Tetesi: Ben Saanane kuna biashara gani unafanya na ubalozi wa Sahara Magharibi na Kundi la TASSC?

Wanabodi
Habari za jumapili!?

Nimepita ktk ukurasa wa facebook wa Ben saa nane na kukuta ameanza kutoa majibu kwa wale waliomtuhumu.
----------------------------------------

"Ben Saanane Unafanya biashara gani na Ubalozi wa Sahara Magharibi"?

Nitatoa Ufafanuzi wa baadhi ya tuhuma ambazo zimesambazwa tangu wiki iliyopita kwenye mitandao na baadhi ya vyombo vya habari .Tuhuma nyingine binafsi sitazijibu hasa zile za kipuuzi. Zile tuhuma za yule anayeleta masuala ya kutooa sitazijibu.Sina muda wa kumjibu mbunge ambae anadhani kumchafua Ben Saanane (kwa sababu ya hasira zake fulani tu) atatibu changamoto zake kisaikolojia kwenye matatizo yake binafsi.Huyu bidada ni wa kuombea!Asitutoe kwenye mstari kwa sababu ya hasira zake binafsi za muda mrefu.

Wale wengine wa upande wetu,Nimewaacha baada ya kupata ushauri sana wa watu ninaowaheshimu.Watakapoendelea sitasita kwenda kinyume na ushauri wao.

Kuna tuhuma iliyozushwa kuanzia JamiiForums yenye kichwa cha habari "Ben Saanane Unafanya biashara gani na ubalozi wa Sahara Magharibi'?
Kisha watoa tuhuma wakaendelea kujenga hoja kuwa kuna fedha zaidi ya Shilingi milioni 12 ziliingizwa kwenye akauntii namba 01J1093293000. Na kwamba kiasi hicho cha fedha kililenga kutumika kulipa watu wanaodaiwa kuwa walitaka kuvuruga ziara ya mfalme Mohammed wa VI wa Morroco na pia kuuuhusisha ubalozi wa Algeria nchini na Kamati ya umoja wa Tanzania na Sahara Magharibi(TASSC).
Wasambaza tuhuma kwenye Mitandao na pia kwenye gazeti la serikali la Habari Leo waliendelea kulalama na kufanya jaribio la kupandikiza hisia kuwa wale waliokuwa wanakosoa ziara ya mfalme wa Morroco ni wasaliti wa nchi na wahujumu wa Uchumi .
Kwamba "Kuishambulia" serikali iliyonisomesha bure ni usaliti na hivyo napaswa kulipa gharama zilizotumika wakati wenzangu waliorudi nchini wanafanya kazi serikalini
Majibu yangu:

i)Sifanyi biashara yoyote na Ubalozi wa Sahara Magharibi

ii) Sina mkakataba wowote na ubalozi wa Sahara Magharibi.

Nina mkataba wa kufanya Consultancy na Balozi mbili za kigeni nchini na Taasisi nyingine mbili za kimataifa tangu mwezi uliopita kuhusiana na masuala ya kisiasa,kijamii,na Kiuchumi nchini sambamba na tathmini ya mwenendo wa haki za binadamu.
Maadili ya kazi yangu na hata Mkataba husika hauniruhusu kuzitaja balozi hizo .Ni suala la professionalism na uadilifu tu.

Ubalozi wa Sahara Magharibi sio miongoni mwa balozi hizo.Vyombo vinavyojiita vya dola kama vina ushahidi wa tuhuma zilizotolewa basi si vichukue hatua?
Balozi zote nchini na Mwenendo wa Mabalozi na maofisa wake huongozwa na mkataba Vienna na ni sehemu ya sheria za kimataifa. Tusichafue balozi na mataifa mengine kwa sababu tu kuna watu fulani wamezidiwa hoja na kuzua propaganda chafu.

iii) Kusomeshwa bure na serikali haimaanishi kuwa nilisaini mkataba wa kunilazimisha kufanya kazi na serikali nirudipo nchini bali kulijenga Taifa langu.Kufanya kazi nje ya serikali na nikaweza kuikosoa na kushauri ni sehemu ya ujenzi wa Taifa na wala silazimishwi kuipenda serikali ya chama cha Mapinduzi.Wapo watu ni watumishi serikalini lakini wanatuletea taarifa na madudu yanayofanyika huko.Vipi hao nao si wanaijenga nchi kwa staili yao? Hasira za nini?

