Ben Saanane na watu wake kumfanyia tafrija ya kuzaliwa Malisa ilhali Mhere Mwita yu taaban ni mzaha

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Binafsi huwa nashangazwa sana na hawa vijana wa BAVICHA. Wakati mwingine ninadhani kuwa wanachokifanya ama ni maigizo au wana matatizo ya malezi kwenye chama chao.

Twende taratibu.
Jumatatu Oktoba 3, 2016, Mwenyekiti wa BAVICHA wilaya ya Geita Mhere Mwita, alipata ajali Mjini Dodoma alipoenda kushuhudia hukumu ya Viongozi wa BAVICHA Taifa walioshtakiwa kwa makosa ya Uchochezi, kesi ambayo viongozi hao walishinda baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha madai hayo. Haijaelezwa mazingira ya ajali hiyo. Haijaelezwa pia kama ni ya pikipiki ama ya gari. Haijaelezwa pia wengine waliohusika kwenye ajali hiyo. Inatia mashaka.

Baada ya kuumia, viongozi wa BAVICHA walimkimbiza kwenye Hospitali ya Mkoa wa Dodoma ambako alipata matibabu ya awali. Hata hivyo, taarifa kutoka kwa mmoja wa viongozi wa BAVICHA ambaye napenda kuchukua fursa hii kumpongeza kwa jinsi anavyonipa ushirikiano juu ya kambi yao, alisema kuwa Hospitali ya Dodoma iliamua kumpa rufaa Mhere Mwita ya kutibiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kitengo cha Mifupa (MOI). Hii ni baada ya tatizo la Mhere Mwita kuwa kubwa kiasi cha Hospitali ya Dodoma kushindwa kulishughulikia kwani alivunjika kwenye maungio ya paja na kiuno ya mguu wa kushoto.

Kutokana na rufaa hiyo, Mhere Mwita alisafirishwa kutoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam na aliwasili Muhimbili (MOI) majira ya saa 12 jioni ya tarehe 4 Oktoba 2016. Logistics za kumpokea Mhere MOI zilikamilika majira ya saa nane usiku wa tarehe 5 Oktoba 2016.
image.jpg

Hata hivyo, cha kushangaza ni kwamba, Makamanda wote ambao walikuwa wanamhudumia Mhere Mwita siku hiyo walielekwa sehemu maalum ambayo iliandaliwa kwa ajili ya kujipongeza. haijaelezwa ni pongezi za aina gani ijapokuwa walizificha kwenye mgongo wa sherehe ya kuzaliwa kwa Malisa Godlisten. Makamanda hao walikunywa vinywaji vikali huku wakifurahi, kuimba na kusherehekea kana kwamba hakuna tatizo kubwa lililomkumba mmoja wa wanafamilia. Ni sherehe, chereko, nderemo na burudani ya kila aina.
image.jpg
image.jpg

Kinachonishangaza zaidi ni dhihaka wanayoendelea kuifanya kwa Mhere Mwita baada ya kupata ajali hiyo. Haikatazwi watu kumtembelea mgonjwa na kupiga naye picha. Ila kwa kweli si fair kabisa. Wakati huu walipaswa kuwa watulivu na kuendelea kumuombea mwenzao ili apone haraka. Kuendelea kufanya dhihaka mbele ya mgonjwa kwa kupiga Selfie na kukenua meno hakika ni jambo la kusikitisha.
image.jpg
image.jpg
image.jpg

Niwaombe tu ndugu zangu wa BAVICHA. Wakati mwingine muwe mnafanya mambo ya kiutu uzima. Muwe mnakuwa basi japo kwa sekunde moja.
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    69.7 KB · Views: 90
unawaonea wivu makamanda wa ukawa kwa jinsi walivyojipanga mbali na siasa wako na miladi yao ya kuwaingizia pesa mf Yericko yuko na biashara zake sio wewe unakaa lumumba nje kwenye bench la wauza vifaa vya ccm na ukimuona Makamba unakimbilia shikamo mzee na wakati wewe ni babu



swissme
 
Nashangaa kumuona kamanda akisherehekea sikuu ya kuzaliwa....

BAVICHA wamechukua unafiki wa Mbowe.
Nakubaliana na wewe Mkuu. Kinochoshangaza ni kwamba wameenda kusherehekea usiku wa manane. Huu ni utoto wa hali ya juu
 
Hao akina Mhere Mwita kutoka Tarime, ngoja atumike....hao wanaokula bata ndio warithi halisi wa chadema....wanatokea kule kilipozaliwa.
Kweli aiseeee! Ukiangalia walioenda kula bata ni wakuleeee kwenye chama. Yeriko Nyerere, Ben Saanane, Malisa GJ, Hilda Newton, nk
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Binafsi huwa nashangazwa sana na hawa vijana wa BAVICHA. Wakati mwingine ninadhani kuwa wanachokifanya ama ni maigizo au wana matatizo ya malezi kwenye chama chao.

