Bend it like Beckham!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Ni nani anapaswa kumwajibisha Kiongozi wa Serikali anayevunja sheria au kupuuzia sheria?

Sisi kama wananchi na Taifa, inakuwaje tunasulubiwa kwa Sheria na ukali tunapofanya makosa ya kupuuza, kuvunja au kupinda sheria?

Kwa nini viongozi wetu wanapenda kupinda ukweli na kutoa maelezo ya uongo bila woga huku wakijua wanavunja sheria?

Kwenye suala la Makontena TICTS na Karamagi, sheria na kanuni zilipindishwa na kuvunjwa, lakini hakuna aliyechukuliwa hatua.

Ukaguzi wa mahesabu wa CAD unaonyesha ukosefu mkubwa wa kufuata kanuni na sheria za kazi na kimahesabu, hakuna anayewajibishwa.

Pesa za BOT kufujwa, hakuna anayewajibishwa.

Mikataba mibovu, hakuna anayewajibishwa.

Hata hili la kuwekeana hirizi au unga wa sumu, ukweli umepindishwa wananchi tunadanganywa kuwa hakuna ushahidi na kilichotokea ni uzushi.

Ni mpaka lini viongozi na watawala wetu wataendelea kupindisha mambo na kudiriki kuvunja sheria bila woga?

Kila wakipindisha jambo na kupiga banana chop, goli twafungwa, je tufanye nini?
 
Ni nani anapaswa kumwajibisha Kiongozi wa Serikali anayevunja sheria au kupuuzia sheria?

Sisi kama wananchi na Taifa, inakuwaje tunasulubiwa kwa Sheria na ukali tunapofanya makosa ya kupuuza, kuvunja au kupinda sheria?

Kwa nini viongozi wetu wanapenda kupinda ukweli na kutoa maelezo ya uongo bila woga huku wakijua wanavunja sheria?

Kwenye suala la Makontena TICTS na Karamagi, sheria na kanuni zilipindishwa na kuvunjwa, lakini hakuna aliyechukuliwa hatua.

Ukaguzi wa mahesabu wa CAD unaonyesha ukosefu mkubwa wa kufuata kanuni na sheria za kazi na kimahesabu, hakuna anayewajibishwa.

Pesa za BOT kufujwa, hakuna anayewajibishwa.

Mikataba mibovu, hakuna anayewajibishwa.

Hata hili la kuwekeana hirizi au unga wa sumu, ukweli umepindishwa wananchi tunadanganywa kuwa hakuna ushahidi na kilichotokea ni uzushi.

Ni mpaka lini viongozi na watawala wetu wataendelea kupindisha mambo na kudiriki kuvunja sheria bila woga?

Kila wakipindisha jambo na kupiga banana chop, goli twafungwa, je tufanye nini?

Tusiwachague viongozi wa namna hiyo.....
 
Kila wakipindisha jambo na kupiga banana chop, goli twafungwa, je tufanye nini?

Kuna haja ya kurudi kwenye sheria zetu kuangalia kama kuna mahala tunaweza kuwashitaki kwa makosa wanayoyafanya makusudi.

Lakini wengine hata baada ya kustaafu tuangalie kama wanaweza kuingia jela hata wakiwa wazee.
 
Tayari tumewachagua na inawezekana usiwachague lakini wakajichagua.

Kumbuka Tanzania ni wachache wanaoshinda kihalali. Si unakumbuka na Kabuye aliyekuwa mbunge wa TLP alishawai kusema hili?

Sasa kama ni hivyo basi tukubali tu kwamba ndivyo tulivyo na maisha yaendelee...unakubali?
 
Inaweza onekana kama haitawezekana ila najua it is just a matter of time even a fool has his own day!
 
Mkuu Kitila

Kwa sasa kunaweza kukawa na kubadilika, tutegemee mabadiliko makubwa baada ya sakata zima la ufisadi mwananchi wa kawaida amepigika na wataendelea kupigika, sasa hivi wanatafuta kulikoni tukawa hivi?

Nafikiri wapinzani wanatakiwa kuongeza nguvu hata sisi wananchi wa kawaida tunatakiwa kuongeza nguvu.

Hila kuna kitu kimoja kinachotakiwa kifanyike kuhusu hili suala zima la ufisadi nalo ni kuitisha maandamano ya amani kuiambia serikali ifuate sheria waliofanya makosa wafikishwe katika vyombo vya sheria.

Vinginevyo hakuna haja ya kuwa na sheria, hakuna haja ya kulipa kodi, hakuna haja hata ya kufanya kazi, hakuna haja ya kuwa na viongozi, hakuna haja ya kuishi ............................
 
Kuna haja ya kurudi kwenye sheria zetu kuangalia kama kuna mahala tunaweza kuwashitaki kwa makosa wanayoyafanya makusudi.

Lakini wengine hata baada ya kustaafu tuangalie kama wanaweza kuingia jela hata wakiwa wazee.


Kuwashitaki?! Wamejilinda kweli kweli. Sheria ya mwendesha mashitaka wa binafsi ni ngumu kuitekeleza. Kuna watu walitaka kutumia sheria hiyo kumshitaki yulkembunge wa Buchosa, mpaka leo bado wanahangaika kupata ruhusa ya kumshitaki chini ya utaratibu huo na anakaribia kumaliza ubunge wake.
Wenyewe wana uhakika hakuna mtanza wa kawaida ambaye anaweza kufanikiwa kuwafungulia mashitaka kwa utaratibu huo na ndio maana hata akina rostam wameanza kututukana kwamba mwenye ushahidi akashitaki, anasema hivyo kwa sababu anajua kwua haitawezekana. Vyombo mahsusi vya kuwafungulia mashitaka vyote ni vyao
 
Sasa kama ni hivyo basi tukubali tu kwamba ndivyo tulivyo na maisha yaendelee...unakubali?


2010 nitachagua bila kinyongo mahali pa kuiweka Tanzania. Kama kuwa kwenye kundi la wananchi wenye IQ below 70 au kundi la nchi zenye wanaume na wanawake wenye akili timamu. Mpaka sasa hivi kwa mtu mweye akili timamu inaonekana kabisa kuwa serikali ni kama kundi la ajabu. Na hata watu wenye heshima zao naona sasa hivi wanaona hata aibu kuwa associated na serikali ya sasa. Much better kuwa nje ya seriklai this time than ever, dignity yako inaweza kuwa eroded vibaya sana.
sasa kama 2010 watu watakubali kuhongwa tena T-shirts, kanga, Kofia, Pilau na ahadi zamuongo na kweli. Then tukubali tu kuwa ndivyo tulivyo.
 
Ni wazi kabisa kuwa tunazo sheria nzuri tu lakini ukweli ni kwamba tusitegemee CCM wanaweza kuchukuliana hatua kali au kufungana wenyewe wakati wanapozivunja,watafunga wengine lakini siyo wao!.Nguzo kuu ndani ya CCM ni kulindana kwa hiyo tusitegemee mabadiliko yoyote kwa hilo.
Naona itabidi tutumie Ukraine staili kudai haki zetu.....

-Wembe
 
Je kama wananchi tunafanya nini kuhakikisha kuwa sisi binafsi tunafuata Sheria?

Najua binadamu si kamili, lakini ikiwa tunapiga kelele kulaumu wavunja Sheria na sisi wenyewe ni mstari wa mbele kupindisha Sheria hata za hapa JF, tunategemea nini kutoka kwa hao tunaowataka wafuate Sheria (CCM na Serikali)?
 
Hivyo ni mkao wa Dereva Kombo, abiria shikilia roho yako?

Mchungaji,
Sikujua kwamba unaweza kumbuka ya Dereva Kombo maana ulikuwa kijana mdogo enzi hizo! Ndiko tunakoelekea. Imenikumbusha joke moja niliyoisikia juu ya "Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya......". Alikuwepo dreva wa bus moja maarufu la safari za DAR-MOMBASA. Dreva wa bus hilo alipofika Mombasa akapata homa kali hakuweza kuendesha gari kurudi DAR. Ikabidi bus hilo akabidhiwe driver mwingine mkazi wa Mombasa ambaye alikuwa hajawahi kufika Dar es Salaam. Katika kutahadharishwa akaambiwa kwamba ukifika sehemu za Wami aendeshe taratibu kwa sababu barabara inatereza sana ni rahisi kupata ajali. Dreva huyo alipoushika usukani akaendesha gari kwa kasi isiyo ya kawaida. Abiria wakawa wameshikilia viti kwa hofu ya kutokea ajali. Wakamsihi Dreva apunguze mwendo lakini hakutaka kuwasikiliza. Hata alipofika Wami hakujua kwamba kafika eneo hatari, speed ikawa ni ile ile kali kupita kiasi. Alipofika Chalinze akafunga brake na kuwauliza abiria, Je Wami bado hatujafika tu? Wakamwambia tumeishapita?!
 
Back
Top Bottom