iv) Kijana Noel Shao ambaye ni Afisa Mahusiano wa Kamati ya Umoja wa Watanzania na wapigania uhuru wa Sahara Magharibi baada ya kufanya mkutano na waandishi wa Habari pale Landmark Hotel,wakakosoa na kulaani ziara ile ya mfalme Mohammed.Baadae aliitwa Polisi na kushikiliwa kwa masaa kadhaa na kuhojiwa.Maswali aliyokuwa anahojiwa ni ya kufedhehesha na mengine yakimlazimisha kukiri kuwa wanatumiwa na vyama vya siasa

v)Tuhuma hizi za fedha ni mkakati maalumu wa kutaka kupandikiza mgawanyiko kwa wale wanaoungana kusimamia Doctrine ya Taifa letu kimataifa katika haki na uhuru wa kujitawala"Right to Self-Determination" ambayo mwalimu Nyerere amekuwa akihubiri kwa muda mrefu.
Lengo ionekane watu wanafanya hivi kwa maslahi yao wenyewe ili wengine warudi nyuma.Wameshindwa kujibu hoja za msingi wanaishia kuokoteza hoja na vioja vya kugawa watu na kuwatoa kwenye mstari .
Tanzania kuweka kisingizio cha Diplomasia ya uchumi kukiuka misingi inayokiuka misimamo yetu kwenye haki za binadamu haikubaliki na tutaikosoa hata kama Rais Magufuli(kwa uelewa wake finyu) kwenye maswala ya diplomasia ataendelea kujitetea kwa kauli za ajabu eti "Paka ni Paka ilimradi akamate panya".

Mwalimu Nyerere hakuwahi kuwa na mtazamo juu ya Makaburu kuwa 'Paka ni paka ilimradi akamate Panya".
Kipindi cha kupambana na makaburu aliwahi kujutia kuruhusu kampuni la De beers kufanya biashara ya almasi kule mwadui wakati ilikuwa imezuiwa.Ni kwa sababu ndilo lililokuwa na monopoly ya biashara ya almasi.
Pamoja na kuwa Nyerere alikuwa mwanamajumui(Pan-Africanist) lakini aliwatetea watu wa BIAFRA waliotaka kujitenga kule Nigeria kwa sababu walikuwa wakibaguliwa kama Wayahudi enzi za Hitler na chama chake cha NAZI.Pamoja na kuwa mkutano wa umoja wa Afrika(OAU) uliofanyika Misri kuwa na lengo la kumsulubisha aliwatuma akina Kawawa akaendelea kuwa na msimamo wake ndio maana hata wakati wa Vita na Idd Amin kwa hasira mtawala wa kijeshi wa Nigeria wakati huo Jenerali Olusegun Obasanjo alitoka nje ya Kikako cha OAU baada ya Nyerere kuanza kuongea.Hakutetereka.
Mwaka 1964 kwa sababu ya doctrine yetu ya kupinga Ukoloni na ukandamizaji,Rais Kwame Nkrumah aliwahi kumshambulia kwa maneno makali Nyerere kwenye mkutano wa Umoja wa Afrika baada ya Tanzania kuchaguliwa kuwa Makao makuu ya kamati ya ukombozi ya Afrika
Nyerere alijibu kuwa yupo tayari makao hayo makuu yahamie Accra Ghana. Miaka 2 baadae Kwame Nkrumah mwenyewe alishindwa kujikomboa alipokabiliwa na uasi na kupinduliwa mwaka 1966.

Propaganda inayofanywa na Rais Magufuli,Serikali na vyombo vyake kuwa kuna nchi tulizowahi kuzisaidia lakini hazitusaidii ni propaganda ya ovyo kabisa na inayochekesha.

Baada ya Nelson Mandela kutoka Gerezani na kuwa Rais Mwaka 1994 huku Tanzania Rais Mkapa aliingia madarakani mwaka 1995 na sera yake ya ubinafsishaji.

Yeye na serikali yake walipigia chapuo kuuzwa kwa makamouni na hata mabenki kama NBC iliyouzwa kwa bei ya kutupwa .Hivi tunataka kuilaumu Afrika Kusini wakati Mkapa ndiye alikuwa kinara wa kupiga chapuo?

Hatuwezi kuacha kusimamia Principle zetu kimataifa kwa visingizio vya ajabu ajabu.Nyerere alisimama kidete hadi Umoja wa nchi huru wa Afrika ukaingiza kwenye mkataba wake azimio la haki za watu na binadamu mwaka 1981.

Fedha za Mfalme Mohammed VI wa Morroco ni fedha za damu.Ni fedha zitokanazo na machozi,jasho na damu za watu wa Sahara wanaoteswa na utawala ule wa kifedhuli kinyume na azimio namba 1514(1960) la umoja wa Mataifa juu ya kukomesha ukoloni.Fedha hizi haramu hazina tofauti na fedha za wauza madawa ya kulevya,Human trafficking,Ujangili na fedha zipatikanazo kwa uharamia.
Morroco imekalia na kuitawala Sahara Magharibi na kunyonya raslimali za nchi ile kisha tunaletewa na kujitapa "Paka ni Paka ilimradi anakamata panya".

Ni sawa na wauaji wa watu wetu wenye ulemavu wa ngozi kukata viungo au hata kuuwa kabisa kisha baada ya hapo wanaingia baa na kujitapa kuwa ilimradi ni fedha hatujali kwa sababu "Paka ni Paka Ilimradi anakamata panya"

Hazina tofauti na wale dada poa wanaojiuza halafu baadae wanajitapa na fedha ni fedha.

Bahati nzuri nae aliwatia aibu maana alivyopokelewa kwa heshima na mizinga 21 ya kijeshi,Red Carpet na Dhifa ya kitaifa kesho yake akaonekana anatangaza Mmea wa bangi na kuwa balozi wake nchini Zanzibar bila kuzingatia Sheria na tamaduni za watu wa zanzibar huku akiwa amekumbatia vimwana.Si mnasema Paka ni Paka ilimradi akamate Panya?

Visingizio kwamba mbona Zanzibar inanyonywa havihalalishi hili la Nchi moja kuikalia kimabavu bila hati yoyote ya kuungana (hata ya kimagumashi kati ya Tanganyika na Zanzibar)

Halafu tunaomba Sala ya Taifa eti "Mungu Ibariki Tanzania...."

Hakuna Mungu wa Unafiki na kuendekeza ufedhuli.

[HASHTAG]#MagufulihakikiPhDyako[/HASHTAG]
[HASHTAG]#MagufuliverifyyourPhD[/HASHTAG]
[HASHTAG]#Freewesternsahara[/HASHTAG]

Aluta continua,Victory Ascerta...
Ben Saanane
Lile swali kuhusu ile .mu.su. uliyokuwa umepewa ili umshughulikie Zito hivi umelijibuje kamanda. Ni hilo tuuu.
 
Mbona Ben sijaona halipojibu Hoja zile zaidi ya mipasho tu.. Zaidi ya kutafuta Kiki fake za ujasiri wa kukosoa upande ambao hayupo.. Ninaamin Ben anayaona kwa ukaribu zaidi mambo yanayo tokea Chadema kuliko yaliyopo ndani ya serikali.. Nilitegemea hawe mkosoaji mzuri sana ndani ya Chadema na kwa Mbowe kabla ya kutafuta Kiki huku nje..

Kama kweli anataka kubadili Tanzania, anatakiwa kuanzia nyumbani.. Chadema iwe safi.. Watu wawe safi.. Tuhamie nje huku.. Tutashirikiana kwa pamoja.. Sio tubague..


[HASHTAG]#ben saanane[/HASHTAG] na ujasiri fake

Yapi hayo yanayotokea CHADEMA? Si uyaseme na kwa uzuri anzisha uzi wake, utajibiwa tu!

Lakini ulichokifanya hapa ni sawa na kuchanganya nyama na mlenda na kuwatengea watu wale!!
 
Huyo Saanane mambo ya Chadema tu yamemshinda sembuse mambo mengine ya juko nje. Kama ni mchambuaji mzuri aanzie na chadema kwanza. Kwa sababu huwezi.ukakimbilia kujenga masuala ya utaifa kwanza wakati masuala ya ndani tu yanatushinda
 
Aliingiziwa fedha zaidi ya Shilingi milioni 12 zilizoingizwa kwenye akaunti yake CRDB akaunti namba 01J1093293000 na ofisa wa ubalozi wa Algeria .Aache kupindisha tuhuma na kuimeza kiaina.Hajajibu tuhuma bado.

Ubalozi wa Canada na india anafanya nao kazi na taasisi mbili za kimarekani na Uingereza.
Kuna wajinga wanaweza kuuza nchi kwa pesa ndogo sana.
 
Mbona Ben sijaona halipojibu Hoja zile zaidi ya mipasho tu.. Zaidi ya kutafuta Kiki fake za ujasiri wa kukosoa upande ambao hayupo.. Ninaamin Ben anayaona kwa ukaribu zaidi mambo yanayo tokea Chadema kuliko yaliyopo ndani ya serikali.. Nilitegemea hawe mkosoaji mzuri sana ndani ya Chadema na kwa Mbowe kabla ya kutafuta Kiki huku nje..

Kama kweli anataka kubadili Tanzania, anatakiwa kuanzia nyumbani.. Chadema iwe safi.. Watu wawe safi.. Tuhamie nje huku.. Tutashirikiana kwa pamoja.. Sio tubague..


[HASHTAG]#ben saanane[/HASHTAG] na ujasiri fake
Mkuu...hapa hushangazwa sana pia na makamarade wenzetu wa shaksiya ya kiwango cha kina Komrade Ben S.....yale wanayoyasema wala hayastaajabishi...kabisa, kabisa, kabisa!
..kinachostaajabisha ni yale ambayo, yanastahili kusemwa, kutolewa ufafanuzi, kuyakiri ktk kweli yake, kunyamaziwa ...!
....namna hii, lazima tukiri kuwa harakati za kuinusuru, kuilinda, na kuiendeleza, Tanzania huru, (naam, Tanzania huru!) kwa kutegemea vijana wasomi wanasiasa,wakiwemo wenye upeo wa juu wa kiwango cha kina Ben, zimefitiniwa na fitna za kila aina! (Ukanda, ukabila, jinsia, udini, "utafutaji pesa", ukibaraka...nk....nk)
...lkn sawia na walivyonusurika kina Shadrack, Meshack, na Abednego wa ktk biblia, watanzania, wenye tafakari huru,na wanyoofu kiuadilifu, watanusurika (kwa maana halisi ya kunusurika!)
 
.....wajumbe, kwa mtu ambae nikifuatilia na nikiziunga mkono harakati za wana wa Sahara Magharibi, kupitia chama chao cha POLISARIO, hususan ktk kipindi kile cha harakati za kijeshi, nashuhudia kuwa mazingira ya kutafuta suluhu ya mgogoro ule yamebadilika mno!
...POLISARIO, inazungumza na mtawala wake...na yapo makubaliano ya aina fulani tayari, baina ya pande zinazohusika ktk mgogoro huo...msimamo wa nchi yetu ktk suala la mgogoro huo lazima uakisi hali halisi ya juhudi za kutafuta suluhu ya mgogoro huo, na si vinginezo...!
...tuhuma binafs kwa Comrade Ben, ni jambo lingine, lkn mtazamo wake (ye Ben), hasi dhidi ya Morocco kwa sbb tu ya nafasi yake ktk mgogoro wa Sahara Magharibi, ktk mazingira ya sasa, ukizingatia mahusiano, mazungumzo yanayoendelea baina ya pande zinazohusika na mgogoro huo, na hali halos iliyopo, ndani ya Uongozi wa POLISARIO ktk harakati zake za ukombozi( ambazo zimebaki kwenye meza ya mazungumzo), unakuwa "uko nyuma ya uhalisia " ya kile ambacho taifa letu linatakiwa kufanya...huu ni wakati stahiki kufungua mahusiano na Morocco, kwa ajili ya si sbb za kiuchumi tu, lkn pia kwa heri ya diplomasia ya kutafuta suluhu ya mgogoro huo...
Meza ya mazungumzo maana yake ni nini? Kwamba sasa Moroco wanaikalia Sahara Magharibi "kidogokidogo", au unalenga kusema kitu gani? Kwahiyo meza ya mazungumzo ina maana yoyote kuliko matokeo ya mazungumzo yenyewe? Au ndio maana mnasema hata Burundi wako katika meza ya mazungumzo kama ilivyokuwa Zanzibar ya Jecha?
 
Kuna mambo ya menivutia kwenye huu utetezi.

1. Anaye jitetea ni Saanane na mwenyekiti wa harakati ya sahara magharibi Shao.

2. Reference ya misimamo ni mwl Nyerere, ila alijutia kufanya biashara ya diamond na de-beer makaburu. Pamoja na kujutia si biashara ilifanyika?

3. Mchambuzi mkubwa hivi mpaka anapata consultancy haelewi kinachoendelezwa na watawala wa SA ya sasa tulivyo jinyima na kuacha fursa nyingi za taifa hili kwa ajili yao. Kweli nimeamini kunawatu wanatumia moyo kufikiri badala ya akili.

Na washawsha!
 
Aliingiziwa fedha zaidi ya Shilingi milioni 12 zilizoingizwa kwenye akaunti yake CRDB akaunti namba 01J1093293000 na ofisa wa ubalozi wa Algeria .Aache kupindisha tuhuma na kuimeza kiaina.Hajajibu tuhuma bado.

Ubalozi wa Canada na india anafanya nao kazi na taasisi mbili za kimarekani na Uingereza.
Algeria ina bifu na Morocco? Hawa wote sio waarabu na pia dhehebu lao ni suni?
 
Tuangalie pia Tanganyika na Zanzibar malalamiko tupu. pia mfn mzuri uchaguzi mkuu mwaka jana. .... Safari ni ndefu sana ya watu kuacha hili jitu linaitwa UNAFIKI.
 
Jamani mnamsingizia Ben Saanane, hana uwezo wa kuvuruga ziara yoyote! hata ya profesa Lipumba tu, kuhusu kutumika hiyo iko wazi kila siku anashinda mitandaoni kumtukana Magufuli kwa sababu ya hela mbuzi anayolipwa na chadema iliyonunuliwa na fisadi lowasana kuhusu kujifagilia kufanya consultancy labda anafanya consultancy ubalozi wa nyumba kumi [HASHTAG]#bensaananeAchaSiasaZaMajiTaka[/HASHTAG]
 
1478426127557.jpg
 
Meza ya mazungumzo maana yake ni nini? Kwamba sasa Moroco wanaikalia Sahara Magharibi "kidogokidogo", au unalenga kusema kitu gani? Kwahiyo meza ya mazungumzo ina maana yoyote kuliko matokeo ya mazungumzo yenyewe? Au ndio maana mnasema hata Burundi wako katika meza ya mazungumzo kama ilivyokuwa Zanzibar ya Jecha?
Punguza munkari, kisha fanya tafakari...wakielewana kama dalili zinavyojionesha?....kura ya maoni ikiangukia upande wa yale ambayo Morocco inayang'ang'ania?
....kuwa mhalisia kivitendo, leo hii unaisaidiaje Polisario, ktk harakati zake kivitendo, ktk mazingira ambayo harakati za kijeshi zimesimama, na wanazungumza?
....kisha siasa za Zanzibar, na Burundi, ulizoziingiza hapa, zinashabihiana kivipi?
...kwa wafuasi wa siasa koko za kukinzana ktk nchi yetu, inaelekea kuna upande unataka tumia suala la ziara ya mfalme wa Morocco, na mahusiano yanayoimarishwa kama bakora dhidi ya wapinzani wao...lkn bahati mbaya ktk hili hii bakora ni dhaifu kwenye mambo yao sawia na kutumia ubua mkavu wa mtama ulioliwa na mchwa, kumpigia mtu mzima...utaishia mtia vumbi na ubua kuvunjika..."hii ( ya Mgogoro wa Sahara magharibi) si silaha inayofaa ktk kukabiliana kwenye siasa zenu koko na za kujishusha" buddy!
 
Back
Top Bottom