Twende taratibu.
Jumatatu Oktoba 3, 2016, Mwenyekiti wa BAVICHA wilaya ya Geita Mhere Mwita, alipata ajali Mjini Dodoma alipoenda kushuhudia hukumu ya Viongozi wa BAVICHA Taifa walioshtakiwa kwa makosa ya Uchochezi, kesi ambayo viongozi hao walishinda baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha madai hayo. Haijaelezwa mazingira ya ajali hiyo. Haijaelezwa pia kama ni ya pikipiki ama ya gari. Haijaelezwa pia wengine waliohusika kwenye ajali hiyo. Inatia mashaka.

Baada ya kuumia, viongozi wa BAVICHA walimkimbiza kwenye Hospitali ya Mkoa wa Dodoma ambako alipata matibabu ya awali. Hata hivyo, taarifa kutoka kwa mmoja wa viongozi wa BAVICHA ambaye napenda kuchukua fursa hii kumpongeza kwa jinsi anavyonipa ushirikiano juu ya kambi yao, alisema kuwa Hospitali ya Dodoma iliamua kumpa rufaa Mhere Mwita ya kutibiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kitengo cha Mifupa (MOI). Hii ni baada ya tatizo la Mhere Mwita kuwa kubwa kiasi cha Hospitali ya Dodoma kushindwa kulishughulikia kwani alivunjika kwenye maungio ya paja na kiuno ya mguu wa kushoto.

Kutokana na rufaa hiyo, Mhere Mwita alisafirishwa kutoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam na aliwasili Muhimbili (MOI) majira ya saa 12 jioni ya tarehe 4 Oktoba 2016. Logistics za kumpokea Mhere MOI zilikamilika majira ya saa nane usiku wa tarehe 5 Oktoba 2016.
View attachment 413940
Hata hivyo, cha kushangaza ni kwamba, Makamanda wote ambao walikuwa wanamhudumia Mhere Mwita siku hiyo walielekwa sehemu maalum ambayo iliandaliwa kwa ajili ya kujipongeza. haijaelezwa ni pongezi za aina gani ijapokuwa walizificha kwenye mgongo wa sherehe ya kuzaliwa kwa Malisa Godlisten. Makamanda hao walikunywa vinywaji vikali huku wakifurahi, kuimba na kusherehekea kana kwamba hakuna tatizo kubwa lililomkumba mmoja wa wanafamilia. Ni sherehe, chereko, nderemo na burudani ya kila aina.
View attachment 413942 View attachment 413944
Kinachonishangaza zaidi ni dhihaka wanayoendelea kuifanya kwa Mhere Mwita baada ya kupata ajali hiyo. Haikatazwi watu kumtembelea mgonjwa na kupiga naye picha. Ila kwa kweli si fair kabisa. Wakati huu walipaswa kuwa watulivu na kuendelea kumuombea mwenzao ili apone haraka. Kuendelea kufanya dhihaka mbele ya mgonjwa kwa kupiga Selfie na kukenua meno hakika ni jambo la kusikitisha.
View attachment 413948 View attachment 413949 View attachment 413950
Niwaombe tu ndugu zangu wa BAVICHA. Wakati mwingine muwe mnafanya mambo ya kiutu uzima. Muwe mnakuwa basi japo kwa sekunde moja.
Ama kweli Mbwa akikaribia kufa hupoteza uwezo wa kunusa!!

Yaani siku hizi mmeishiwa hoja dhidi ya CHADEMA mpaka mnaanzisha thread za kichoko kiasi hiki?

Mnatia kinyaa sana!!
 
Eti kamanda kamanda anasherekea siku ya kuzaliwa!!!!!......wakiume sampuli ya Martin kadinda
Hiyo haikuwa sherehe ya kuzaliwa bali sherehe hiyo ilitumika kama kiini macho. Wapo wanaosema kuwa sherehe hiyo ilikuwa ni kuwapongeza viongozi wa BAVICHA Taifa kwa kushinda kesi
 
Ama kweli Mbwa akikaribia kufa hupoteza uwezo wa kunusa!!

Yaani siku hizi mmeishiwa hoja dhidi ya CHADEMA mpaka mnaanzisha thread za kichoko kiasi hiki?

Mnatia kinyaa sana!!
Pole sana Mkuu. Punguza jazba. Huu mchezo hauhitaji hasira
 
Chadema chama cha mapicha picha....'makamanda' wamevaa gloves kuigiza.....huyu Mwita akipona atajifunza lakini kama naye wamemfanya 'msukule' watamtumie baadaye wata-Mu Wangwe'
Hakika Mkuu. Akitoka hospitali akili yake aiweke sawa
 
Back
Top Bottom