - frustration. Kama hawa vijana wangekuwa na uwezo wa kuja hapa Jambo Forums wangetoa msongamano wa mawazo yao hapa na kutoa hoja zao. Lakini tujiulize hawa vijana ambao wana elimu duni, wana nafasi gani ya kutoa hoja zao. Wanafukuzwa kila kukicha, wananyanyasika na vyombo vya dola, na wanaona kama wamesalitiwa. sasa basi, mnafikiri ni njia gani iliyopo kwa wao kuonyesha hasira yao? Kuunguza bendera kwao ni njia moja kali ya kuonyesha hasira yao. Badala ya kuwaadhibu vikali ni lazima serikali ijaribu kuelewa kwamba wananchi lazima wapewe elimu na uwezo wa kutoa mawazo yao. Lakini pia ni lazima wananchi waone kwamba wana haki ya kubadili hali zao. Hivi sasa wao wanaamini they are helpless. Sidhani kama tunaweza kuwalaumu bali tunahitaji kutafakari. Hawajamwua mtu, hawajaharibu mali ya mtu (bendera zile ni mali zao), it's a form of expression.
 
Madela, kuna kaukweli fulani katika maneno yako. Ila nadhani wengi tumezoea kuona picha ya kuchomwa bendera ya Marekani na Israeli kwa sababu ya mgogoro wa Wapalestina. Sasa sijui kama mgogoro ndani ya CCM au nchini umefikia kiwango cha hiyo ya waarabu na Wamarekani.. tusipoangalia mtaona watu wanachoma bendera ya Tanzania... (ingawa kwenye hili sheria iko wazi kabisa).
 
Susuviri na MKJJ

Mtafaruku wowote uanzishwao na serikali, wenye matokeo ya kudhoofisha na kuua vyanzo vya uchumi wa wananchi wanyonge, ni mtafaruku ambao siku zote huwa chanzo cha kuiangusha serikali.

Watu wa mataifa mengi Duniani huchoma bendera kama ishara ya mwisho kabisa ya kuchoshwa na kero huku wakipeleka ujumbe usemao wako tayari kwa mapambano.

Vita ya kati ya serikali na wananchi siku zote apataye kisago ni mwananchi na aibukaye mshindi ni wananchi vile vile.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom